Serikali haioni mateso ya watoto wadogo kupindi hiki cha mvua kubwa na ikasimamisha kwa muda

USSR

JF-Expert Member
Jul 15, 2015
9,896
22,667
Baada ya maji kuwasomba watoto na kuwauwa kule Arusha nilijua serikali ingeona nini kitatokea, na sasa wanasema itachukua wiki mbili kunyesha kwa kiwango kikubwa namna hii na watoto wa kitanzania wanasota huku wale wa nchi za jirani wamesitisha ukatili huu kwa muda

Ukiwa njiani unawaona watoto wadogo 5yrs na ziada wakiwa njiani wamenyeshewa wanakwenda shule au wanatoka wapo chepechepe kwa mvua, viatu vimejaa tope na kulowa maji yanayotililika kwenye barabara zilizojaa maji na vidibwi .

Vitabu na madaftari yamelowa wengine hawana hata masweta wanapigwa na baridi

Kuna ulazima gani haswa wa watoto hawa wateseke kipindi kigumu cha namna hii wakati uwezo wa kutatua hili upo wazi.

USSR
 
Hapo ndiyo utajua kuwa viongozi wengi serikalini wana uwezo mdogo mno wa kupambanua mambo.tujiulize uhai wa watoto na elimu zao kipi kitangulie??
 
wale wa day school ndio wanapata tabu zaidi.. wa boarding naona hawana shida sn lbd kama eneo la shule lipo kwenye hatari ya kupatwa na mafuriko.

serikali hata hivyo ingesitisha kwa muda masomo ili kupisha hizi mvua na kuwapa nafuu kidogo wa day school mana ndio walio wengi zaidi.
 
Baada ya maji kuwasomba watoto na kuwauwa kule Arusha nilijua serikali ingeona nini kitatokea ,na sasa wanasema itachukua wiki mbili kunyesha kwa kiwango kikubwa namna hii na watoto wa kitanzania wanasota huku wale wa nchi za jirani wamesitisha ukatili huu kwa muda

Ukiwa njiani unawaona watoto wadogo 5yrs na ziada wakiwa njiani wamenyeshewa wanakwenda shule au wanatoka wapo chepechepe kwa mvua ,viatu vimejaa tope na kulowa maji yanayotililika kwenye barabara zilizojaa maji na vidibwi .

Vitabu na madaftari yamelowa wengine hawana hata masweta wanapigwa na baridi

Kuna ulazima gani haswa wa watoto hawa wateseke kipindi kigumu cha namna hii wakati uwezo wa kutatua hili upo wazi .

USSR
Kama unaisubiri serikali hii ifanye kitu umefeli!....mm nikiona mvua na hali ya hewa mbovu nawaambia watoto wasiende shule!
 
Baada ya maji kuwasomba watoto na kuwauwa kule Arusha nilijua serikali ingeona nini kitatokea ,na sasa wanasema itachukua wiki mbili kunyesha kwa kiwango kikubwa namna hii na watoto wa kitanzania wanasota huku wale wa nchi za jirani wamesitisha ukatili huu kwa muda

Ukiwa njiani unawaona watoto wadogo 5yrs na ziada wakiwa njiani wamenyeshewa wanakwenda shule au wanatoka wapo chepechepe kwa mvua ,viatu vimejaa tope na kulowa maji yanayotililika kwenye barabara zilizojaa maji na vidibwi .

Vitabu na madaftari yamelowa wengine hawana hata masweta wanapigwa na baridi

Kuna ulazima gani haswa wa watoto hawa wateseke kipindi kigumu cha namna hii wakati uwezo wa kutatua hili upo wazi .

USSR
masuala haya,
kwa mamlaka sio ya kuamka tu na kuamua kwasababu umeskia fulani anaona huruma watoto wanachapwa baridi mahali fulani au wamepata athari fulani....

lazima kutathmini kwa kina na kujiridhisha mwenendo wa hali ya hewa na athari zilizokwisha tokea na zinazoweza kutokea mbeleni kuputia kamati za ulinzi na usalama za maeneo husika...

subra na ustahimilivu ni muhimu sana kwenye mambo haya :whatBlink:
 
Mkenda wizara inamshinda hii, huu ni muda alitakiwa aseme shule zifungwe kwa angalau week 2 mpaka hali itulie ndo wafungue, yeye anawaza mbege tu.
 
Chukua hatua kwa ajili ya mtoto wako, huko shuleni kwenyewe hawasomi, walimu wamekumbatia wake zao, watoto wanacheza tu darasani
 
Kuna maamuzi kama mzazi unapaswa uyachukue wewe mwenyewe usisubiri 'Serikali', ukisubiri hicho kinachoitwa serikali utasubiri sanan mpaka yesu arudi, wenzio wanayaona mafuriko kwenye TV tu huko nchi za nje
 
Back
Top Bottom