Bila bila
JF-Expert Member
- Dec 20, 2016
- 21,524
- 37,838
Sidhani kama ni Kashfa Kwa nchi kama unavyosema. Ila haiwezekani Chama cha soka kikaanzisha mashindano mwishoni mwa kalenda ya mwaka ya Soka halafu Wenye busara wakakaa kimya. Muungano unajulikana ni 26 April na maadhimisho ya miaka 60 yalijulikana kitambo, iweje mashindano yaanzishwe ghafla kàma tumbo la kuhara?Ndiyo maana kuna wakati nasema huu tunaoita utani wa jadi tuufutilie mbali maana watu wamekuwa wajinga wajinga tu na wengine inasababisha mioyo yao inabeba roho za husda, chuki, wivu na takataka zingine.
Morocco wana Kombe la Mfalme. Hakuna ubaya kuwa na mashindano ambayo yanaenzi mfumo wetu wa nchi. Watu wajinga wajinga ndiyo wanaweza kutoa kauli kama hizi za kulibeza.
NB. Kombe la Muungano lipangiwe ratiba maalumu na utaratibu unaoeleweka badala ya kuwa la kushtukiza kama ilivyotokea mwaka huu. Pia zawadi kwa mshindi iwe kubwa zaidi ingawa nimesikia kuanzia mwakani mshindi anaondoka na milioni 100.
Mods Cookie Active futeni huu uzi, hauna tofauti na kuikashfu nchi.