Tunadhani hii case closed!
Wengi ndani na nje ya CCM mmekuwa mkihoji kwa nini Mwenezi wa CCM Paul Makonda amekuwa akifanya ziara na misafara mirefu kuliko hata PM na Naibu PM.
Katika ziara zake amekuwa akisikiliza kero za wananchi na kuwapigia simu papo kwa papo Waziri au Mkurugenzi na kutoa...
Labda ipo njia ya kistaarabu zaidi ya kuandika haya mambo. Tunashangazwa wote nadhani katika haya maneno yanayosemwa kati ya Katibu Mwenezi Makonda na Waziri Bashe. Na pia wapo wengine.
Haya ni mambo mabaya. Kama Mbunge Gwajima alivyokuwa anasema jana kwamba mtoto wa tajiri wa Unguja alitoweka...
Katika watu wanaopaswa kutii sheria za barabarani ni Watu hawa, Majaji, Jeshi, Viongozi wa serikali, ila katika nchi yetu hii ipo tofauti sana, yan wanaongoza kuvunja sheria mnoo, bila hata sababu za msingi, na hata zingekwepo hawakupaswa kuvunja sheria.
Unakuta wanapita Njia ya magari ya...
Ni kawaida kwamba katika nchi nyingi matajiri wakubwa utakuta ni wafanya biashara, lakini sio Tanzania. Kwa sasa wanaoongoza kwa kuwa matajiri wakubwa Tanzania ni wanasiasa waliopo madarakani au waliokuwa madarakani huko nyuma. Halafu wanafuatiwa na viongozi wa serikali, pamoja na ndugu zao...
Taarifa ikufikie popote ulipo kwamba, Katibu wa TEC Padri Kitima, leo 8/01/2024 Ametoa maoni ya Baraza la Maaskofu wa Kikatoliki ndani ya Bunge la Tanzania, kama Mchango wa Kanisa hilo kwenye Miswada ya Sheria za Uchaguzi.
TEC imesema kwamba Viongozi wa Serikali hawapaswi na iwe mwiko kwao...
Makamu mwenyekiti wa CCM Tanzania bara ndugu Abdulrahaman Kinana amekemea baadhi ya viongozi wa CCM wanaowadhalilisha viongozi na watendaji wa serikali hadharani.
Kinana amesema badala yake wanatakiwa kutumia vikao halali vya chama kufikisha ujumbe wao.
Jiwe hili limerushwa.
Wakati wa majanga kumekuwepo na kasumba viongozi kutangulia na makamera yao wakielekeza wataalam namna ya kufanya uokoaji!
Hii haina afya kabisa!
Kwa waliosomea elimu ya majanga watanielewa!
Wakati wa majanga ingekuwa vyema zaidi wataalam wetu wangepewa nafasi ya kuonesha utaalam wao...
Ofisi ya Tais Tamisemi ina viongozi kama ngozi, kazi yao kulinda maslah ya wajuu yao. Ngozi kazi yake kubwa ni kukinga, hicho ndicho wanachokifanya watu wa Tamisemi.
Ukiangalia idara za afya , elimu, ujenzi nk kazi yao ni kuweka limit nothing more than just keeping and helping leaders...
Siku hizi mjini Kuna kasumba ya viongozi wetu wanasiasa, kazi Yao ni kukera wananchi. Nasikitiswa na hivyo vitendo wanavyovifanya.
Kuna serikali ya awamu ya Nne, Tano na Sita. Asilimia 98 ya watendaji ni wale wale, yaani ndio waliotenda hizo awamu zote. Lakini kinachosikitishwa ni kuwa madudu...
MASIKINI ATABAKI KUWA MASIKINI na tajiri atatajirika zaidi aliimba msanii Jaguar toka Kenya. Msemo huu unaonekana kukita mzizi nchini Tanzania.
Tanzania inatumia bilioni 558 kwa mwaka kununua magari ya viongozi! Hatujapigia mahesabu gharama za vipuri,matengenezo na mafuta ya bure wanayopewa...
