singanojr
JF-Expert Member
- Sep 24, 2020
- 1,525
- 8,547
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA SITA
Najma alimwangalia Roma aliekuwa na Begi lake mgongoni na kumfanya taswira ya miezi sita nyuma ijijenge katika kichwa chake , alikumbuka siku ambayo alimpokea Roma alikuwa amebeba begi hilo hilo utofauti wa leo ni kwamba Roma alikuwa kwenye mavazi mazuri kuliko kipindi kilichopita.
“Kaka anaroho mbaya ni kweli kamfukuza Roma kama alivyosema”
Najma alimwangalia Roma kwa uso uliojaa maswali mengi , huku akiwaza moja kwa moja kuwa Juma atakuwa amemfukuza Roma na sasa Roma alikuwa akiondoka kwenda kupanga kwingine.
“Najma naomba tuongee kabla sijaondoka”
“Juma naomba niongee na Najma , sitaki kuacha deni nyuma”Aliongea Roma na Juma alitikia kwa kutingisha kichwa huku akiwaacha.
“Jana ulikuwa wapi Roma , Nisamehe kaka yangu kachukua maamuzi ya kukufukuza”
“Nifate Najma nje tukaongee”aliongea Roma huku akitangulia na Najma alitangulia , ila Najma alishangaa pale alipomuona Roma akifungua mlango wa gari ya kifahari ambayo hakuwahi kuwaza mtu kama Roma anaweza kuinunua , ghafla yale mawazo aliokuwa nayo juu ya Roma kuwa mtu mkubwa aliekuwa akijifanyisha masikini yalianza kurudi upya , ila kwake hakuwa na shida , aliingia ndani ya gari kwa kusitasita.
“Hii gari umeitoa wapi Roma , ni nzuri mno nitakuja kununua yangu kama hii”Aliongea Najma na kumfanya Roma Atoe tabasamu lililojaa uchungu moyoni mwake kwani aliamini taarifa anayokwenda kumwambia mwanadada huyu itamwachia machungu mengi moyoni.
“Najma naomba unisikilize jambo ninalokuambia, na pia nitaomba unisamehe kama nitakukwaza na kukuumiza , ila sitaki kukuficha ukweli wote Najma”Aliongea Roma na kumfanya Mrembo huyu amwangalie.
“Usijali wewe niambie tu Roma nipo tayari kusikilia lolote ili mradi liwe jambo la ukweli”Roma alivuta pumzi na kukusanya ujasiri aliokuwa nao ndani yake .
“Jana nimefanikiwa kukutana na mwanamke niliepotezana nae kwa miaka mingi ambaye nilidhania amefariki na baada ya kuonana tumefunga ndoa rasmi na unavyoniona hapa mimi ni mume wa mtu , najua ni kiasi gani unanipenda Najma na ndio maana siku zote nilikuwa nikijizuia kutokuzikubali hisia zako….”Roma kabla hata hajamaliza mlango wa gari ulifunguliwa na Najma alitoka na kukimbilia ndani kwao hakutaka tena kusikiliza maneno ya Roma,
Roma alibaki akiwa hajui ni kipi afanye , lakini hakuwa na jinsi , ili mradi ashauweka wazi ukweli wote mbele ya Najma, basi aliona ni vyema kwa mwanadada huyo kumsahau kaika maisha yake.
****
Ni muda wa Asubuhi ndani ya jengo la Club B, katika chumba ambacho kilikuwa ni ofisi ya mwanadada mrembo maarufu ndani ya eneo hili la Chalambe Maji matitu , alionekana Rose akiwa amekaa kwenye kiti chake cha kuzunguka huku mbele yake kukiwa na tarakishi kubwa iliokuwa imewashwa , huku mwanadada huyu akionekana kusoma taarifa iliokuwa kwenye mfumo wa Softcopy.
Ofisi yake ilikuwa ni kubwa , iliokua imependezeshwa na samani za bei ya juu kuonesha kuwa mwanadada huyu hakuwa vibaya kwenye swala la kifedha na kwa namna alivyokuwa amevaa na namna ambavyo alikuwa kaitumia Tarakishi hio alionekana kuwa Profesheno.
Baada ya dakika kadhaa za kukaa hapo ndani , mlango wake uligongwa na akaingia kijana mmoja alievalia suti na miwani ya jua akiwa na kipara kilichokuwa kinang`aa , bwana huyu alionekana kuwa ni wale vijana waliokuwa wakifanya mazoezi.
“Niambie Zonga unataarifa gani?”
“Madam taarifa niliokuwa nayo ni kwamba Roma kapata mke”
“Unamaanisha nini?”
“Kwa taarifa nilizokuwa nazo sasa Roma kafunga ndoa jana na leo amekuja sehemu anayoishi na kuchukua mizigo yake na kuhamia kwa mke wake”Maneno ya Zonga yalikuwa kama kisu cha moto kilichokuwa kikipita katika moyo wa mwanadada huyu.
“Bosi..!”Aliita zonga mara baada ya kumuona bosi wake akitoa machozi, na Rose aliyafuta haraka haraka na kisha aliachia tabasamu la ujasiri.
“Endelea kufatilia ni mwanamke gani Roma kamuoa” Aliongea Rose na Zonga alitoka
“Huyu fala ana nyota bwana , yaani mrembo kama bosi anatoa machozi kwa ajili ya fala mbeba mizigo , huyu jamaa ana nini mimi sina” Alijiongelesha Zonga ndani ya moyo wake huku akitoka ne ya ofisi.
Rose alisimama na kusogelea dirisha na kuangalia baadhi ya watu waliokuwa kwenye pilikapilika za kutafuta maisha huku akionekana ni mwenye mawazo sana huku akijizuia kulia.
“Stori yetu haiwezi kuisha hivi Roma ,Siku ulionikoa kwenye mikono ya baba yangu ndio ulikuwa mwanzo wa stori yetu na haikuwa bahati mbaya hata kidogo , nimetumia pesa nyingi sana kukutafuta na mpaka kukupata , siwezi kukuachia kirahisi” Alijiongelesha Rose.
****
Roma hakujali sana , aliendesha gari lake mpaka Kigamboni na kupokelewa na Bi Wema kwani mke wake hakuwa amerudi kutoka kazini, baada ya kuweka lile begi , alitoka nje na kuzunguka upande wa Yard ya magari huku mkononi akiwa ameshikilia kile kiboksi alicho toka nacho Mbagala , aliangalia sehemu ya kificha kiboksi hiko , lakini hakupata na mara akapata wazo na kuondoka ndani ya eneo hilo na kuingia chumba cha mazezi , aliangalia sehemu rahisi ya kuhifadhi kiboksi hicho , na alifanikiwa kupaona na kisha alikiweka vizuri na kuziba na kisha alitoka nje.
