Kahama: Bertha Mabula adai polisi kutaka kumbambikia kesi ya ugaidi kutaka kulipua Mahakama Kuu

mwanamwana

JF-Expert Member
Aug 1, 2011
1,077
4,114
Bertha.jpg

Bertha Mabula amesema anahofia usalama wake kwa madai ya kubaini Polisi Mjini Kahama wanataka kumbambikia kesi ya ugaidi wakidai alitaka kulipua Mahakama Kuu Kanda ya Shinyanga wakati akifuatilia mwenendo wa shauri lake kwa ajili ya kukata rufani.

Bertha amedai alifika Mahakama Kuu kwa ajili ya kuchukua mwenendo wa shauri la madai dhidi ya mfanyabiashara Tumsime Tibaijuka ili akakate rufani kwa kutoridhishwa na uamuzi wa mahakama hiyo.

"Wakati naenda mahakamani Shinyanga nilikodi teksi inayoendeshwa na Beatus Mandali, alinifikisha akanisubiri nilipomaliza kupata huduma tuligeuza kurudi Kahama, nilipata taarifa kuna Polisi walikuwa wananisubiri maeneo ya Tinde wanikamate, lakini kwa bahati ilinyesha mvua kubwa, wakati tunapita eneo hilo hawakutuona.

"Siku ya pili nilipata taarifa dereva Beatus alikamatwa na askari akiwa katika kituo chake cha kazi, akapelekwa Kituo cha Polisi Kahama akituhumiwa kubeba gaidi anayetaka kulipua mahakama," amedai Bertha.

Amedai dereva alipofikishwa kituoni alihojiwa kisha akaachiwa na kuambiwa asimjulishe kuhusu tukio hilo, lakini dereva aliamua kumsimulia Bertha kuwa anatafutwa kwa tuhuma za ugaidi.

"Derava aliponiambia nilimpigia simu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Janeth Magomi kumfahamisha njama hizo na akaahidi atafuatilia tukio hilo.

"Niliendelea kuwasiliana naye kwa njia ya WhatsApp na meseji zote ninazo nikimfahamisha hofu yangu ya kubambikiwa kesi hiyo, akasema angekuja Kahama, lakini bado nasubiri huenda atakuja," amedai Bertha.

Dereva teksi, Beatus akithibitisha tukio la kukamatwa kwake kwa njia ya simu, amedai alikamatwa akiwa stendi anapofanyia kazi, askari walikwenda na karandinga la polisi kumkamata.

"Askari waliniambia wananikamata kwa sababu jana nilibeba magaidi walikuwa wamevaa hijabu, nilijibu niliyembeba kumpeleka Shinyanga mahakamani alikuwa kavaa dera.

"Walinikamata kwa kuwa nilikuwa na gari niliendesha gari yangu kuelekea Kituo cha Polisi Kahama huku nyuma nikisindikizwa na karandinga la Polisi.

"Nilihojiwa nikiwa katika ofisi ya upelelezi, niliulizwa jana nilienda wapi, nilijibu Shinyanga, nikaambiwa nilibeba magaidi wamevaa hijabu, nilijibu niliyembeba alikuwa kavaa dera, askari aliandika maelezo kwenye simu kubwa, mwingine alikuwa kabeba bunduki ndiye aliyekuwa ananipiga picha.

"Maelezo yalitumwa sikujua yalitumwa wapi, baada ya kumaliza mpelelezi, Edes Jackson aliniambia nisiende kumwambia mtu yeyote, lakini dada Bertha aliponipigia nilimwambia," amedai.

Amedai baada kumwambia Bertha alipigiwa simu na Afande Edes akamwambia alidhani ana bichwa kubwa anazo akili kumbe hana akili.

“Niliwindwa tangu mchana sikuwapo mjini, nilipoingia wakaja kunikamata, waliniambia walinivizia Tinde jana, lakini walishangaa nilipitaje hawakuniona.

"Nilikamatwa mbele ya watu wengi kituoni na waliponifuatilia kunitoa walijibiwa niko Polisi kwa ajili ya uchunguzi," amedai.

Askari mmoja anayetuhumiwa kuwapo katika msafara wa kumkamata dereva huyo alipopigiwa simu kuulizwa kuhusu tukio hilo, Afande Edes Jackson, alidai haruhusiwi kutoa taarifa yoyote kwa sababu sio msemaji.

"Unaniulizaje maswali hayo, sina mamlaka ya kutoa taarifa, muulize RPC Shinyanga, unakuja kwangu mwenye renki ndogo hivi, kwa akili ya utu uzima uliyonayo kwani mtu kukamatwa lazima aingizwe mahabusu.

"Unaweza kutuhumiwa ukakamatwa, ukapekuliwa na kuachiwa, hizo taarifa kaulize mkoani watakujibu alikamatwa, alikaa mahabusu muda gani msiniulize mimi," alidai Afande Edes akimjibu mwandishi kwenye simu.

Mfanyabiashara Tumsime anayetuhumiwa wakati dereva anakamatwa askari alimpigia simu kuuza shauri lilikuwa namba ngapi, alipoulizwa kwa kupigiwa simu kuhusu hoja hiyo alidai anamfahamu Bertha Mabula na walikuwa na kesi ambayo imeshatolewa uamuzi.

"Masuala kwamba nawafahamu askari waliomkamata dereva, mimi siwajui na kama alikamatwa kituoni kutakuwa na taarifa zake, huyo dereva wake pia simjui," amedai Tumsime.

Akizungumzia tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Magomi amedai hana taarifa za Bertha kutaka kukamatwa kwa tuhuma za ugaidi.

"Taarifa za huyo mfanyabiashara kutaka kukamatwa mimi sina na bahati nzuri huwa nina tabia ya kukagua vitabu, Bertha Mabula, wala simjui.

"Kama anasema tuliwasiliana kwa simu labda nilisahau kama binadamu, sikumbuki, unajua kufanya kazi kwa simu mtu kama binadamu unaweza kusahau, mimi nipo aje kuniona," amedai RPC Magomi.

Baada ya shauri la madai kutupiliwa mbali, Bertha amewasilisha kusudio la kukata rufani akipinga hukumu ya Mahakama Kuu Shinyanga kwa madai kwamba hakutendewa haki na ushahidi wake wa maandishi pamoja na mashahidi wengine watano wa upande wake haukuzingatiwa.

Pamoja na kufanya hivyo pia Machi 28, mwaka huu alimwandikia barua Jaji Kiongozi yenye kichwa cha habari kutoridhishwa na uamuzi uliotolewa na Jaji Frank Mahimbali, kwenye shauri namba 03/2023.

Katika shauri hilo, mdai Bertha Mabula dhidi ya Tumsime Tibaijuka na Tunel Incorporation Limited, anadai Sh. milioni 295 alizomkopesha Tumsime kwa ajili ya kufanya biashara, ambazo anadai hajawahi kuzilipa.

Chanzo: Nipashe
 
Ni kosa kubwa sana hawa Polisi wanalifanya wanawafundisha watu walipue mahakama na ofisi zao wao waendelee kuwafundisha Raia wema kwamba hata mahakama inaweza kulipuliwa ipo siku watakuja kujuta sana...
 
