Mbunge Kwagilwa Nhamanilo: Rais Samia ndio aliruhusu shughuli za kisiasa kuendelea, kwanini hamkuhoji wakati ule huyu ni Mzanzibari?

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,994
961
"Jambo hili watu wengi wamelizungumzia huko nje, wapo waliolipotosha na wapo waliokwenda mbali zaidi na kuzungumza yale ambayo ni hatari kwa Umoja wa nchi yetu na mshikamano wa Taifa letu. Nataka niwakumbushe wakati nchi yetu ilipopita kipindi kigumu cha COVID-19 wakati Dunia yote ilijifungia ndani haikuzalisha, Watanzania tulikuwa tunatembea mtaani na tulikuwa tunafanya shughuli zetu na Makamu wa Rais wa nchi hii alikuwa ni Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ndiye alikuwa Mshauri mkuu wa Rais aliyekuwepo, tulivuka salama na hatukumtilia mashaka kuwa ni Mtanzania au si Mtanzania" - Mhe. Kwagilwa Reuben Nhamanilo, Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini

"Jambo hili hatupaswi kuliendekeza yanapokuja mambo ya msingi ya hoja tutofautiane kwa hoja na si kwa kubaguana. Miaka Miwili iliyopita shughuli za kisiasa hazikuwa zinaruhusiwa kufanyika; hapakuwa na Mkutano wa Chama cha siasa wala Press Conference za kwenye vyombo vya Habari. Ni Rais huyu huyu alikuja kufungua minyororo" - Mhe. Kwagilwa Reuben Nhamanilo, Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini

"Kwanini wakati ule hamkuhoji kuwa huyu ni Mzanzibar amekuja kufungulia vyombo vya Habari? Miaka Miwili iliyopita kulikuwa na magazeti zaidi ya 4 yamefungiwa, Online TV, Online Media karibu vyombo 30 - 40 vimefungiwa. Ni Rais huyu huyu aliyepo alifungua vyombo vyote vilivyokuwa vimefungiwa. Mpaka sasa hakuna kesi Mahakamani ya Chombo chochote cha Habari wala mwandishi wa Habari" - Mhe. Kwagilwa Reuben Nhamanilo, Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini.


====

Pia soma:
Tundu Lissu: Tuna Rais Mzanzibari anayeweza kwenda Ngorongoro na kutoa Amri kwa Wanajeshi wafukuze wamasai wote
 
..Katiba ndio imeruhusu mikutano na maandamano.

..Mimi ningemsifu Rais Samia kama Katiba ingekuwa inakataza mikutano na maandamano, halafu yeye akaibadilisha na kuruhusu haki hizo.

..Pia Rais akifanya jambo la heri atasifiwa, na akifanya jambo la hovyo atalaumiwa. Rais akifanya jambo la heri sio kibali cha kutokulaumiwa akikosea mbele ya safari.
 
"Jambo hili watu wengi wamelizungumzia huko nje, wapo waliolipotosha na wapo waliokwenda mbali zaidi na kuzungumza yale ambayo ni hatari kwa Umoja wa nchi yetu na mshikamano wa Taifa letu. Nataka niwakumbushe wakati nchi yetu ilipopita kipindi kigumu cha COVID-19 wakati Dunia yote ilijifungia ndani haikuzalisha, Watanzania tulikuwa tunatembea mtaani na tulikuwa tunafanya shughuli zetu na Makamu wa Rais wa nchi hii alikuwa ni Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ndiye alikuwa Mshauri mkuu wa Rais aliyekuwepo, tulivuka salama na hatukumtilia mashaka kuwa ni Mtanzania au si Mtanzania" - Mhe. Kwagilwa Reuben Nhamanilo, Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini

"Jambo hili hatupaswi kuliendekeza yanapokuja mambo ya msingi ya hoja tutofautiane kwa hoja na si kwa kubaguana. Miaka Miwili iliyopita shughuli za kisiasa hazikuwa zinaruhusiwa kufanyika; hapakuwa na Mkutano wa Chama cha siasa wala Press Conference za kwenye vyombo vya Habari. Ni Rais huyu huyu alikuja kufungua minyororo" - Mhe. Kwagilwa Reuben Nhamanilo, Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini

"Kwanini wakati ule hamkuhoji kuwa huyu ni Mzanzibar amekuja kufungulia vyombo vya Habari? Miaka Miwili iliyopita kulikuwa na magazeti zaidi ya 4 yamefungiwa, Online TV, Online Media karibu vyombo 30 - 40 vimefungiwa. Ni Rais huyu huyu aliyepo alifungua vyombo vyote vilivyokuwa vimefungiwa. Mpaka sasa hakuna kesi Mahakamani ya Chombo chochote cha Habari wala mwandishi wa Habari" - Mhe. Kwagilwa Reuben Nhamanilo, Mbunge wa Jimbo la Handeni Mjini.


====

Pia soma: Tundu Lissu: Tuna Rais Mzanzibari anayeweza kwenda Ngorongoro na kutoa Amri kwa Wanajeshi wafukuze wamasai wote
Kwamba huyo mbunge haijui Katiba au?
 
Back
Top Bottom