Baada ya kurudi ndani kwenye chumba chake aliwasha tarakishi na kisha akaingia kwenye mtandao na kuangalia namna ya kupata kazi , bahati nzuri , aliona baadhi ya makampuni mbalimbali yaliokuwa yakitangaza ajira , alichagua kazi aliona inafaa na kisha aliandika CV yake na kuituma pamoja na vivuli vya vyeti ambavyo alivitoa kwenye akaunti ya Barua Pepe yake , aliomba kwenye kampuni tatu harakaharaka na kisha alijilaza kitandani , lakini hakukaa muda mrefu , aliitwa na Bi wema na kuambiwa chakula tayari ashuke wakale.
Roma baada ya kula chakula kitamu kilichokuwa kimeandaliwa na Bi Wema , alirudi chumbani kwake huku kwenye kichwa cheke akiwa na mpango wa kwenda kupiga misele mjini maana alikuwa na kiasi cha pesa kilichokuwa kikimruhusu kufanya hivyo.
Alijiandaa haraka haraka, kwa kuvalia tisheti yake iliomtoa vyema na Jeans pamoja na Raba kisha alichukua ufunguo wa gari na kumuaga Bi Wema na kisha alitoa gari nduki.
Masaa machache tu alikuja kuonekana akiwa maeneo ya Posta kwenye moja ya saluni ya kisasa maarufu ,aliegesha gari yake kwa ustadi mkubwa huku waliokuwa karibu na eneo hilo wakiliangalia gari lake kwa matamanio.
Roma hakujali sana , alitoka kwenye gari na kisha aliingia ndani ya saluni hii ya kiume kwa ajili ya kutengenezwa nywele zake kitendo ambacho kilifanyika kwa muda mfupi sana , baada ya kupendeza kwa staili aliokuwa anataka yeye , aliendesha gari yake kuelekea upande wa Ocean road.
Muda wa saa kumi na mbili ndio muda ambao Roma alikuwa anarudi na sasa alikuwa anaingiza gari yake ndani ya jumba lao la kifahari , lakini ile anaingia aliona gari ambayo kwa haraka haraka alijua sio gari ya Edna , aliamini kulikuwa na ugeni ila hakujua ni ugeni wa mtu gani , ila aliamini kwakuwa ashafika , basi majibu ya maswali yake yatajibiwa akiingia ndani.
Baada ya kuingia ndani ni kweli aliona mwanaume mmoja ambae baada ya kumwangalia sura yake ilikuwa inakuja hivi na kupotea , mwanaume huyu hakuwa peke yake bali na mke wake alikuwepo.
“My Wife Am back!”Aliongea Roma na kumfanya kijana aliekuwa amekaa kwenye sofa amwangalie huku akionyesha chuki ya waziwazi na Roma aliliona hilo na kwakua alikuwa sio mtu wa kujali sana alisogea upande wa kushoto alipokuwa mke wake na kumbusu shavuni , kitendo ambacho Edna hakuzuia na Roma aligundua jambo pia kwa mara ya pili.
“Babe huyu ni nani?”
“Anaitwa Abubakari ni mwanaume ambaye nilikuwa nikikuambia”.
“Oooh ! unamaanisha yule mwanaume ambaye humpendi ndio huyu bwana”.
Maneno hayo yalimkera mno Abuu ila alijitahidi kujizuia mbele ya Edna.
“Braza vipi mimi ni Roma , ni mume wa Edna nimesikia habari nyingi juu ya kumsumbua mke wangu hivyo braza kaa mbali na mke wangu ama nitakufanya jambo baya”Aliongea Roma na kumfanya Abuu atabasamu kifedhuli.
“Wewe mbeba mizigo utanifanya nini labda.. usifikiri nimekaa kimya ukajua nakuogopa Edna ni wangu wewe ni wakuja tu na muda wowote utaondoka na kuurudia umasikini wak..”Ilikuwa ni kitendo cha haraka sana ambacho Roma alikifanya kwani kabla ya Abuu hajamaliza kuongea alikuwa hewani akining`inia kwenye mkono wa Roma,bwana huyu alikuwa akivuta pumzi kwa shida huku akijaribu kuongea neno lakini ni kama Roma hakujali na nia ya kumuua bwana huyu ilionekana waziwazi kwenye macho ya Roma.
“Roma Stoop..!!”Ilikuwa ni sauti ya kitetemeshi ya Edna iliomfanya Roma amtupe Abubakari chini kama furushi.
“Nikihesabu mpaka nne bado upo hapa ndani nakuaa .. moja,, mbili .. tatu..” Lakini kabla hajamaliza Abuu alisimama na kumwangalia Roma kwa macho makali na kisha alitoka huku akishika shingo yake, na hii ni baada ya kuona kuwa Roma hakuwa akitania kwani macho yake yalikuwa yamejaa hasira kali kiasi kwamba alionekana kuwa tayari kwa kuua muda wowote.
Upande wa Edna alishangazwa na uwezo wa nguvu aliokuwa nao Roma, namna ambavyo Roma alimning`iza hewani Abuu kilimuogopesha na kumuacha kwenye maswali.
“Mbona haupo makini Roma , unajitafutia matatizo , unajua nguvu iliokuwepo nyuma ya Abuu wewe?”
“Kwa hio kukiwa na nguvu kubwa nyuma yake nimuogope na akikanyaga mguu wake hapa tena namuua..”Aliongea Roma huku kiini cha macho yake kilichokuwa kimebadilika rangi kuwa kijani kilirudi na kuwa kama kawaida na kutokana na hasira alizokuwa nazo Roma hakutaka kubaki hapo sebuleni na kupandisha ngazi kwenda chumbani kwake na kufunga mlango kwa nguvu , huku akimuacha Edna aliekuwa akimwangalia kwa wasiwasi mkubwa.
Baada ya Roma kuingia kwenye chumba chake moja kwa moja alienda kuoga huku akituliza hasira zake, baada ya kujiona yupo sawa alisogelea Laptop yake na ile anaiwasha aliona ‘Notification’ kwenye barua pepe ikionesha kuna ujumbe , alifungua na kukuta kuna jumbe tatu.
“Mr Roma Ramoni we are happy to inform you that tomorrow we would like to do an interview with you regarding the job request you submitted to us , it will be our honor to see you tomorrow at xxx time”
“Ndugu Roma tunafuraha kukuambia kwamba tunapenda kufanya usaili na wewe kesho kulingana na ombi la kazi uliloliwasilisha kwetu , itakuwa heshima kwetu kama tutakuona kesho”.
Alifungua meseji ya pili na kisha akasoma.
“Hellow Mr Roma Ramoni we reviewed your job Request and your Credential’s that you submitted to us and confirmed they are Valid,We are replaying back to inform you to attend interview tomorrow morning at xxx time”
Karibia kampuni zote tatu zilikuwa zimerudhisha majibu ya kumtaka Roma kwenda kwenye interview siku ya kesho , alitabasamu na kuona kumbe kutafuta kazi ni rahisi hivyo, lakini licha ya majibu hayo alipanga kwenda kwenye kampuni moja tu na hivyo alitakiwa kuchagua kamouni moja ya kwenda kwa siku ya kesho.
“Vexto Group of Companies ndio moja ya kampuni ambayo Roma alidhamiria kwenda kufanya usaili kesho , kilichomvutia kuhusu hii kampuni kwanza ilikuwa ni kampuni kubwa sana ndani ya Afrika Mashariki na Kati yote ambayo ilikuwa inaendeshwa kwa thamani ya pesa kiasi cha Dola bilioni ishirini, Pili makao makuu ya kampuni hii yalikuwa makao makuu ya kampuni ya mavazi na mitindo ifahamikayo kwa jina la E- Styllus Wear , kampuni ambayo ilikuwa ikiaminika kwa kuwa na warembo wakali.
“Hii ndio kampuni nzuri , nitakutana na warembo wengi”
SEHEMU YA SABA
Muda wa saa mbili kamili za usiku Roma alishuka kwa ajili ya chakula , chakula ambacho alikula kama alikuwa na njaa ya wiki nzima , kwani alimaliza kalibia chakula chote kilichokuwa kwenye mabakuli.
Edna aliishia kujisemea kuwa Roma hakuwa ni mwenye aibu hata kidogo kwa upande wa Bi Wema alifurahishwa sana na uwezo wa kula wa Roma.
“Bebi Edna kesho naenda kwenye usaili”
“Sawa mafanikio mema”Aliongea Edna huku akinyanyuka na kutoa vyombo na baada ya kumaliza alipandisha ngazi na kwenda chumbani kwake , upande wa Roma hakuwa na mudi ya kubaki ndani hapo kwani alitoka na funguo zake na kuondoka.
Nusu saa mbele alikuwa alikuwa akiingia Chalambe Mbagala katika Rango kubwa la Club B, aliegesha gari lake na kuingia ndani huku akikutana na watu waliokuwa wamechangamka.
Zonga ndio mtu wa kwanza kumuona Roma, na alimsogelea kisha akamkaribisha kwa bashasha.
“Rose yuko wapi?”
“Madam Boss yupo ofisini kwake , itakuwa vyema kama utaenda kumuona”Aliongea Zonga na Roma alichukua upande ambao ofisi ya Rose ilikuwepo , alifungua mlango bila kugonga na kuingia ndani na kumkuta Rose aliekuwa amejiegamiza kwenye masofa huku pembeni kukiwa na chupa kibao za bia.
“Romaaa!”Aliongea Rose huku akinyanyuka na kivivu na kumsogelea kisha akamkumbatia huku machozi yakiwa yanamtoka , alianza kulia kwa kwikwi kiasi ambacho kilimshangaza Roma.
“Roma kwanini hukuniambia unamwanamke mpaka unaniumiza kiasi hiki”Aliongea Rose na kumfanya Roma atambue Rose anataarifa za yeye kuoa , Roma hakutaka kuongea chochote Zaidi ya kumtoa kifuani na kumwangalia usoni na kuona uso wa mrembo huyu ulivyokuwa kwenye majonzi , alisogeza mdomo wake na kugusisha na mdomo wa Rose na mwanamke hakuleta shida kwani aliupokea kwa pupa na walianza kukiss huku hisia zikiwa zinaongezeka kila baada ya sekunde
Ni ndani ya robo saa mbele Rose na Roma walionekana ndani ya kitanda kilichokuwa ndani ya ofisi hii ya Rose , huku mwanadada huyu akitoa miguno ambayo ilimfanya Roma kuongeza spidi ya kupiga kiuno.
Mchezo ulichukua Zaidi ya dakika tisini mpaka pale ambapo Roma aliweza kutua mzigo wake huku akiwa ni mwenye kuhema kwa nguvu , lakini kwa upande wa Rose akionekana akiwa hoi,Roma alimwangalia mwanadada huyu na kuona alikuwa kwenye maumivu na yote hio ni mara baada ya kugundua kuwa Rose alikuwa Bikra , jambo hili lilimshangaza.
“Twende nyumbani kwako , nitalala huko”Aliongea Roma na Rose alitingisha kichwa na walikokotana kwamlango tofauti na ule wa Bar na kisha Roma alimpandisha Rose kwenye Gari na kuondoka.
Sehemu aliokuwa akiishi Rose ni hapo hapo kwani walichukua dakika mbili kufika ndani ya Jumba la Kifahari la mwanadada huyu.
Roma alimsaidia Rose kwa kumkanda sehemu zake za siri ili kupoza maumivu na kisha waliingia kwenye shuka na kukumbatiana.
“Masikini nimeshakuwa mchepuko”
“Ndio huo ndio uhalisia unaopaswa ukubali , lakini sitokulazimisha kuendelea na mimi”
“Siwezi Roma nipo tayari kuwa mchepuko wako ila sio kukukosa kabisa”
Roma hakuongea kitu Zaidi ya kumkumbatia Rose huku akitabasamu.
“Mke hatanuna ukilala kwangu?”
“Hilo lisikusumbue mrembo eh , au unataka niondoke”
“Hapana nimeongea tu baba usiondoke”
“Saa moja kamili Roma aliamka na kuanza kumpapasa Rose ambaye alimpa ushirikiano wa kutosha na ndani ya dakika kadhaa mbele walipiga cha asubuhi na Roma akaingia bafuni na kumuaga Rose kwa kumuambia kuwa alikuwa na Usalili na kampuni
“Karibu nyumbani Mr Roma”Aliongea Bi wema baada ya kumuona Roma akiingia sebuleni , na wakati huu Bi wema alikuwa na Edna mezani wakinywa chai ya Asubuhi.
Roma alisalimia , huku akiliwa buyu na Mke wake wala hakujali na kukaa mezani na kujisevia msosi na kuanza kula kama hana akili nzuri , hakujali macho mabaya ya Edna.
“Bi Wema Asante kwa chai nzito , mimi ngoja nikajiandae kwa ajili ya kwenda kwenye usaili”.
“Bebi Edna niweke mume wako kwenye maombi nipate kazi”Aliongea Roma na bila hata ya kusubiri jibu alipandisha ngazi kuelekea kwenye chumba chake.
Ni muda waa saa tatu na nusu Roma aliegesha gari yake sehemu maalumu ndani ya jengo hili refu lililokkuwa likipatikana ndani ya Posta mtaa wa Samora , baada ya kutoka kwenye gari moja kwa moja alienda mapokezi na kujieleza kwa mwanadada mmoja mrembo huku akiwa ni mwenye kushangazwa na uzuri wa kila mfanyakazi wa kampuni hii.
“Hii sehemu ni sahihi kabisa kwangu”Alijiongelesha Roma huku akimkonyeza mrembo Mmoja aliekuwa eneo la mapokezi na mrembo huyo alitabasamu na kisha kumpita Roma .
Roma alishangazwa na watu waliokuwa wamekuja kwa ajili ya usahili kwani wote walikuwa ni wanawake tena warembo huku mwanaume aliemuona hapo ndani ni mmoja tu , tena ni jamaa mmoja hivi kibonge.
“Hey Boy na wewe umekuja kwenye usaili?”
“Ndio kaka , vipi wewe?”
“Hata mimi pia ,niite Jacob”
“Namini niite Roma”
“Sasa Roma wewe nini kimekuvutia kuja kuomba kazi hapa?”
“Sababu kubwa mimi ya kuja kuomba kazi hapa ni Warembo , nasikia hii kampuni ina mapini sio mchezo”
“Kaka nadhani umejionea mwenyewe ni kweli hii kampuni imejaa warembo”
“Vipi wewe?”
“Mimi sababu kubwa sio warembo ila kuna mrembo mmoja ndio amenifanya kuja kufanya kazi hapa”
“Yupi huyo”
“CEO”
“Unamaanisha CEO wa hii kampuni ni mwanamke na ni mrembo pia?”
“kaka ndani ya hii kampuni hakuna anaemfikia kwa uzuri CEO , kama huamini uliza uambiwe”Aliongea Kibonge
Wakati Roma na kibonge wanaongea , kibonge zamu yake ilifikia na kuingia kwenye chumba cha usaili na baada kama ya nusu saa alitoka huku akionekana kama mtu aliekosa tumaini.
“Vipi kaka mbona hivyo”
“Nimeulizwa maswali yote nimeshindwa kujibu sina ninalojua , ndoto yangu ya kuwa karibu na CEO imekufa kila la kheri kaka”Aliongea Kibongea na wakati huo huo Roma alisikia jina lake na kusogelea mlango na kuingia .
Ile anaingia tu alijikuta akipokewa na sura mbili anazozifahamu na sura moja asioifahamu , jumla ya wasaili walikuwa watatu , mtu wa kwanza Roma alimkumbuka vyema kwa urembo wake , lakini sio hivyo tu pia alimkumbuka kwa kumsaidia Shilingi Elfu tano siku ambayo aliachwa njiani na mke wake Edna, Mrembo yule msaili pia alimkumbuka vyema Roma na kujikuta akitabasamu mara baada ya kukutanisha nae macho,Siura ya pili Roma kuifahamu ni mdada alipishana nae Mapokezi , huyu ni mrembo aliemkonyeza.
“MisterRoma Ramoni nini kimekuvutia mpaka ukaomba kufanya kazi na sisi??”Aliuliza mrembo wa Buku tano.
“Kilichonivutia kwakweli si kingine Zaidi ya warembo, napenda kufanya kazi kwenye mazingira ambayo nazungukwa na warembo”Alijibu Roma kwa kujiamini na kuwafanya wasaili waangaliane na kutabasamu.
“Okey Mr Ramoni kwenye CV yako ulioanisha kwamba unajua kuzungumza Lugha za mataifa mbalimbali Zaidi ya kumi jambo ambalo tunamashaka nalo licha ya kwamba vyeti vyako vinaonesha una Masters ya uongozi wa biashara kutoka chuo cha Harvard , hivyo basi tumekuandalia maneno kumi ya lugha tofauti tofauti unazojua ili utuambie maana ya hayo maneno”
“Hakuna shida hilo ni rahisi sana kwangu”Aliongea Roma na kisha yule dada wa Mapokezi alionyesha maneno hayo kwa kutumia tarakishi na projekta na Roma alianza kusoma maneno hayo.
Yalianza kuonekana maneno ya kijerumani na Roma aliyasoma na kuyatolea tafsiri na wale walithibitisha ni sahihi , ikaja lugha ya kiarabu nayo hivyo hivyo , ikaja lugha ya kireno ikawa hivyo hivyo , ikaja kifaransa , kikorea , kichina Kinyarwanda …
Wasaili hawa walishangazwa mno na uwezo wa Roma , hawakuwahi kukutana na mtu ambae anajua Lugha nyingi kama Roma ..
Roma aliulizwa maswali mengi mengi na kuyajibu kiufasaha na wasaili wakakubaliana kumpa kazi Roma katika kitengo cha Public Relation.
“Karibu Vexto Roma, kwa kupata kwako kazi naamini Mke hatakuacha njiani tena mpaka kukosa nauli”Aliongea mwanadada yule msaili huku akitabasamu.
“Asante sana”
“Naitwa Doris Alex afisa mwajiri mkuu wa kampuni”.
“Nafurahi kufahamina na mrembo kama wewe Doris”Aliongea Roma na kumfanya mwanadada huyu kutabasamu na kufanya mashavu yake kuacha vishimo(Dimples)
“Naomba nichukue fursa hii kukuonesha baadhi ya maeneo ya kampuni kabla hatujaanza kazi rasmi”Aliongea Doris na Roma alitingisha kichwa na wote wakaingia kwenye Lift , Roma muda wote tabasamu halikuwa likimwishia usoni , alijiona kama vile yupo kwenye mbingu ya warembo, mrembo Dorisi alikuwa amempagawisha mno.
“Hii ndio Floor ambayo viongozi wa juu ya kampuni ofisi zao zipo , hii ni ofisi ya mhasibu mkuu wa makampuni ya Vexto , hii ni ofisi yangu”Huku wakiingia na Roma aliisifia ofisi ya Doris.
Wakati Dorisi akiendelea kumpa shule Roma mara simu ya ofisi yake ilitoa mlio kuashiria inaita , alipokea na kuweka sikioni na kisha akashusha mkonga.
“Unaonekana kuwa na bahati sana Roma,CEO anataka kuonana na wewe jambo ambalo sio la kawaida”Aliongea Doris na alimpeleka mpaka kwenye mlango wa ofisi uliojitenga na kisha alifungua na kukutana na sekretari alimchangamkia na kumkaribisha , Sekretari alikuwa wakawaida sana , hakuwa mrembo sana.
“Boss! Mr Ramoni has arrived”Aliongea Sekretari
“Let him in”
“You may go in na tafadhari hakikisha unakuwa na heshima mbele ya bosi , sio mtu ambaye kila mtu anaweza kuingia kwenye ofisi yake”Aliongea mwanadada huyu na Roma aliingia ndani ya ofisi hio kubwa huku akiwa na tabasamu la kukutana na CEO mrembo maana kwenye kichwa cheka alikuwa akikumbuka maneno ya Kibonge aliekuja nae kufanya usaili muda mfupi uliopita.
“Akinivutia namtongoza ,CEO kitu gani bwana”aliwaza
Roma alijikuta akipagawa baada ya kumuona mtu ambae hakumtegemea kuwa ndio CEO”
ITAENDELEA JUMATATU WADAU
Najma alimwangalia Roma aliekuwa na Begi lake mgongoni na kumfanya taswira ya miezi sita nyuma ijijenge katika kichwa chake , alikumbuka siku ambayo alimpokea Roma alikuwa amebeba begi hilo hilo utofauti wa leo ni kwamba Roma alikuwa kwenye mavazi mazuri kuliko kipindi kilichopita.
“Kaka anaroho mbaya ni kweli kamfukuza Roma kama alivyosema”
Najma alimwangalia Roma kwa uso uliojaa maswali mengi , huku akiwaza moja kwa moja kuwa Juma atakuwa amemfukuza Roma na sasa Roma alikuwa akiondoka kwenda kupanga kwingine.
“Najma naomba tuongee kabla sijaondoka”
“Juma naomba niongee na Najma , sitaki kuacha deni nyuma”Aliongea Roma na Juma alitikia kwa kutingisha kichwa huku akiwaacha.
“Jana ulikuwa wapi Roma , Nisamehe kaka yangu kachukua maamuzi ya kukufukuza”
“Nifate Najma nje tukaongee”aliongea Roma huku akitangulia na Najma alitangulia , ila Najma alishangaa pale alipomuona Roma akifungua mlango wa gari ya kifahari ambayo hakuwahi kuwaza mtu kama Roma anaweza kuinunua , ghafla yale mawazo aliokuwa nayo juu ya Roma kuwa mtu mkubwa aliekuwa akijifanyisha masikini yalianza kurudi upya , ila kwake hakuwa na shida , aliingia ndani ya gari kwa kusitasita.
“Hii gari umeitoa wapi Roma , ni nzuri mno nitakuja kununua yangu kama hii”Aliongea Najma na kumfanya Roma Atoe tabasamu lililojaa uchungu moyoni mwake kwani aliamini taarifa anayokwenda kumwambia mwanadada huyu itamwachia machungu mengi moyoni.
“Najma naomba unisikilize jambo ninalokuambia, na pia nitaomba unisamehe kama nitakukwaza na kukuumiza , ila sitaki kukuficha ukweli wote Najma”Aliongea Roma na kumfanya Mrembo huyu amwangalie.
“Usijali wewe niambie tu Roma nipo tayari kusikilia lolote ili mradi liwe jambo la ukweli”Roma alivuta pumzi na kukusanya ujasiri aliokuwa nao ndani yake .
“Jana nimefanikiwa kukutana na mwanamke niliepotezana nae kwa miaka mingi ambaye nilidhania amefariki na baada ya kuonana tumefunga ndoa rasmi na unavyoniona hapa mimi ni mume wa mtu , najua ni kiasi gani unanipenda Najma na ndio maana siku zote nilikuwa nikijizuia kutokuzikubali hisia zako….”Roma kabla hata hajamaliza mlango wa gari ulifunguliwa na Najma alitoka na kukimbilia ndani kwao hakutaka tena kusikiliza maneno ya Roma,
Roma alibaki akiwa hajui ni kipi afanye , lakini hakuwa na jinsi , ili mradi ashauweka wazi ukweli wote mbele ya Najma, basi aliona ni vyema kwa mwanadada huyo kumsahau kaika maisha yake.
****
Ni muda wa Asubuhi ndani ya jengo la Club B, katika chumba ambacho kilikuwa ni ofisi ya mwanadada mrembo maarufu ndani ya eneo hili la Chalambe Maji matitu , alionekana Rose akiwa amekaa kwenye kiti chake cha kuzunguka huku mbele yake kukiwa na tarakishi kubwa iliokuwa imewashwa , huku mwanadada huyu akionekana kusoma taarifa iliokuwa kwenye mfumo wa Softcopy.
Ofisi yake ilikuwa ni kubwa , iliokua imependezeshwa na samani za bei ya juu kuonesha kuwa mwanadada huyu hakuwa vibaya kwenye swala la kifedha na kwa namna alivyokuwa amevaa na namna ambavyo alikuwa kaitumia Tarakishi hio alionekana kuwa Profesheno.
Baada ya dakika kadhaa za kukaa hapo ndani , mlango wake uligongwa na akaingia kijana mmoja alievalia suti na miwani ya jua akiwa na kipara kilichokuwa kinang`aa , bwana huyu alionekana kuwa ni wale vijana waliokuwa wakifanya mazoezi.
“Niambie Zonga unataarifa gani?”
“Madam taarifa niliokuwa nayo ni kwamba Roma kapata mke”
“Unamaanisha nini?”
“Kwa taarifa nilizokuwa nazo sasa Roma kafunga ndoa jana na leo amekuja sehemu anayoishi na kuchukua mizigo yake na kuhamia kwa mke wake”Maneno ya Zonga yalikuwa kama kisu cha moto kilichokuwa kikipita katika moyo wa mwanadada huyu.
“Bosi..!”Aliita zonga mara baada ya kumuona bosi wake akitoa machozi, na Rose aliyafuta haraka haraka na kisha aliachia tabasamu la ujasiri.
“Endelea kufatilia ni mwanamke gani Roma kamuoa” Aliongea Rose na Zonga alitoka
“Huyu fala ana nyota bwana , yaani mrembo kama bosi anatoa machozi kwa ajili ya fala mbeba mizigo , huyu jamaa ana nini mimi sina” Alijiongelesha Zonga ndani ya moyo wake huku akitoka ne ya ofisi.
Rose alisimama na kusogelea dirisha na kuangalia baadhi ya watu waliokuwa kwenye pilikapilika za kutafuta maisha huku akionekana ni mwenye mawazo sana huku akijizuia kulia.
“Stori yetu haiwezi kuisha hivi Roma ,Siku ulionikoa kwenye mikono ya baba yangu ndio ulikuwa mwanzo wa stori yetu na haikuwa bahati mbaya hata kidogo , nimetumia pesa nyingi sana kukutafuta na mpaka kukupata , siwezi kukuachia kirahisi” Alijiongelesha Rose.
****
Roma hakujali sana , aliendesha gari lake mpaka Kigamboni na kupokelewa na Bi Wema kwani mke wake hakuwa amerudi kutoka kazini, baada ya kuweka lile begi , alitoka nje na kuzunguka upande wa Yard ya magari huku mkononi akiwa ameshikilia kile kiboksi alicho toka nacho Mbagala , aliangalia sehemu ya kificha kiboksi hiko , lakini hakupata na mara akapata wazo na kuondoka ndani ya eneo hilo na kuingia chumba cha mazezi , aliangalia sehemu rahisi ya kuhifadhi kiboksi hicho , na alifanikiwa kupaona na kisha alikiweka vizuri na kuziba na kisha alitoka nje.
