UAE yaitaka Israel ikome kuwahusisha na kile wanachokiita kuitawala Gaza baada ya vita

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,471
11,454
Waziri mkuu wa falme za kiarabu,Abdullah bin Zayed amemshushua waziri mkuu wa Israel,Benjamin Netanyahu kwa kauli yake aliyoitoa hivi karibu kwamba nchi ya UAE, Saudi Arabia na mataifa mengine ya kiarabu yatasaidia kuiendesha Gaza baada ya vita.

Waziri huyo kwanza amemtaka Netanyahu kutambua kwamba hivi sasa Israel imeivamia Gaza na kwamba hakuna haki ya kufanya hivyo. Akaongeza kuwa Israel iache kuihusisha UAE na mpango wowote wa kuhalalisha nchi hiyo kuendelea kuwepo Gaza.

Zaidi ya hivyo bwana Abdullah akasema nchi yake inalaani kitendo cha jeshi la Israel kukikalia kituo cha mpakani cha Rafah na kuzuia kuingizwa misaada ya mahitaji kwa wapalestina.

UAE ndio nchi ya mwanzo katika miaka ya karibuni, mnamo mwaka 2020 kurudisha mahusiano ya kidiplomasia na taifa hilo la kiyahudi hatua ambayo imeendelea kupingwa na wananchi wa nchi hiyo.

UAE lashes out at Netanyahu over joining post-war Gaza administration

 
Waziri mkuu wa falme za kiarabu,Abdullah bin Zayed amemshushua waziri mkuu wa Israel,Benjamin Netanyahu kwa kauli yake aliyoitoa hivi karibu kwamba nchi ya UAE, Saudi Arabia na mataifa mengine ya kiarabu yatasaidia kuiendesha Gaza baada ya vita.

Waziri huyo kwanza amemtaka Netanyahu kutambua kwamba hivi sasa Israel imeivamia Gaza na kwamba hakuna haki ya kufanya hivyo. Akaongeza kuwa Israel iache kuihusisha UAE na mpango wowote wa kuhalalisha nchi hiyo kuendelea kuwepo Gaza.

Zaidi ya hivyo bwana Abdullah akasema nchi yake inalaani kitendo cha jeshi la Israel kukikalia kituo cha mpakani cha Rafah na kuzuia kuingizwa misaada ya mahitaji kwa wapalestina.

UAE ndio nchi ya mwanzo katika miaka ya karibuni, mnamo mwaka 2020 kurudisha mahusiano ya kidiplomasia na taifa hilo la kiyahudi hatua ambayo imeendelea kupingwa na wananchi wa nchi hiyo.

UAE lashes out at Netanyahu over joining post-war Gaza administration

wafadhiri wa Hamas wanazi jitokeza , ngoja wasuse halau Israel itawale maana waarabu hawana akili ya kuona kesho
 
Waarabu wameona ushirikiano na mrusi una manufaa zaidi hapo mbeleni
Ukishirikiana na Mrusi uwezekano wako mkubwa ni kuwa maskini tu yaani hautakwepa hilo.

Wakati wa USSR mataifa yote ya Ulaya Mashariki yaliyotwaliwa na iliyokuwa Jumuiya ya Kisovieti yote kwa ujumla wao yaliishia kuwa watembeza bakuli na ilikuwa ni kawaida kabisa kukuta kwenye nchi hizo maeneo ya vijijini watu wakiwa na vyoo vya matundu kama tu Afrika.

Lakini baada ya Marekani kuiua USSR na mataifa hayo kujiunga na Jumuiya ya Ulaya na kuachana na Russia ndipo vipato vya wananchi ktk nchi hizo vimeongezeka mara tano na chumi zao zimekuwa vizuri sana. Russia ni nchi moja ya hovyo sana kujiweka nayo karibu.
 
Ukishirikiana na Mrusi uwezekano wako mkubwa ni kuwa maskini tu yaani hautakwepa hilo.

Wakati wa USSR mataifa yote ya Ulaya Mashariki yaliyotwaliwa na iliyokuwa Jumuiya ya Kisovieti yote kwa ujumla wao yaliishia kuwa watembeza bakuli na ilikuwa ni kawaida kabisa kukuta kwenye nchi hizo maeneo ya vijijini watu wakiwa na vyoo vya matundu kama tu Afrika.

Lakini baada ya Marekani kuiua USSR na mataifa hayo kujiunga na Jumuiya ya Ulaya na kuachana na Russia ndipo vipato vya wananchi ktk nchi hizo vimeongezeka mara tano na chumi zao zimekuwa vizuri sana. Russia ni nchi moja ya hovyo sana kujiweka nayo karibu.
Gazeti reefu,,,kiufupi tu upepo unabadilika sio enzi za 19.... na kitu hizi, nyie bakini na akili hizo hizo watu wanataka haki sio ubabe wa kizamani
 
Ukishirikiana na Mrusi uwezekano wako mkubwa ni kuwa maskini tu yaani hautakwepa hilo.

Wakati wa USSR mataifa yote ya Ulaya Mashariki yaliyotwaliwa na iliyokuwa Jumuiya ya Kisovieti yote kwa ujumla wao yaliishia kuwa watembeza bakuli na ilikuwa ni kawaida kabisa kukuta kwenye nchi hizo maeneo ya vijijini watu wakiwa na vyoo vya matundu kama tu Afrika.

Lakini baada ya Marekani kuiua USSR na mataifa hayo kujiunga na Jumuiya ya Ulaya na kuachana na Russia ndipo vipato vya wananchi ktk nchi hizo vimeongezeka mara tano na chumi zao zimekuwa vizuri sana. Russia ni nchi moja ya hovyo sana kujiweka nayo karibu.
Jibu lako lipo juu hapo
 
Back
Top Bottom