Ndio tuelewe madai ya katiba mpya ni muhimu na sio kuachia CHADEMA peke yao kutupigania,ingawa maelezo ni ya upande mmoja still yanaonyesha ni jinsi gani walimia meno nchini hapa wanahangaika,hapa police ni suspects kwa hiyo hawawezi kujichunguza ili kuleta haki,kesi hii kwa katiba mpya,ofisi mbili zingechunguza kwa haki PP na IPID,kinyume cha hapo hakuna kitakachofanyika hapo,mdai haki ameshatishwa hapo na hii itakua cold case,kesi ya yule mzazi aliyefiwa na mwanae shuleni pale Lindi ipo wapi? Cold case
 
Katiba inahitaji mtu mmoja tu mwenye akili timamu, public figure mwenye ushawishi kuongoza jahazi la kudai katiba

Sasa kule chadema kina lissu wapo wapo km uji tu kazi kujiropokea
Ndio tuelewe madai ya katiba mpya ni muhimu na sio kuachia CHADEMA peke yao kutupigania,ingawa maelezo ni ya upande mmoja still yanaonyesha ni jinsi gani walimia meno nchini hapa wanahangaika,hapa police ni suspects kwa hiyo hawawezi kujichunguza ili kuleta haki,kesi hii kwa katiba mpya,ofisi mbili zingechunguza kwa haki PP na IPID,kinyume cha hapo hakuna kitakachofanyika hapo,mdai haki ameshatishwa hapo na hii itakua cold case,kesi ya yule mzazi aliyefiwa na mwanae shuleni pale Lindi ipo wapi? Cold case
 
Katiba inahitaji mtu mmoja tu mwenye akili timamu, public figure mwenye ushawishi kuongoza jahazi la kudai katiba

Sasa kule chadema kina lissu wapo wapo km uji tu kazi kujiropokea
Wakati wewe umefwata mkia wako ,push back yako ipo wapi
 
Mahakama na polisi lao moja nakumbuka pia mahakama imewahi kuwafungulia kesi ya kukutwa na nyaraka za serikali/nyara na uhujumu uchumu baada ya mtu huyo kuwasilisha nyaraka na mihuri ya mahakama zilizookotwa kwa Jaji kwa shinikizo la Naibu Msajili -Kanda ya Sumbawanga na kufunguliwa kesi wakidai lazima wamfunge lakini waligonga mwamba baada ya mahakimu na waendesha mashitaka kujitoa mara kwa mara na kuachishwa kazi Naibu Msajili huyo pamoja na kuamishwa kwa RCO,mwendesha mashitaka wa mkoa,na kustafu kwa jaji mfawidhi Mrango ambao walikuwa kundi moja kitu kilichopelekea Kaimu Jaji Mfawidhi Mh.Mkea aliruhusu dhamana na baadae mtuhumiwa kuachiwa kwa mashahidi kutofika mahakamani akiwemo mtoa taarifa Mtaki
 
Katika shauri hilo, mdai Bertha Mabula dhidi ya Tumsime Tibaijuka na Tunel Incorporation Limited, anadai Sh. milioni 295 alizomkopesha Tumsime kwa ajili ya kufanya biashara, ambazo anadai hajawahi kuzilipa.

Soma hukumu ya kurasa 41 :

Jaji wa mahakama kuu mheshimiwa F.H Mahimbali J katika utangulizi wa hukumu yake anasisitiza msemo wa KiSwahili " Mali bila Daftari huisha bila Habari" - mwisho wa nukuu. . ......Taarifa hiyo inarejelea tu umuhimu wa kutunza rekodi za fedha za biashara ipasavyo, ambazo zinaweza kupatikana wakati wowote ikihusisha biashara fulani ili kumsaidia mtu kujua mali na madeni yake....

Soma Hukumu nzima :

Tanzania Citation


Bertha Mabula Kinungu and Another

vs

Tumsime Modest Tibaijuka
and Another (Civil Case No. 3 of 2023) [2024] TZHC 735 (8 March 2024)

....msemo wa KiSwahili " Mali bila Daftari huisha bila Habari" The statement is simply referring to the importance of keeping financial records of business properly, which can be retrieved at any time involving a particular business to aid one know his/her assets and liabilities. ....

Source: Bertha Mabula Kinungu and Another vs Tumsime Modest Tibaijuka and Another (Civil Case No. 3 of 2023) [2024] TZHC 735 (8 March 2024)
 
Back
Top Bottom