Baada ya kurudi ndani kwenye chumba chake aliwasha tarakishi na kisha akaingia kwenye mtandao na kuangalia namna ya kupata kazi , bahati nzuri , aliona baadhi ya makampuni mbalimbali yaliokuwa yakitangaza ajira , alichagua kazi aliona inafaa na kisha aliandika CV yake na kuituma pamoja na vivuli vya vyeti ambavyo alivitoa kwenye akaunti ya Barua Pepe yake , aliomba kwenye kampuni tatu harakaharaka na kisha alijilaza kitandani , lakini hakukaa muda mrefu , aliitwa na Bi wema na kuambiwa chakula tayari ashuke wakale.
Roma baada ya kula chakula kitamu kilichokuwa kimeandaliwa na Bi Wema , alirudi chumbani kwake huku kwenye kichwa cheke akiwa na mpango wa kwenda kupiga misele mjini maana alikuwa na kiasi cha pesa kilichokuwa kikimruhusu kufanya hivyo.
Alijiandaa haraka haraka, kwa kuvalia tisheti yake iliomtoa vyema na Jeans pamoja na Raba kisha alichukua ufunguo wa gari na kumuaga Bi Wema na kisha alitoa gari nduki.
Masaa machache tu alikuja kuonekana akiwa maeneo ya Posta kwenye moja ya saluni ya kisasa maarufu ,aliegesha gari yake kwa ustadi mkubwa huku waliokuwa karibu na eneo hilo wakiliangalia gari lake kwa matamanio.
Roma hakujali sana , alitoka kwenye gari na kisha aliingia ndani ya saluni hii ya kiume kwa ajili ya kutengenezwa nywele zake kitendo ambacho kilifanyika kwa muda mfupi sana , baada ya kupendeza kwa staili aliokuwa anataka yeye , aliendesha gari yake kuelekea upande wa Ocean road.
Muda wa saa kumi na mbili ndio muda ambao Roma alikuwa anarudi na sasa alikuwa anaingiza gari yake ndani ya jumba lao la kifahari , lakini ile anaingia aliona gari ambayo kwa haraka haraka alijua sio gari ya Edna , aliamini kulikuwa na ugeni ila hakujua ni ugeni wa mtu gani , ila aliamini kwakuwa ashafika , basi majibu ya maswali yake yatajibiwa akiingia ndani.
Baada ya kuingia ndani ni kweli aliona mwanaume mmoja ambae baada ya kumwangalia sura yake ilikuwa inakuja hivi na kupotea , mwanaume huyu hakuwa peke yake bali na mke wake alikuwepo.
“My Wife Am back!”Aliongea Roma na kumfanya kijana aliekuwa amekaa kwenye sofa amwangalie huku akionyesha chuki ya waziwazi na Roma aliliona hilo na kwakua alikuwa sio mtu wa kujali sana alisogea upande wa kushoto alipokuwa mke wake na kumbusu shavuni , kitendo ambacho Edna hakuzuia na Roma aligundua jambo pia kwa mara ya pili.
“Babe huyu ni nani?”
“Anaitwa Abubakari ni mwanaume ambaye nilikuwa nikikuambia”.
“Oooh ! unamaanisha yule mwanaume ambaye humpendi ndio huyu bwana”.
Maneno hayo yalimkera mno Abuu ila alijitahidi kujizuia mbele ya Edna.
“Braza vipi mimi ni Roma , ni mume wa Edna nimesikia habari nyingi juu ya kumsumbua mke wangu hivyo braza kaa mbali na mke wangu ama nitakufanya jambo baya”Aliongea Roma na kumfanya Abuu atabasamu kifedhuli.
“Wewe mbeba mizigo utanifanya nini labda.. usifikiri nimekaa kimya ukajua nakuogopa Edna ni wangu wewe ni wakuja tu na muda wowote utaondoka na kuurudia umasikini wak..”Ilikuwa ni kitendo cha haraka sana ambacho Roma alikifanya kwani kabla ya Abuu hajamaliza kuongea alikuwa hewani akining`inia kwenye mkono wa Roma,bwana huyu alikuwa akivuta pumzi kwa shida huku akijaribu kuongea neno lakini ni kama Roma hakujali na nia ya kumuua bwana huyu ilionekana waziwazi kwenye macho ya Roma.
“Roma Stoop..!!”Ilikuwa ni sauti ya kitetemeshi ya Edna iliomfanya Roma amtupe Abubakari chini kama furushi.
“Nikihesabu mpaka nne bado upo hapa ndani nakuaa .. moja,, mbili .. tatu..” Lakini kabla hajamaliza Abuu alisimama na kumwangalia Roma kwa macho makali na kisha alitoka huku akishika shingo yake, na hii ni baada ya kuona kuwa Roma hakuwa akitania kwani macho yake yalikuwa yamejaa hasira kali kiasi kwamba alionekana kuwa tayari kwa kuua muda wowote.
Upande wa Edna alishangazwa na uwezo wa nguvu aliokuwa nao Roma, namna ambavyo Roma alimning`iza hewani Abuu kilimuogopesha na kumuacha kwenye maswali.
“Mbona haupo makini Roma , unajitafutia matatizo , unajua nguvu iliokuwepo nyuma ya Abuu wewe?”
“Kwa hio kukiwa na nguvu kubwa nyuma yake nimuogope na akikanyaga mguu wake hapa tena namuua..”Aliongea Roma huku kiini cha macho yake kilichokuwa kimebadilika rangi kuwa kijani kilirudi na kuwa kama kawaida na kutokana na hasira alizokuwa nazo Roma hakutaka kubaki hapo sebuleni na kupandisha ngazi kwenda chumbani kwake na kufunga mlango kwa nguvu , huku akimuacha Edna aliekuwa akimwangalia kwa wasiwasi mkubwa.
Baada ya Roma kuingia kwenye chumba chake moja kwa moja alienda kuoga huku akituliza hasira zake, baada ya kujiona yupo sawa alisogelea Laptop yake na ile anaiwasha aliona ‘Notification’ kwenye barua pepe ikionesha kuna ujumbe , alifungua na kukuta kuna jumbe tatu.
“Mr Roma Ramoni we are happy to inform you that tomorrow we would like to do an interview with you regarding the job request you submitted to us , it will be our honor to see you tomorrow at xxx time”
“Ndugu Roma tunafuraha kukuambia kwamba tunapenda kufanya usaili na wewe kesho kulingana na ombi la kazi uliloliwasilisha kwetu , itakuwa heshima kwetu kama tutakuona kesho”.
Alifungua meseji ya pili na kisha akasoma.
“Hellow Mr Roma Ramoni we reviewed your job Request and your Credential’s that you submitted to us and confirmed they are Valid,We are replaying back to inform you to attend interview tomorrow morning at xxx time”
Karibia kampuni zote tatu zilikuwa zimerudhisha majibu ya kumtaka Roma kwenda kwenye interview siku ya kesho , alitabasamu na kuona kumbe kutafuta kazi ni rahisi hivyo, lakini licha ya majibu hayo alipanga kwenda kwenye kampuni moja tu na hivyo alitakiwa kuchagua kamouni moja ya kwenda kwa siku ya kesho.
“Vexto Group of Companies ndio moja ya kampuni ambayo Roma alidhamiria kwenda kufanya usaili kesho , kilichomvutia kuhusu hii kampuni kwanza ilikuwa ni kampuni kubwa sana ndani ya Afrika Mashariki na Kati yote ambayo ilikuwa inaendeshwa kwa thamani ya pesa kiasi cha Dola bilioni ishirini, Pili makao makuu ya kampuni hii yalikuwa makao makuu ya kampuni ya mavazi na mitindo ifahamikayo kwa jina la E- Styllus Wear , kampuni ambayo ilikuwa ikiaminika kwa kuwa na warembo wakali.
“Hii ndio kampuni nzuri , nitakutana na warembo wengi”
SEHEMU YA SABA
Muda wa saa mbili kamili za usiku Roma alishuka kwa ajili ya chakula , chakula ambacho alikula kama alikuwa na njaa ya wiki nzima , kwani alimaliza kalibia chakula chote kilichokuwa kwenye mabakuli.
Edna aliishia kujisemea kuwa Roma hakuwa ni mwenye aibu hata kidogo kwa upande wa Bi Wema alifurahishwa sana na uwezo wa kula wa Roma.
“Bebi Edna kesho naenda kwenye usaili”
“Sawa mafanikio mema”Aliongea Edna huku akinyanyuka na kutoa vyombo na baada ya kumaliza alipandisha ngazi na kwenda chumbani kwake , upande wa Roma hakuwa na mudi ya kubaki ndani hapo kwani alitoka na funguo zake na kuondoka.
Nusu saa mbele alikuwa alikuwa akiingia Chalambe Mbagala katika Rango kubwa la Club B, aliegesha gari lake na kuingia ndani huku akikutana na watu waliokuwa wamechangamka.
Zonga ndio mtu wa kwanza kumuona Roma, na alimsogelea kisha akamkaribisha kwa bashasha.
“Rose yuko wapi?”
“Madam Boss yupo ofisini kwake , itakuwa vyema kama utaenda kumuona”Aliongea Zonga na Roma alichukua upande ambao ofisi ya Rose ilikuwepo , alifungua mlango bila kugonga na kuingia ndani na kumkuta Rose aliekuwa amejiegamiza kwenye masofa huku pembeni kukiwa na chupa kibao za bia.
“Romaaa!”Aliongea Rose huku akinyanyuka na kivivu na kumsogelea kisha akamkumbatia huku machozi yakiwa yanamtoka , alianza kulia kwa kwikwi kiasi ambacho kilimshangaza Roma.
“Roma kwanini hukuniambia unamwanamke mpaka unaniumiza kiasi hiki”Aliongea Rose na kumfanya Roma atambue Rose anataarifa za yeye kuoa , Roma hakutaka kuongea chochote Zaidi ya kumtoa kifuani na kumwangalia usoni na kuona uso wa mrembo huyu ulivyokuwa kwenye majonzi , alisogeza mdomo wake na kugusisha na mdomo wa Rose na mwanamke hakuleta shida kwani aliupokea kwa pupa na walianza kukiss huku hisia zikiwa zinaongezeka kila baada ya sekunde
Ni ndani ya robo saa mbele Rose na Roma walionekana ndani ya kitanda kilichokuwa ndani ya ofisi hii ya Rose , huku mwanadada huyu akitoa miguno ambayo ilimfanya Roma kuongeza spidi ya kupiga kiuno.
Mchezo ulichukua Zaidi ya dakika tisini mpaka pale ambapo Roma aliweza kutua mzigo wake huku akiwa ni mwenye kuhema kwa nguvu , lakini kwa upande wa Rose akionekana akiwa hoi,Roma alimwangalia mwanadada huyu na kuona alikuwa kwenye maumivu na yote hio ni mara baada ya kugundua kuwa Rose alikuwa Bikra , jambo hili lilimshangaza.
“Twende nyumbani kwako , nitalala huko”Aliongea Roma na Rose alitingisha kichwa na walikokotana kwamlango tofauti na ule wa Bar na kisha Roma alimpandisha Rose kwenye Gari na kuondoka.
Sehemu aliokuwa akiishi Rose ni hapo hapo kwani walichukua dakika mbili kufika ndani ya Jumba la Kifahari la mwanadada huyu.
Roma alimsaidia Rose kwa kumkanda sehemu zake za siri ili kupoza maumivu na kisha waliingia kwenye shuka na kukumbatiana.
“Masikini nimeshakuwa mchepuko”
“Ndio huo ndio uhalisia unaopaswa ukubali , lakini sitokulazimisha kuendelea na mimi”
“Siwezi Roma nipo tayari kuwa mchepuko wako ila sio kukukosa kabisa”
Roma hakuongea kitu Zaidi ya kumkumbatia Rose huku akitabasamu.
“Mke hatanuna ukilala kwangu?”
“Hilo lisikusumbue mrembo eh , au unataka niondoke”
“Hapana nimeongea tu baba usiondoke”
“Saa moja kamili Roma aliamka na kuanza kumpapasa Rose ambaye alimpa ushirikiano wa kutosha na ndani ya dakika kadhaa mbele walipiga cha asubuhi na Roma akaingia bafuni na kumuaga Rose kwa kumuambia kuwa alikuwa na Usalili na kampuni
“Karibu nyumbani Mr Roma”Aliongea Bi wema baada ya kumuona Roma akiingia sebuleni , na wakati huu Bi wema alikuwa na Edna mezani wakinywa chai ya Asubuhi.
Roma alisalimia , huku akiliwa buyu na Mke wake wala hakujali na kukaa mezani na kujisevia msosi na kuanza kula kama hana akili nzuri , hakujali macho mabaya ya Edna.
“Bi Wema Asante kwa chai nzito , mimi ngoja nikajiandae kwa ajili ya kwenda kwenye usaili”.
“Bebi Edna niweke mume wako kwenye maombi nipate kazi”Aliongea Roma na bila hata ya kusubiri jibu alipandisha ngazi kuelekea kwenye chumba chake.
Ni muda waa saa tatu na nusu Roma aliegesha gari yake sehemu maalumu ndani ya jengo hili refu lililokkuwa likipatikana ndani ya Posta mtaa wa Samora , baada ya kutoka kwenye gari moja kwa moja alienda mapokezi na kujieleza kwa mwanadada mmoja mrembo huku akiwa ni mwenye kushangazwa na uzuri wa kila mfanyakazi wa kampuni hii.
“Hii sehemu ni sahihi kabisa kwangu”Alijiongelesha Roma huku akimkonyeza mrembo Mmoja aliekuwa eneo la mapokezi na mrembo huyo alitabasamu na kisha kumpita Roma .
