Idriss Deby Itno ashinda uchaguzi Chad

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,506
9,289
Kiongozi wa kijeshi nchini Chad Mahamat Idriss Deby Itno ndiye mshindi wa uchaguzi uliofanyika wiki hii, kulingana na matokeo ya awali yaliyotangazwa usiku wa kuamkia Ijumaa.

Matokeo hayo yamepingwa na mpinzani wake mkuu Succes Masra. Matokeo hayo yaliyokuwa yanatarajiwa Mei 21, yametolewa wiki moja mapema, na yamemuonesha Deby Itno akiwa na asilimia 61 ya kura huku Masra akipata asilimia 18.5 ya kura hizo. Kumesikika milio ya risasi N'djamena baada ya matokeo hayo kutangazwa.

Chad ilifanya uchaguzi wake baada ya kucheleweshwa kwa muda mrefu, huku ikiwa chini ya utawala wa kijeshi kwa miaka mitatu. Wachambuzi wanasema walitarajia ushindi kwa Mahamat Deby Itno ambaye yuko madarakani.

Njama ya kuchakachua matokeo​


Deby Itno alichukua madaraka baada ya babake aliyekuwa uongozini kwa kipindi cha miongo mitatu, kuuwawa katika mapambano na waasi mwaka 2021.


Nchi hiyo yenye utajiri wa mafuta na yenye idadi ya watu milioni 18, haijafanya uchaguzi huru na haki tangu ilipopata uhuru wake 1960 kutoka kwa Ufaransa.

Saa chache kabla kutolewa kwa tangazo hilo la tume inayosimamia uchaguzi wa Chad, Masra alichapisha hotuba katika mtandao wa kijamii wa Facebook, akizituhumu mamlaka nchini humo kwa njama ya kutaka kuchakachua matokeo.

==============================

Chad's state election body said on Thursday interim president Mahamat Idriss Déby had won the May 6 presidential election outright with over 60 percent of the vote, citing provisional results, even as his main challenger declared himself the winner.

The electoral commission said Déby beat his prime minister Succès Masra, who only garnered 18.53 percent. The results are due to be confirmed by the Constitutional Council.

Masra claimed victory earlier on Thursday, saying that the election results were being manipulated.

Déby was proclaimed transitional president by fellow army generals in 2021 after his father, Idriss Déby Itno, who had ruled Chad with an iron fist for 30 years, was killed in a gun battle with rebels.

The interim leader promised an 18-month transition to democracy but then extended it by two years.

Opposition figures have since fled, been silenced or joined forces with Déby.

Déby's cousin and chief election rival Yaya Dillo Djérou was shot point-blank in the head in an army assault on February 28, according to his party.

The International Federation for Human Rights had warned that the election appeared "neither credible, free nor democratic".

The International Crisis Group also noted that "a number of problems in the run-up to the balloting cast doubt on its credibility".
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom