Rais Samia atoa Nishani za Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuzindua Kitabu cha Miaka 60 ya Historia ya Ofisi ya Makamu wa Rais

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,854
12,089
Rais Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akitoa Nishani za Miaka 60 ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuzindua Kitabu cha Miaka 60 ya Historia ya Ofisi ya Makamu wa Rais katika Viwanja vya Ikulu - Chamwino Dodoma tarehe 24 Aprili 2024.


View: https://www.youtube.com/live/EmRN8w3uk7w?si=SMHMMsNu_3_zvd_f

20240424_161312.jpg

Rais Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Mama Salma Kikwete Nishani ya Mwalimu Julius
Kambarage Nyerere aliyoipokea kwa niaba ya Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwenye hafla iliyofanyika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.

20240424_161451.jpg

Rais Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Mama Janeth Magufuli Nishani ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ambayo aliipokea kwa niaba ya Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli katika halfa iliyofanyika lkulu Chamwino, Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.

20240424_161631.jpg
Rais Samia Suluhu Hassan akimtunuku na kumvalisha Nishani ya Mwenge wa Uhuru Daraja la Pili Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Samwel Malecela kwenye hafla iliyofanyika Ikulu ya Chamwino, Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024

20240424_161840.jpg
Rais Samia Suluhu Hassan akimtunuku na kumvalisha Nishani ya Mwenge wa Uhuru Daraja la Pili Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Awamu ya Tatu Mhe. Fredrick Sumaye kwenye hafla iliyofanyika katika Ikulu ya Chamwino Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.
WhatsApp Image 2024-04-24 at 17.24.02_c273a283.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimpa Rais Mstaafu wa Zanzibar Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein vitabu vya Miaka 60 ya Historia ya Ofisi ya Makamu wa Rais pamoja na Kitabu cha Safari za Picha ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa miaka 60 kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.
WhatsApp Image 2024-04-24 at 14.27.33_b6ec1a67.jpg

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimtunuku na kumvalisha Nishani ya Mwenge wa Uhuru Daraja la Pili Makamu Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mohamed Gharib Bilal kwenye hafla iliyofanyika katika Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma tarehe 24 Aprili, 2024.
WhatsApp Image 2024-04-24 at 17.51.56_a0bd83af.jpg
 
Rais wa JMT mh Dr Samia Suluhu Hassan amemtumukia Nishani ya Mwalimu Nyerere Shujaa Magufuli

Nishani hiyo kakabidhiwa mama Janeth Magufuli mjane wa Shujaa

Source: Ayo TV

Watu wa Legacy tunashangilia 😂😂🔥🔥
Ni kuelekea uchaguzi
 
Hongera kwake kwa kutunukiwa nishani hiyo .

Ila tukianza kuongelea yaliyofanyika enzi za "shujaa" kama kwa Ben Saanane, Azory Gwanda, Leopold Lwajabe , Roma Mkatoliki, Mohamed Dewji na wengineo wengi tunaomba muwe mnazijibu hoja sio kusema aachwe apumzike wakati nishani mnampa hamuachi apumzike.
 
Hongera kwake kwa kutunukiwa nishani hiyo .

Ila tukianza kuongelea yaliyofanyika enzi za "shujaa" kama kwa Ben Saanane, Azory Gwanda, Leopold Lwajabe , Roma Mkatoliki, Mohamed Dewji na wengineo wengi tunaomba muwe mnazijibu hoja sio kusema aachwe apumzike wakati nishani mnampa hamuachi apumzike.
Tulia wewe bwege

Mbona unatumia ID feki sasa
 
Unafiki kwenye siasa ni kwa sababu ya kuwapumbaza wapumbavu tu. 🙌🏽 🙌🏽
 
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi akizungumza wakati wa hafla ya utoaji nishani kwa viongozi mbalimbali na uzinduzi wa vitabu viwili cha Historia ya Ofisi ya Makamu wa Rais na safari ya picha za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwa ni shamrashamra za Miaka 60 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar katika viwanja vya Ikulu Chamwino tarehe: 24 Aprili, 2024.
 

Attachments

  • VID-20240424-WA0085.mp4
    26.1 MB
Back
Top Bottom