Mei Mosi ni faida au hasara kwa Taifa?

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Feb 20, 2016
14,370
21,033
Sikukuu ya Mei Mosi, inayojulikana pia kama Siku ya Wafanyakazi Duniani, inaadhimishwa kwa kusherehekea mchango wa wafanyakazi katika kujenga jamii na kuboresha hali zao za kazi.

Sikukuu hii ina historia ndefu ya kutetea haki za wafanyakazi na kuimarisha mazingira ya kufanya kazi, na imekuwa ikisherehekewa tangu karne ya 19. Katika maeneo mengi, watu hupanga maandamano, mikutano, na matukio mbalimbali kama vile mijadala na matamasha ili kujadili masuala ya kazi na kuimarisha umoja wa wafanyakazi. Katika nchi nyingine, Mei Mosi ni siku ya mapumziko rasmi.

1-5-2024 Pale Arusha uwanja wa Mpira walijaa serikali yote isipokuwa Rais mpenwa Samia.
Wafanyakazi walilipia flana na kofia, usafiri na malazi huku maofisi yakiwalipa posho za safari na per diem kwenda kwenye sikukuu/.
Katika hali ya kuogofya, sikukuu ikageuka ya kumsifi mama , kusifia wadudu[wahuni wa chugga], kusifia bodaboda na waongoza watalii huku wafanyakazi wakiachwa wapigwe jua kali na kuahidiwa POSHO nzuri ambapo badae walikwenda kuzidai kwa aliye waahidi.

Kuna ulazima wa kutumia mabilioni uwanjani ilhali mita chache kuna watoto wanazaliwa sakafuni?
Kuna haja ya kusheherekea kuwatoa watu Tanga na kilmanajor, manyara kuja kuangalia "wadudu"-panya road ?

sherehe ilikuwa ya kuangalia maslahi ya mfanyakazi na kumpongeza mfanyakazi ama ya umsifia fulani?​
 
Sikukuu ya Mei Mosi, inayojulikana pia kama Siku ya Wafanyakazi Duniani, inaadhimishwa kwa kusherehekea mchango wa wafanyakazi katika kujenga jamii na kuboresha hali zao za kazi.

Sikukuu hii ina historia ndefu ya kutetea haki za wafanyakazi na kuimarisha mazingira ya kufanya kazi, na imekuwa ikisherehekewa tangu karne ya 19. Katika maeneo mengi, watu hupanga maandamano, mikutano, na matukio mbalimbali kama vile mijadala na matamasha ili kujadili masuala ya kazi na kuimarisha umoja wa wafanyakazi. Katika nchi nyingine, Mei Mosi ni siku ya mapumziko rasmi.

1-5-2024 Pale Arusha uwanja wa Mpira walijaa serikali yote isipokuwa Rais mpenwa Samia.
Wafanyakazi walilipia flana na kofia, usafiri na malazi huku maofisi yakiwalipa posho za safari na per diem kwenda kwenye sikukuu/.
Katika hali ya kuogofya, sikukuu ikageuka ya kumsifi mama , kusifia wadudu[wahuni wa chugga], kusifia bodaboda na waongoza watalii huku wafanyakazi wakiachwa wapigwe jua kali na kuahidiwa POSHO nzuri ambapo badae walikwenda kuzidai kwa aliye waahidi.

Kuna ulazima wa kutumia mabilioni uwanjani ilhali mita chache kuna watoto wanazaliwa sakafuni?
Kuna haja ya kusheherekea kuwatoa watu Tanga na kilmanajor, manyara kuja kuangalia "wadudu"-panya road ?

sherehe ilikuwa ya kuangalia maslahi ya mfanyakazi na kumpongeza mfanyakazi ama ya umsifia fulani?​
Kwa mara ya kwanza naona sherehe ya wafanyakazi, wanaopewa kipaumbele ni wadudu jobless.

Idea ya kondaboy
 
Back
Top Bottom