Huyu Mwanajeshi aliyekuwa akihutubia leo si ndiyo yule muuza madafu wa Ikulu, au?

Kumbe haujawahi kuona... Nilijua haipo kabisa. Ndio ipo Advanced Training ambayo wewe unataka kuaminisha watu fikra zako kwamba haipo
I got you exactly where I want you!

Haya, tell me…..what kind of takedown defenses are they taught in their advanced mixed martial arts training?

What types of submissions are they taught?
 
  • Kicheko
Reactions: K11
Huwezi kulinganisha fighting skills za special forces na za professional MMA fighter.

Totally two different things.

Mjinga hapa ni wewe.
Wakili Msomi Ngabu umemuona komando wetu wa kitanganyika?

Jamaa ana kakifua aseee, ametuna kidari dizaini fulani hivi ila naamini hata wewe ukimuwahi za chembe mbili tu anatema ulimi nje. Mchumba sana huyu!

Ukiwapiganisha hawa makomando wetu (wa kitanganyika) na makomando wa uRaya au US (USA baby) wanachakazwa mbaya!

Achana na US wewe, kombora moja tu komando wetu chali!

Kideri na maini vyote vinaparaganyika na kusawajika.
 
Wakili Msomi Ngabu umemuona komando wetu wa kitanganyika!

Jamaa ana kakifua aseee, ametuna kidari dizaini fulani hivi ila naamini hata wewe ukimuwahi za chembe mbili tu anatema ulimi nje. Mchumba sana huyu!

Ukiwapiganisha hawa makomando wetu (wa kitanganyika) na makomando wa uRaya au US (USA baby) wanachakazwa mbaya.

Achana na US wewe, kombora moko tu komando chali.
Ukiwa vitani halafu ujikute unahitaji kupigana ngumi ili ujinasue, umekwisha!
 
Ukiwa vitani halafu ujikute unahitaji kupigana ngumi ili ujinasue, umekwisha!
Technology is key katika nyakati hizi.

Hawa watunisha videri mimi siwaaminigi kivile, halafu wamefanyiwa brainwashing mbaya huko kwenye mafunzo yao wanajikuta nunda fulani hivi!

Nina kaka yangu ni mjeda ila nikimuangalia siku hizi namuona kama liroboti fulani. He is no longer rational.

Kitanganyika mwanajeshi ni ngumi zaidi na mabavu, ndivyo walivyofundishwa hivyo.

Ukiwa njema unamfumua vizuri tu unamsigina na anatulia.
 
Awali ya yote wanakidoni Binafsi Huwa hatupendi kushabikia jambo bila kujuwa nyuma ya pazia Kuna Nini?

Siku zote ukiona mtu wa operation ana expose ile operation basi ktk jicho lakijasusi maswali Huwa mengi ila pia Huwa na majibu.

Sio jambo lakawaida mtu alie undercover kuwa exposed sio rahisi.

Mossad ambao chini ya vikosi vyao maalumu vya assassination wamekuwa na haka katabia ila mara zote Huwa wanatoa hizo taarifa baada ya miongo kadhaa. Mfano nikatikamiaka ya hivi karibuni Dunia imeweza kujuwa vile Mossad walifanya mauwaji ya kulipiza kwa viongozi wa Hamas kutokana na mauwaji ya Munich German ambapo Waziri Mkuu wa wakati ule aliapa kila alie panga au kutekeleza Yale mauwaji lazima auwawe. Hii ni moja ya operation ngumu sana ilio tekelezwa na Mossad chini ya special force Kidon🤔.

Ktk Dunia ya ujasusi kila kitu kinawezekana. Ikumbukwe ktk Taifa lolote duniani Kuna special walinzi wa Rais ambao hawa hutoka ktk idara nyeti za usalama na jeshi. Ni team ambayo wanasema Huwa inabadilika baada ya muda wa Rais kuisha.🤔

Nikatika team hii ambayo imesheheni wadunguaji na viumbe hatari ktk Tasinia ya usalama ndio Huwa na aina hii ya watu, wauza mahindi, matunda au kuchoma nyama yes hawa ni special unit ya ulinzi wa Rais ambao huratibu usalama wa Rais na vile wanaweza cheza na hisia zenu.

Inasemekana huko miaka ya nyuma jeshi kilikuwa halina intelligence yake jambo lilikuwa likileta shida ktk mambo ya taarifa. Hivyo chini ya wanakidoni wa Tz ikaanzishwa hiyo military intelligence ambayo matokeo yake ndio hayo mnaona sasa. Nadhani mnanielewa.

Twende kwenye awali why mchoma mahindi amegeuka kuwa komando japo yeye anakataa jambo Hilo kitu ambachobni sahihi maana hatokubali. Haya Yesu ashuke maana kukiri kwake kwaweza kuwa ndio mwisho wa safari yake.😭🤐.