Roma alishangazwa na watu waliokuwa wamekuja kwa ajili ya usahili kwani wote walikuwa ni wanawake tena warembo huku mwanaume aliemuona hapo ndani ni mmoja tu , tena ni jamaa mmoja hivi kibonge.
“Hey Boy na wewe umekuja kwenye usaili?”
“Ndio kaka , vipi wewe?”
“Hata mimi pia ,niite Jacob”
“Namini niite Roma”
“Sasa Roma wewe nini kimekuvutia kuja kuomba kazi hapa?”
“Sababu kubwa mimi ya kuja kuomba kazi hapa ni Warembo , nasikia hii kampuni ina mapini sio mchezo”
“Kaka nadhani umejionea mwenyewe ni kweli hii kampuni imejaa warembo”
“Vipi wewe?”
“Mimi sababu kubwa sio warembo ila kuna mrembo mmoja ndio amenifanya kuja kufanya kazi hapa”
“Yupi huyo”
“CEO”
“Unamaanisha CEO wa hii kampuni ni mwanamke na ni mrembo pia?”
“kaka ndani ya hii kampuni hakuna anaemfikia kwa uzuri CEO , kama huamini uliza uambiwe”Aliongea Kibonge
Wakati Roma na kibonge wanaongea , kibonge zamu yake ilifikia na kuingia kwenye chumba cha usaili na baada kama ya nusu saa alitoka huku akionekana kama mtu aliekosa tumaini.
“Vipi kaka mbona hivyo”
“Nimeulizwa maswali yote nimeshindwa kujibu sina ninalojua , ndoto yangu ya kuwa karibu na CEO imekufa kila la kheri kaka”Aliongea Kibongea na wakati huo huo Roma alisikia jina lake na kusogelea mlango na kuingia .
Ile anaingia tu alijikuta akipokewa na sura mbili anazozifahamu na sura moja asioifahamu , jumla ya wasaili walikuwa watatu , mtu wa kwanza Roma alimkumbuka vyema kwa urembo wake , lakini sio hivyo tu pia alimkumbuka kwa kumsaidia Shilingi Elfu tano siku ambayo aliachwa njiani na mke wake Edna, Mrembo yule msaili pia alimkumbuka vyema Roma na kujikuta akitabasamu mara baada ya kukutanisha nae macho,Siura ya pili Roma kuifahamu ni mdada alipishana nae Mapokezi , huyu ni mrembo aliemkonyeza.
“MisterRoma Ramoni nini kimekuvutia mpaka ukaomba kufanya kazi na sisi??”Aliuliza mrembo wa Buku tano.
“Kilichonivutia kwakweli si kingine Zaidi ya warembo, napenda kufanya kazi kwenye mazingira ambayo nazungukwa na warembo”Alijibu Roma kwa kujiamini na kuwafanya wasaili waangaliane na kutabasamu.
“Okey Mr Ramoni kwenye CV yako ulioanisha kwamba unajua kuzungumza Lugha za mataifa mbalimbali Zaidi ya kumi jambo ambalo tunamashaka nalo licha ya kwamba vyeti vyako vinaonesha una Masters ya uongozi wa biashara kutoka chuo cha Harvard , hivyo basi tumekuandalia maneno kumi ya lugha tofauti tofauti unazojua ili utuambie maana ya hayo maneno”
“Hakuna shida hilo ni rahisi sana kwangu”Aliongea Roma na kisha yule dada wa Mapokezi alionyesha maneno hayo kwa kutumia tarakishi na projekta na Roma alianza kusoma maneno hayo.
Yalianza kuonekana maneno ya kijerumani na Roma aliyasoma na kuyatolea tafsiri na wale walithibitisha ni sahihi , ikaja lugha ya kiarabu nayo hivyo hivyo , ikaja lugha ya kireno ikawa hivyo hivyo , ikaja kifaransa , kikorea , kichina Kinyarwanda …
Wasaili hawa walishangazwa mno na uwezo wa Roma , hawakuwahi kukutana na mtu ambae anajua Lugha nyingi kama Roma ..
Roma aliulizwa maswali mengi mengi na kuyajibu kiufasaha na wasaili wakakubaliana kumpa kazi Roma katika kitengo cha Public Relation.
“Karibu Vexto Roma, kwa kupata kwako kazi naamini Mke hatakuacha njiani tena mpaka kukosa nauli”Aliongea mwanadada yule msaili huku akitabasamu.
“Asante sana”
“Naitwa Doris Alex afisa mwajiri mkuu wa kampuni”.
“Nafurahi kufahamina na mrembo kama wewe Doris”Aliongea Roma na kumfanya mwanadada huyu kutabasamu na kufanya mashavu yake kuacha vishimo(Dimples)
“Naomba nichukue fursa hii kukuonesha baadhi ya maeneo ya kampuni kabla hatujaanza kazi rasmi”Aliongea Doris na Roma alitingisha kichwa na wote wakaingia kwenye Lift , Roma muda wote tabasamu halikuwa likimwishia usoni , alijiona kama vile yupo kwenye mbingu ya warembo, mrembo Dorisi alikuwa amempagawisha mno.
“Hii ndio Floor ambayo viongozi wa juu ya kampuni ofisi zao zipo , hii ni ofisi ya mhasibu mkuu wa makampuni ya Vexto , hii ni ofisi yangu”Huku wakiingia na Roma aliisifia ofisi ya Doris.
Wakati Dorisi akiendelea kumpa shule Roma mara simu ya ofisi yake ilitoa mlio kuashiria inaita , alipokea na kuweka sikioni na kisha akashusha mkonga.
“Unaonekana kuwa na bahati sana Roma,CEO anataka kuonana na wewe jambo ambalo sio la kawaida”Aliongea Doris na alimpeleka mpaka kwenye mlango wa ofisi uliojitenga na kisha alifungua na kukutana na sekretari alimchangamkia na kumkaribisha , Sekretari alikuwa wakawaida sana , hakuwa mrembo sana.
“Boss! Mr Ramoni has arrived”Aliongea Sekretari
“Let him in”
“You may go in na tafadhari hakikisha unakuwa na heshima mbele ya bosi , sio mtu ambaye kila mtu anaweza kuingia kwenye ofisi yake”Aliongea mwanadada huyu na Roma aliingia ndani ya ofisi hio kubwa huku akiwa na tabasamu la kukutana na CEO mrembo maana kwenye kichwa cheka alikuwa akikumbuka maneno ya Kibonge aliekuja nae kufanya usaili muda mfupi uliopita.
“Akinivutia namtongoza ,CEO kitu gani bwana”aliwaza
Roma alijikuta akipagawa baada ya kumuona mtu ambae hakumtegemea kuwa ndio CEO”
ITAENDELEA JUMATATU WADAU