Kocha wa Simba Benchikha awasilisha barua rasmi ya kuomba kuondoka mwishoni mwa msimu

Haya endeleeni kujifariji
Tujifariji kwani kafanya kipi cha maana Simba hadi aogopwe? Hata akibaki ni taarifa nzuri kwa Yanga kuendeleza ubabe kwenye ligi kuu na FA. Huyu kocha si ndiye aliyeifanya USMA ishike nafasi ya 12 kwenye msimamo wa ligi ya Algeria?
 
Simba ni ya benchika, mpk itakapo chukua ubingwa wa Africa msimu ujao ndo mtakubali, msichokijua ni kuwa benchika amekuja simba kimkakati na asingeweza kuchukua kombe coz simba ilikua mbovu, ngojeni dirisha la usajili lifunguliwe ndo muone.
Simba hii inahitaji kusajili wachezaji saba wenye viwango na kuacha wengine rundo. Msimu ujao haitakuwa na jipya.
 
Habari za uhakika ni kwamba yule Kocha aliyefeli vibaya simba kuliko makocha wote ameomba kuondoka simba ifikapo mwisho wa msimu.

Sababu ni kwamba Simba hawampi thamani pia haoni mipango yoyote ya Simba kusonga mbele badala yake wao Simba wanasonga ugali na dagaa Zanzibar.

Hata ningekuwa mimi, ningeomba kuondoka aisee! Timu gani hiyo inaamini tu kwenye ushirikina na pia kuwekeza kwenye mpira wa maneno zaidi, kuliko vitendo!
 
Baada ya Kuona anafundisha timu yenye wachezaji wenye vichwa vigumu kumuelewa hatimaye kocha la makombe limeamua litumie njia mbadala kujiondokea baada ya kudai linaondoka kutokana na matatizo ya KIFAMILIA🤣🤣

Ikumbukwe ni majuzi tu baada ya kutandikwa na yanga alikiri mwenyewe kuwa tokea aanze kudundisha soka ajawai kukutana na timu yenye wachezaji wenye vichwa vigumu kumuelewa Kama wa Simba, Sasa kaamua kuchomoka kiaina kaona CV inaporomoshwa kwa Kasi ya kimondo!
Hivi kibu , Saidoo, Shabalala wanacheza kwa kufata maelekezo ya mwalimu.
 
Tujifariji kwani kafanya kipi cha maana Simba hadi aogopwe? Hata akibaki ni taarifa nzuri kwa Yanga kuendeleza ubabe kwenye ligi kuu na FA. Huyu kocha si ndiye aliyeifanya USMA ishike nafasi ya 12 kwenye msimamo wa ligi ya Algeria?
Da mara anaharibu CV mara USMA 😁elimu elimu elimu.
 
Wachezaji wa Simba wanacheza tu bila fomesheni, hawana mipango ya kufunga magoli na hawana uchungu wa kuipigania brand yao. Kuna mechi Aziz Ki alitolewa nje akiwa benchi bado akawa anahamasisha na kufundisha wenzake waliobaki uwanjani. Kageuka kocha msaidizi!

Huyu Benchika ataenda atakuja kocha mwingine wachezaji wasipobadilika lori zima la makocha litaishia msimbazi!

Msimu ujao bado utakuwa wa Yanga kwakuwa Simba itakuwa ikijenga timu, mbumbumbu wanatakiwa kutuliza akili kusajili wachezaji wa matokeo sio majina. Mbangula mmoja tu beki wanne wa kolowizard wameshindwa kumkaba timu nzima uchochoro!!
 
Wachezaji wa Simba wanacheza tu bila fomesheni, hawana mipango ya kufunga magoli na hawana uchungu wa kuipigania brand yao. Kuna mechi Aziz Ki alitolewa nje akiwa benchi bado akawa anahamasisha na kufundisha wenzake waliobaki uwanjani. Kageuka kocha msaidizi!

Huyu Benchika ataenda atakuja kocha mwingine wachezaji wasipobadilika lori zima la makocha litaishia msimbazi!

Msimu ujao bado utakuwa wa Yanga kwakuwa Simba itakuwa ikijenga timu, mbumbumbu wanatakiwa kutuliza akili kusajili wachezaji wa matokeo sio majina. Mbangula mmoja tu beki wanne wa kolowizard wameshindwa kumkaba timu nzima uchochoro!!
 
Habari za uhakika ni kwamba yule Kocha aliyefeli vibaya simba kuliko makocha wote ameomba kuondoka simba ifikapo mwisho wa msimu.

Sababu ni kwamba Simba hawampi thamani pia haoni mipango yoyote ya Simba kusonga mbele badala yake wao Simba wanasonga ugali na dagaa Zanzibar.

Swali fikirishi je anamaanisha familia ya Simba? Hapa tumieni akili mnembo
 
Hakuna kocha mwenye heshima yake akakubali timu inachezeshwa ndondo kati kati ya ligi
 
Back
Top Bottom