Kuna somo kubwa sana ktk ulimwengu wakijasusi lazima wa Tanzania mjifunze nakuamka sasa. Kiufupi Amiri jeshi mkuu wa majeshi ya Tz ametuma msg ngumu sana kwa watanzania na wale wanamzunguka.

Msg yake nifupi sana Mimi ni mama ila msinichukue poa. Nimevaa gauni ila ndani Nina combat ya kikomando na tusifanyiane mchezo.

Ndugu zangu kiufupi hapo Jirani panafuka Moshi na zipo taarifa amabazo sio rasmi Tz wanataka chomoa better 🤐

Ila wanashauriwa kabla ya kuchomoa yatawakuta mambo magumu sana hivyo mna pewa wosia muwe makini. Ndio sura ni ya mchoma mahindi ila Yeye sie mchoma mahindi mmemfananisha🤐🤔
Mnahangaika burw hakuna Ujasusi hapo.

Ni Maigizo ya Mama kuonesha kwamba anapenda Wanyonge hadi wauza madafu...na tukio la jana ndio kazi halisi ya Kachero.

Sasa kuna ujasusi gani hapo?
 
I got you exactly where I want you!

Haya, tell me…..what kind of takedown defenses are they taught in their advanced mixed martial arts training?

What types of submissions are they taught?

I got you exactly where I want you!

Haya, tell me…..what kind of takedown defenses are they taught in their advanced mixed martial arts training?

What types of submissions are they taught?
Mi pia nilijua utakimbilia huko kujionyesha kwamba na wewe si haba kwenye Martial Arts.. Nilishawahi kukuambia huko kabla huwa huna hoja za maana kulinda Facts zako. Ujinga wako mwingi huwa unajaribu kuuficha kwenye Vingereza vingi ambavyo havina maana katika kulinda hoja zako. Utoto mwingi sana
 
Ndugu zangu Watanzania,

Jana hapa nilileta andiko langu nikasema kuwa nimefanya uchunguzi wa kina sana tena sana wa kuchunguza watu hawa wawili kati ya yule komandoo aliyekuwa kiongozi wa kikosi maalumu cha makomando pamoja na yule kijana muuza madafu wa ikulu. Ambapo watu walikuwa wanasema ni mtu mmoja.jambo ambalo mimi nililipinga sana japo andiko langu likaja kuunganishwa na lingine na hivyo kuzima hoja yangu kwa njia hiyo.

Sasa ukweli ni ukweli tu hata ukipingwa na watu wengi lakini unabakia kuwa ukweli tu. Mimi jana nilipingwa na kushambuliwa sana humu jukwaani na wengine kunitukana matusi kuwa mimi nimekurupuka,wengine kusema mimi ni chawa nisiye na akili na wengine kusema mimi ni hasara na aibu hata kwa wazazi walionizaa. Nilivumilia hali na udhalilishaji wote kwa kuwa mimi ni mvumilivu na mtu mwenye ngozi ngumu .hivyo nikaamua kuwasamehe tu kama kawaida yangu.

Sasa leo Ayo Tv wamemtafuta yule muuza madafu wa ikulu na kumfanyia mahojiano ambapo kwa sasa ameweza kununua boda boda mpya kutokana na pesa aliyoipata siku ile Ikulu ,ambapo ameongezea kwenye ile aliyokuwa nayo kama akiba yake.amesema hata yeye alishangaa sana watu walipoanza kumfananisha na yeye mwenyewe aliangalia maadhimisho yale na kushangaa.

Ndugu zangu Watanzania tusipende kufuata mikumbo na kusombwa na ujinga unaokuwa umeanzishwa na mtu mmoja na kuufanya kusambaa kama moto wa petroli na kila mtu kuanza kuiamini bila kufanya utafiti.Mimi huwa sikurupuki na kuanza kuamini jambo na kulisambaza bila kujilidhisha ukweli wa jambo husika.ndio maana jana baada ya uchunguzi wangu wa kina na Elimu yangu ya kumsoma mtu katika uso wake juu ya mfanano ,hasa kwa kuangalia macho,pua,mdomo,paji la uso,upana wa sura ,umbile la mdomo wakiwa wamefumba mdomo ,mkao wa pua kutoka juu pamoja na muonekano wao kwa ujumla nikaja kugundua kwa haraka haraka kuwa ni watu wawili tofauti kabisa.

Ninashangaa watu wengine wenye heshima zao nao waliingia kwenye mkumbo huo wa kuamini taarifa zile za kizushi kabisa.tujifunze kuwa watafiti na watulivu katika mambo mbalimbali na siyo kumezeshwa tu Matango pori au kuimbishwa kama makasuku. Kukumbwa kamwe na katu usimuamini mtu katika habari au taarifa yoyote ile bila ya wewe kujiridhisha ndio ukaitoa.

Leo mimi ni shujaa japo jana nilionekana kama mjinga na mwehu.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom