Huyu Mwanamke tangu alipokuja kwangu kang'ang'ania kukaa hataki kuondoka

mahatmaxlla

JF-Expert Member
Nov 26, 2017
882
1,399
Wakuu habari za muda na wakati kama huu.

Binafsi naamini wengi wetu tu wazima wa afya na wale wachache wenye changamoto fulani kiafya basi Mungu awatie nguvu na awape steps zingine ahead.

Niende kwenye mada moja kwa moja.
mnamo tarehe sita ya mwezi wa saba mwaka jana niliamishwa kituo cha kazi sasa niko mkoani huku kanda ya kati.
Nimeishi mwenyewe kwa mwezi mmoja na nusu mpaka kufikia mwezi wa tisa nikawa nimepata mwanamke wa kuishi nae.mwanamke huyu nilikutana nae jioni moja ndani ya supermarket akiwa anapata mahitaji yake kama ilivyo kawaida.

Tuliongea vizuri hiyo siku tukabadilishana namba,kesho yake tuliongea vizuri zaidi kwa njia ya simu tukapanga kukutana,sikuwaza sana kuhusu mazingira ama eneo la kukutana nikamwambia aje kwangu nae hakusita akakubali.

Kweli kesho ingine jioni mida ya saa kumi na mbili alifika kwangu tukapata chakula pamoja tukafurahi tukalana kisawa sawa mpaka mida ya saa nne usiku.nikajaribu kumwambia kuhusu kumpigia dereva wangu wa tax amrudishe,manzi akasema sio mbaya ata akilala kwa siku hiyo moja kwani sijapenda kampani yake?mwanaume nikasema aah! kulala tu sio big deal sana lala tu mama i real appreciate your company

Manzi akalala,usiku mzima ikawa ni fujo tu.....gheto likageuka msitu mtoto full kucheza na miti.asubuhi hii hapa nikaamka mapema nikajianda kabla sijaondoka nikamuachia maelekezo nikaingia mzigoni,nikajua nikirudi sito mkuta coz ndo tulivokubaliana na alisema nimuachie funguo moja then akija next time atakuja nayo.

Jioni narudi ghetto namkuta ndani karelax na wala hana ata wasiwasi tena kapiga deki vizuri kapulizia malashi katandika kitanda katulia anatizama movie.na kubwa zaidi kapika mpaka na chakula cha jioni.

Daah!sikutaka kuhoji sana maana alivonipokea nilijihisi kama mfalme vile. chap maji yakapelekwa bafuni nikapewa taulo moja kwa moja kuoga.siku ya pili ikapita ya tatu ya nne narudi toka mzigoni nakuta mtoto kafatia nguo zingine kwake.

Kumbe nilikuoa nimeoa bila kujua wakuu,mwezi ukaisha miezi mitatu ikapita mwezi wa kumi na mbili mwishoni nikasema kiukweli siwezi oa kifala namna hii.wakati udsm na mtoto mkali kumzidi na tayari nimezaa nae mtoto mmoja,kwanini huyu manzi wa mkoani anigande kiasi hiki.

Nikamueleza kuwa nina mke yuko dar anasoma na ninamtoto nae tayari na hivi karibuni atakuja kuniona sasa inakuwaje hapo hebu tushauriane tunafanyaje mamaangu ww mwenyewe si unaelewa tulivokutana mimi na ww.jibu alonipa nilichoka zaidi,akaniambia yy aje tutakuwa wote....nikamjibu mama si unakwako akasema ndio ila nimepafunga na hapa kwako siondoki.wakuu hapo ndo nilipo jua kwanini dunia duara.

Kwa kifupi tulizozana sana ikabidi niwe nakodi chumba cha mshikaji wangu mwingine ambae muda mwingi anakuwa safarini.hiki chumba ndo huwa nakutana na huyu babe mama wangu nilie zaa nae.

Siku ya leo ndo kanikela zaidi huyu mwanamke nilie oa bila kutegemea.na hii ndo sababu pekee ya mimi kuandika uzi huu.amenipigia simu niko kibanda umiza nachek game ya yanga.......kwamba anashida na laki mbili na nusu kuna emegency imetokea alinipa maelekezo kibao sana nikasema ni kweli sina budi kumsaidia.....nikamuelekeza sehemu yenye hela nikakata simu nikaendelea kutizama burudani.

Mpira umeisha nimerudi nyumbani cha ajabu sijakuta mtu,nimekaa ndani ya masaa mawili mwanamke karudi amefika tu ananiomba samahani mara oooh mume samahani nimetumia laki yako nyingine pasi na kukushirikisha hvyo naomba unisamehe nimechukua laki tatu na nusu badala ya laki mbili na nusu kama ulivyo niambia.na nimeshatumia hivyo naomba unisamehe.

Kabla ajamaliza kusema nikamwambia hebu nyamaza kimya kwanza.nikawa nimevimba nikatoka nje nikatafakari sana.mpaka sasa sielewi nifanyaje,haipiti wiki tunagombana sana ana amri na mbishi na king'ang'anizi mno.asione unachart au unaongea na simu utakula kofi la mgongo ht sms ikiingia saa sita za usiku ikiwa ya mwanamke basi utaeleza kwanini imeingia muda huo.miezi yote hiyo tuloishi nae kila nilipokuwa namwambia kuhusu kurudi kwake hakuwahi kunielewa ht mara moja.na binafsi sina mpango wa kufunga nae pingu za maisha ni yeye tu na ubishi wake.

Ushauri wenu kwangu:
Wakuu nifanyaje mbona sielewi ina maana ndo nimeoa hivi hivi!napitia wakati mgumu sana na mgogoro wa nafsi na stress nyingi mno.kuna muda najichukia nakujiona mjinga wa mwisho.najuta na nailaani vikali ile siku na saa pale supermarket.

Nisaidieni natokaje hapa.
 
Asante kwa Chai.

images (1) (1).jpeg


PambanaZaidi/CottonandMore
 
Wakuu habari za muda na wakati kama huu.

Binafsi naamini wengi wetu tu wazima wa afya na wale wachache wenye changamoto fulani kiafya basi Mungu awatie nguvu na awape steps zingine ahead.

Niende kwenye mada moja kwa moja.
mnamo tarehe sita ya mwezi wa saba mwaka jana niliamishwa kituo cha kazi sasa niko mkoani huku kanda ya kati.
Nimeishi mwenyewe kwa mwezi mmoja na nusu mpaka kufikia mwezi wa tisa nikawa nimepata mwanamke wa kuishi nae.mwanamke huyu nilikutana nae jioni moja ndani ya supermarket akiwa anapata mahitaji yake kama ilivyo kawaida.

Tuliongea vizuri hiyo siku tukabadilishana namba,kesho yake tuliongea vizuri zaidi kwa njia ya simu tukapanga kukutana,sikuwaza sana kuhusu mazingira ama eneo la kukutana nikamwambia aje kwangu nae hakusita akakubali.

Kweli kesho ingine jioni mida ya saa kumi na mbili alifika kwangu tukapata chakula pamoja tukafurahi tukalana kisawa sawa mpaka mida ya saa nne usiku.nikajaribu kumwambia kuhusu kumpigia dereva wangu wa tax amrudishe,manzi akasema sio mbaya ata akilala kwa siku hiyo moja kwani sijapenda kampani yake?mwanaume nikasema aah! kulala tu sio big deal sana lala tu mama i real appreciate your company

Manzi akalala,usiku mzima ikawa ni fujo tu.....gheto likageuka msitu mtoto full kucheza na miti.asubuhi hii hapa nikaamka mapema nikajianda kabla sijaondoka nikamuachia maelekezo nikaingia mzigoni,nikajua nikirudi sito mkuta coz ndo tulivokubaliana na alisema nimuachie funguo moja then akija next time atakuja nayo.

Jioni narudi ghetto namkuta ndani karelax na wala hana ata wasiwasi tena kapiga deki vizuri kapulizia malashi katandika kitanda katulia anatizama movie.na kubwa zaidi kapika mpaka na chakula cha jioni.

Daah!sikutaka kuhoji sana maana alivonipokea nilijihisi kama mfalme vile. chap maji yakapelekwa bafuni nikapewa taulo moja kwa moja kuoga.siku ya pili ikapita ya tatu ya nne narudi toka mzigoni nakuta mtoto kafatia nguo zingine kwake.

Kumbe nilikuoa nimeoa bila kujua wakuu,mwezi ukaisha miezi mitatu ikapita mwezi wa kumi na mbili mwishoni nikasema kiukweli siwezi oa kifala namna hii.wakati udsm na mtoto mkali kumzidi na tayari nimezaa nae mtoto mmoja,kwanini huyu manzi wa mkoani anigande kiasi hiki.

Nikamueleza kuwa nina mke yuko dar anasoma na ninamtoto nae tayari na hivi karibuni atakuja kuniona sasa inakuwaje hapo hebu tushauriane tunafanyaje mamaangu ww mwenyewe si unaelewa tulivokutana mimi na ww.jibu alonipa nilichoka zaidi,akaniambia yy aje tutakuwa wote....nikamjibu mama si unakwako akasema ndio ila nimepafunga na hapa kwako siondoki.wakuu hapo ndo nilipo jua kwanini dunia duara.

Kwa kifupi tulizozana sana ikabidi niwe nakodi chumba cha mshikaji wangu mwingine ambae muda mwingi anakuwa safarini.hiki chumba ndo huwa nakutana na huyu babe mama wangu nilie zaa nae.

Siku ya leo ndo kanikela zaidi huyu mwanamke nilie oa bila kutegemea.na hii ndo sababu pekee ya mimi kuandika uzi huu.amenipigia simu niko kibanda umiza nachek game ya yanga.......kwamba anashida na laki mbili na nusu kuna emegency imetokea alinipa maelekezo kibao sana nikasema ni kweli sina budi kumsaidia.....nikamuelekeza sehemu yenye hela nikakata simu nikaendelea kutizama burudani.

Mpira umeisha nimerudi nyumbani cha ajabu sijakuta mtu,nimekaa ndani ya masaa mawili mwanamke karudi amefika tu ananiomba samahani mara oooh mume samahani nimetumia laki yako nyingine pasi na kukushirikisha hvyo naomba unisamehe nimechukua laki tatu na nusu badala ya laki mbili na nusu kama ulivyo niambia.na nimeshatumia hivyo naomba unisamehe.

Kabla ajamaliza kusema nikamwambia hebu nyamaza kimya kwanza.nikawa nimevimba nikatoka nje nikatafakari sana.mpaka sasa sielewi nifanyaje,haipiti wiki tunagombana sana ana amri na mbishi na king'ang'anizi mno.asione unachart au unaongea na simu utakula kofi la mgongo ht sms ikiingia saa sita za usiku ikiwa ya mwanamke basi utaeleza kwanini imeingia muda huo.miezi yote hiyo tuloishi nae kila nilipokuwa namwambia kuhusu kurudi kwake hakuwahi kunielewa ht mara moja.na binafsi sina mpango wa kufunga nae pingu za maisha ni yeye tu na ubishi wake.

Ushauri wenu kwangu:
Wakuu nifanyaje mbona sielewi ina maana ndo nimeoa hivi hivi!napitia wakati mgumu sana na mgogoro wa nafsi na stress nyingi mno.kuna muda najichukia nakujiona mjinga wa mwisho.najuta na nailaani vikali ile siku na saa pale supermarket.

Nisaidieni natokaje hapa.
Picha?
 
Jini hilo🤣🤣🤣🤣.

Ndio mkome kuparamia paramia watu ovyo🤣.

Ukute alikesha sana kwenye maombi mixer waganga wa kienyeji kuomba mume. Sasa mume umejipeleka mwenyewe unatarajia akuache.

Mtaani kugumu ndugu. Ukute hiyo supermarket uliyomkuta alikuwa kwenye mingo ya kufuatilia majibu ya sala zake. Mara kidume ukajitokeza na shobo zako🤣🤣🤣.

Na ukitaka kuisoma namba hasa jitusue umpe mimba.
 
Kwa ulivyo elezea naona kwakifupi huyo mwanamke hakufai na atakusumbua sana mkuu.
Jambo la pili naona kama wewe ni aina ya vijana wenye malengo na misimamo lakini madomo zege na wenye hofu ya kutongoza lakini wapenda nyabe.
Kama vipi tafuta nyumba nyingine kimya kimya, then fanya namna huyo mwanamke asafiri hata kwenda kwao/ama aende sehem siku nzima then akitoka tu.... hama chap na kisha umuachie vitu vyake tu humo ndani.
Usipo fanya hivyo naona kabisa unaenda kuandaliwa mimba chap na ndipo utakua umepigwa lock na kwa muandiko wako ndio naona hautoweza kujichomoa kabisaaaa alafu utaanza mawazo ya kujiua.
 
Japo siamini kama ni kweli,lakini acha nikupe mbinu. Kama umefikia hatua ya kuwa na akiba ndani,unajiweza. Kitu kama hiki kiliwahi tokea. Ikawa hivi: siku moja,mwambie hapo hapawafai,unatafuta nyumba nyingine mhamie. Kama siku 2 badae, mwambie apange kila kitu,usiku mtahama. Chukua gari,pakia vyako. Vikiisha,begi lake shusha,panda gari. Mwambie mhusika,umekodi wewe,haingii mtu kasoro wewe na vitu vyako. Tembea.
Hili ukiona ni gumu,vitu vyote weka,mwambie kwenye gari hamtoshi,mtaenda na pikipiki. Utajua mwenyewe mazingira umeyaandaaje. Fika sehemu,agizeni hata soda. Toka kama unaenda uani,panda pikipiki. Begi la chupi utajua kama utalitunza,utamrudishia au utalitupa.
Ila sasa,somo umepata, uhuni na uzinzi acha. Shobo zako ndo chanzo cha hayo.
 
Hii ilitaka kunikuta, nimechukua namba dada kumbe anasali kwa mwamposa huko kashaambiwa atakaetaka namba ndio mumeo. Siku ya pili anafosi aje kwangu, nikamuelekeza akachukua bajaji akaja mpaka sehemu nilipokuwa mbali kidogo na kwangu. Katika stori nikamwambia pale napokaa kuna dada ananisaidia kupika nampa mahitaji kwa hiyo ukimkuta kwangu usistuke maana huwa namuachia funguo aniwekee msosi kabisa ila anapenda movie so tunaweza kumkuta kwangu kajiachia, dada akasema sasa nikifika kwako si atanichukia maana utawala wake wa kukupikia utakuwa umeisha nimeuchukua mimi, nikasema thubutuuu, nikatafuta sababu akarudi alipotoka.
 
Back
Top Bottom