Serikali inategemea kufanya mabadiliko makubwa kiutendaji hivi karibuni; mabadiliko hayo yataenda sambamba na kuwafuta kazi baadhi ya viongozi waliokwama kufanya kwa ueledi na viongozi wa vyombo vya dola. Lengo ni kuleta sura mpya za vijana watakaozitafsiri kwa vitendo 4R za Mhe.Rais
Sambamba...
Nimeona clip ya Nape Nauye akifoka na kumwambia Tundu Lissu amuheshimu Rais Samia kwa kuwa ni mama yake. Sawa hatukatai kuwa kila mtu anastahili heshima na si viongozi tu wa serikali na kisiasa.
Kosa kubwa ni pale machawa wa viongozi wanataka chawa wao wasikosolewe wala kofokewa wanapofanya...
Wakati mwingine nahisi kukasirika! Hivi ni kweli viongozi wetu wanachukizwa na umaskini uliopo nchini?
Angalia posho wanazolipana! Zinaendana na hali ya kiuchumi ya nchi?
Angalia magari ya anasa wanayoyanunua kwa ajili ya matumizi ya watumishi wa Serikali! Wangeyanunuua kama wangetakiwa...
Mfumo wa uteuzi wa viongozi wa serikali umekuwa na changamoto kubwa nchini kwetu. Mara nyingi, uteuzi hufanywa kwa misingi ya uhusiano wa kisiasa au urafiki badala ya uwezo na uzoefu wa mgombea. Hii imepelekea kuwepo kwa viongozi wasio na uwezo wa kusimamia vizuri masuala ya umma na kusababisha...
Katika nyanja ya Uongozi, kumekuwa na changamoto kubwa katika mfumo wa uteuzi wa viongozi wa serikali. Mara nyingi, uteuzi hufanywa kwa misingi ya uhusiano wa kisiasa au urafiki badala ya uwezo na uzoefu wa mgombea. Hii imepelekea kuwepo kwa viongozi wasio na uwezo wa kusimamia vizuri masuala ya...
Ninafuatilia kwenye runinga tukio la kuuaga mwili wa aliyekuwa mtumishi wa serikali na mwanadiplomasia mbobezi ndg Bernard Membe.
Ninawiwa kuwaasa viongozi wetu wa serikali, bunge na mahakama mliopewa dhamana ya kulitumikia taifa letu, kulitazama jeneza la aliyekuwa kiongozi kama ninyi mlivyo...
Ripoti ya Wataalamu wa Haki za Binadamu kutoka Umoja wa Mataifa (UN) imebaini baadhi ya Maafisa wa Serikali ya Sudan Kusini wamekuwa wakifanya Unyanyasaji Mkubwa dhidi ya Raia ikiwemo Kushambulia, Kujeruhi, Kuua na Ubakaji.
Pia, Ripoti imesema Serikali haijaonesha kuweka uzito katika kudhibiti...
Yaan ina tia hasira na pia inahuzinisha, mnashindwa ingia ubia na wamiliki wa Ccm wanaomiliki viwanja vingi mapato yakaenda halmashauri kwenye mgawanyo? hao waarabu wanaotunyanyasa ubora wa viwanja vyao unachangia.
Huku mnaweza fanya kitu kizur kikatutambulisha watanzania. Hata mashindano yenu...
Rais Samia Suluhu Hassan amewataka viongozi wa Serikali kujitathmini kwa nafasi zao kama wana maadili ya uongozi.
Rais Samia amezungumza hayo alipofanya mkutano wa faragha wa Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa Arusha (AICC)...
Imekuwa kawaida kipindi cha Mfungo wa ramadhani viongozi wa serikali, taasisi mbalimbali za serikali na binafsi kufuturisha.
Sasa basi ili kuondoa dhana ya upendeleo au double standard ni vyema basi katika kipindi hiki cha Mfungo wa Kwaresma basi futari ikaandaliwa pia na taasisi hizo.
Ni...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.