Teko Modise
JF-Expert Member
- May 20, 2017
- 1,963
- 6,109
Kipindi akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani na Nchi, alikuwa anamiliki timu ya Singida Utd ya pale mkoani Singida. Akajaza wachezaji wa kigeni kibao kama vile Michel Rusheshagonga, Shafik Batambuze, Tafazwa Kutinyu nk
Wadhamini nao wakajitokeza wa kutosha mpaka jezi ikawa imechafuka kwa matangazo ya wadhamini.
Miaka michache baadae akatumbuliwa na hayati Magufuli, hatimae na mrija wa pesa ukapungua, wadhamini wakajitoa Singida ikashuka na kusahaulika ligi kuu bara.
Aliporudishwa kwenye Baraza la Mawaziri enzi ya Magufuli, akakaa kwa adabu bila kujihusisha na umiliki wa timu.
Baada ya kifo cha hayati Magufuli, Mama Samia akawa Rais na kumchagua Mwigulu kuwa Waziri wa Fedha. Ndani ya mwaka mmoja tu, tayari timu yake mpya aliyoinunua ya DTB imepanda daraja huku baadhi ya wachezaji waliopandisha timu hiyo wakiwa ni wale wale waliotumika enzi ya Singida Utd.
Japo amekuwa akikanusha kuwa yeye sio mmiliki, lakini ukweli siku zote haujifichi. DTB ina mastaa kibao kama Juma Abdul, Amis Tambwe, David Mwantika, Nicholaus Gyan, Tafazwa Kutinyu, na wengineo wengi.
Hizi fedha huwa anatoa wapi? Ni kwanini huwa anamiliki akiwa na cheo tu Serikalini?
Wadhamini nao wakajitokeza wa kutosha mpaka jezi ikawa imechafuka kwa matangazo ya wadhamini.
Miaka michache baadae akatumbuliwa na hayati Magufuli, hatimae na mrija wa pesa ukapungua, wadhamini wakajitoa Singida ikashuka na kusahaulika ligi kuu bara.
Aliporudishwa kwenye Baraza la Mawaziri enzi ya Magufuli, akakaa kwa adabu bila kujihusisha na umiliki wa timu.
Baada ya kifo cha hayati Magufuli, Mama Samia akawa Rais na kumchagua Mwigulu kuwa Waziri wa Fedha. Ndani ya mwaka mmoja tu, tayari timu yake mpya aliyoinunua ya DTB imepanda daraja huku baadhi ya wachezaji waliopandisha timu hiyo wakiwa ni wale wale waliotumika enzi ya Singida Utd.
Japo amekuwa akikanusha kuwa yeye sio mmiliki, lakini ukweli siku zote haujifichi. DTB ina mastaa kibao kama Juma Abdul, Amis Tambwe, David Mwantika, Nicholaus Gyan, Tafazwa Kutinyu, na wengineo wengi.
Hizi fedha huwa anatoa wapi? Ni kwanini huwa anamiliki akiwa na cheo tu Serikalini?