Katavi: TAKUKURU yabaini usimamizi mbovu katika miradi ya Serikali

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,851
12,088

Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Katavi, Faustine Maijo amesema miradi inayotekelezwa na Serikali kwa manufaa ya Wananchi inashindwa kukamilika kwa wakati kutokana na baadhi ya Watumishi wa Serikali kushindwa kuisimamia ipasavyo.

Maijo amesema Watumishi wa Serikali wanapaswa kuzingatia taratibu za usimamizi wa miradi ili iweze kukamilika kwa wakati.

Amesema Mtumishi atakayeshindwa kusimamia miradi ya Serikali Sheria kali zitachukuliwa dhidi yake ikiwemo kuwapeleka katika vyombo vya Kisheria.

Aidha, amewaomba Wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa taasisi hiyo ili kuzuia na kubaina uzembe au ubora katika miradi mbalimbali.
 
TAAKUUKUURUUU ni li mbwa lililochoka limevimbiwa minyama linajamba jamba tu na limekosa mwelekeo kabisaaa, kuna mambo yanafikirisha sana hawa jamaa wanalipwa na kodi za wananchi lakini sijawasikia wakifanya kweli kushughulikia mauzauza yanayoendelea huko Tanzania, kimsingi bora hata yule mjeda mara mia nane kuliko huyo polisi mwarabu hamna kitu kabisa tangu aingie ni uozo tu shame kabisa utaskia sijui wamekamata nesi na panadol nne , sijui mwalimu kala hela ya dawati moja wakati CAG kaffumua mauozo chungu nzima sasa unajiuliza hawa jamaa wanafanyaga nini
 
Back
Top Bottom