JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,317
- 5,479
WAMILIKI MABASI YA SAULI NA NEW FORCE WATAKIWA KUJIELEZA KABLA YA KUCHUKULIWA HATUA ZA KIUDHIBITI
Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imefanya kikao kilichohusisha Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani na wamiliki wa mabasi ya Sauli na New Force yaliyosababisha ajali ya tarehe 28 Machi, 2024 majira ya saa tisa na dakika arobaini na mbili (09:42) alfajiri, ambapo magari matatu yaligongana eneo la Mashamba ya Mpunga Wilayani Kibaha, Mkoani Pwani katika barabara ya Morogoro. Kufuatia kikao hicho, Mamlaka imewataka wasafirishaji hao kutoa maelezo kwa maandishi kabla ya kuchukua hatua za kiudhibiti dhidi yao.
Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, ajali hiyo imetokana na uzembe wa dereva wa basi namba T668DTF Scania mali ya Mwalabhila Sauli kutaka kuyapita magari mengine bila kuchukua tahadhari ya watumiaji wengine wa barabara.
Aidha, madhara ya ajali hiyo yalichangiwa na uzembe wa dereva wa basi namba T175DZU linalomilikiwa na kampuni ya New Force kushindwa kuacha umbali wa gari lililokuwa mbele yake kama inavyopaswa na kusababisha vifo vya watu wawili (2), majeruhi na uharibifu mkubwa wa mali.
Kwa mujibu wa taarifa za Mfumo wa Kufuatilia Mwenendo wa Magari (VTS), tarehe ya tukio magari namba T175DZU na T6668DTF yalianza safari kutoka Dar es salam kwa pamoja saa nane na dakika arobaini na nne (8:44) usiku, ambapo kwa mujibu wa leseni walizopewa, mabasi hayo yalipaswa kuanza safari saa tisa kamili (9:00) na saa kumi na dakika thelathini (10:30) alfajiri, mtawalia.
Aidha, uchunguzi zaidi kwenye mifumo ya Mamlaka unaonesha kuwa madereva wa mabasi hayo wamesajiliwa kwenye mifumo ya Mamlaka lakini hawakutumia vitufe vya utambulisho (i-Button).
Kwa jumla, makosa yaliyobainika yamechangiwa na madereva pamoja na wamiliki wa mabasi hayo. Mamlaka inawakumbusha wamiliki na madereva kutimiza wajibu wao kwa mujibu wa Sheria katika kutoa huduma za usafiri.
Hata hivyo, takwimu zinaonesha kuwa, safari za mabasi ya usiku nchini, zina matukio machache ya ajali na vifo ukilinganisha na safari za mchana. Kati ya mwezi Oktoba 2023 na Februari, 2024 kulitokea jumla ya ajali 68 ambazo kati yake ajali 10 tu zilitokea usiku.
Vilevile katika kipindi hicho, vifo vilivyotokana na ajali za mabasi vilikuwa 9 ambapo vifo 4 vilitokana na safari za usiku. Mamlaka inawashukuru watoa huduma za usafiri wa mabasi ya masafa marefu kwa ushirikiano wao katika kutekeleza ratiba za safari za usiku.
Imetolewa na;
Salum Pazzy
Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano
Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) imefanya kikao kilichohusisha Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani na wamiliki wa mabasi ya Sauli na New Force yaliyosababisha ajali ya tarehe 28 Machi, 2024 majira ya saa tisa na dakika arobaini na mbili (09:42) alfajiri, ambapo magari matatu yaligongana eneo la Mashamba ya Mpunga Wilayani Kibaha, Mkoani Pwani katika barabara ya Morogoro. Kufuatia kikao hicho, Mamlaka imewataka wasafirishaji hao kutoa maelezo kwa maandishi kabla ya kuchukua hatua za kiudhibiti dhidi yao.
Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, ajali hiyo imetokana na uzembe wa dereva wa basi namba T668DTF Scania mali ya Mwalabhila Sauli kutaka kuyapita magari mengine bila kuchukua tahadhari ya watumiaji wengine wa barabara.
Aidha, madhara ya ajali hiyo yalichangiwa na uzembe wa dereva wa basi namba T175DZU linalomilikiwa na kampuni ya New Force kushindwa kuacha umbali wa gari lililokuwa mbele yake kama inavyopaswa na kusababisha vifo vya watu wawili (2), majeruhi na uharibifu mkubwa wa mali.
Kwa mujibu wa taarifa za Mfumo wa Kufuatilia Mwenendo wa Magari (VTS), tarehe ya tukio magari namba T175DZU na T6668DTF yalianza safari kutoka Dar es salam kwa pamoja saa nane na dakika arobaini na nne (8:44) usiku, ambapo kwa mujibu wa leseni walizopewa, mabasi hayo yalipaswa kuanza safari saa tisa kamili (9:00) na saa kumi na dakika thelathini (10:30) alfajiri, mtawalia.
Aidha, uchunguzi zaidi kwenye mifumo ya Mamlaka unaonesha kuwa madereva wa mabasi hayo wamesajiliwa kwenye mifumo ya Mamlaka lakini hawakutumia vitufe vya utambulisho (i-Button).
Kwa jumla, makosa yaliyobainika yamechangiwa na madereva pamoja na wamiliki wa mabasi hayo. Mamlaka inawakumbusha wamiliki na madereva kutimiza wajibu wao kwa mujibu wa Sheria katika kutoa huduma za usafiri.
Hata hivyo, takwimu zinaonesha kuwa, safari za mabasi ya usiku nchini, zina matukio machache ya ajali na vifo ukilinganisha na safari za mchana. Kati ya mwezi Oktoba 2023 na Februari, 2024 kulitokea jumla ya ajali 68 ambazo kati yake ajali 10 tu zilitokea usiku.
Vilevile katika kipindi hicho, vifo vilivyotokana na ajali za mabasi vilikuwa 9 ambapo vifo 4 vilitokana na safari za usiku. Mamlaka inawashukuru watoa huduma za usafiri wa mabasi ya masafa marefu kwa ushirikiano wao katika kutekeleza ratiba za safari za usiku.
Imetolewa na;
Salum Pazzy
Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano