Hidaya Kimbunga Mawinguni na Watoto Pekupeku Wanacheza Mpira wa Makaratasi Barabarani

Mohamed Said

JF-Expert Member
Nov 2, 2008
21,071
30,419
KIMBUNGA HIDAYA MAWINGUNI WATOTO WANACHEZA MPIRA WA MAKARATASI PEKUPEKU MTAANI

Jioni inakimbilia Maghrib na kama kungekuwa na jua mtu angeweza kuliona limebadilika rangi linaenda kuzama upande wa magharibi.

Toka asubuhi hali ni ya mawingu na baridi baada ya mvua ya usiku kucha na upepo mkali jana.

Hali hii ya leo si ya kawaida Dar es Salaam.


View: https://youtu.be/ZkTLHAj_KOw?si=4LCpDR_mR13qXwSN
Binafsi hali inanikumbusha hali kama hii Glasgow miaka mingi iliyopita.

Taa zimewashwa hata zile za mitaani saa saba mchana unadhani usiku.

Watu wanakuwa hawana raha na hawa ni wenyeji wameishi maisha hayo ya giza kuingia mchana na baridi kali toka kuzaliwa kwao.

Kwangu mgeni upweke ule wa kutoona watu nje kama kawaida inaongeza ukiwa na majonzi.

Afadhali ukiwa London au mji wowote ule lakini si Glasgow, Uskochi tangia mwanzo ni mji ambao kwa kiasi fulani umejiinamia na watu weusi wachache sana.

Nimekaa kibaraza cha Masjid Nur jirani na kwangu naangalia watoto wanacheza mpira barabarani.

Umeme hakuna toka asubuhi.
Ndani nyumbani giza tupu.

Naogopa kuwasha taa ya solar isije ikesha chaji na usiku ikawa tabu zaidi.

Majonzi.

Watoto hawa mimi nilipokuwa umri wao nacheza mpira kwenye kiwanja na nimevaa Adidas na bukta na sichezi mpira wa makaratasi kama huu wanaocheza wao.

Hapa nazungumza mwaka wa 1966 si leo 2024.

2024 watoto wanacheza mpira pekupeku tena wa makaratasi.

Nashusha pumzi.
Nimeelemewa kwa fikra.

Nimetoa simu yangu nawapiga video hawa watoto huku nikowaombea dua wasianguke kwani wanacheza mpira sehemu ya mbele ya nyumba ambayo mwenyewe kwa kutafuta usafi ameweka zege sawa na upana wa nyumba yake.

Kawatengenezea watoto kiwanja cha mpira cha zege mtaani watoto wamepate mahali pa kucheza.

Fikra imerudi kwa Hidaya.
Si hidayi kimbunga.

Hidaya alikuwa mtoto mwenzangu tunasoma darasa moja la kwanza Lutheran Primary School, Moshi baadae shule hii ikawa Stanley Primary School.

Kila siku asubuhi nakutana na Hidaya njiani tunaongozana kwenda shule pamoja.

Sisi wawili peke yetu njia nzima.
Sote tuna umri wa miaka saba.

Nikaondoka Moshi kuja Dar es Salaam niko darasa la tano.

Miaka mingi ikapita nafanya kazi Tanga na wateja wangu wasafirishaji kahawa kupitia bandari ya Tanga wako Moshi na Arusha.

Nikawa sipungui Moshi na kila nikifika Moshi nikawa wakati mwingine napita nje ya nyumbani kwa kina Hidaya lakini haikunijia fikra ya kumuuliza.

Siku moja nikiwa Moshi kwenye barza yangu ya hapo mjini ambayo wengi wa wanabarza ni wenzangu ambao tulisoma sote utotoni shule ya msingi nikamuuliza Hidaya.

''Hidaya kafariki siku hizi za karibuni alikuwa nurse Mawenzi Hospital.''

Hili ndilo jibu nililopewa.

Huwezi kuhisi ni kiasi gani moyo uliniuma kwa majonzi.

Miaka zaidi ya 40 imepita nilipokuwa na Hidaya tukienda shule pamoja.

Leo nikiwa pale kibaraza cha Masjid Nur 'mood'' yangu iko chini kwa hali ya hewa achilia mbali ile kuwa nawatazama watoto wanacheza mpira wa makaratasi pekupeku mwaka wa 2024.

Ubongo ni injini ya ajabu sana.

Uwezo wake ni mkubwa unaweza kukupeleka kwingi ukiwa hapo ulipokaa bila ya hata kunyanyua mguu.

Kulikuwa na fundi mshoni Magomeni Mtaa wa Dosi na Jaribu jina lake Hidaya.

Hidaya maana yake ni zawadi na ni jina la kike.
Fundi Hidaya alikuwa mwanamme.

Hidaya alikuwa mshoni wa nguo bingwa.

Leo kwa Fundi Hidaya ilipokuwa barza kubwa ya vijana watoto wa mjini hakuna mtu.

Ndiyo nikiwa pale nikawa nimesafiri hadi Uingereza 1990s nikarudi Dar es Salaam 1960s na Moshi nikienda shule asubuhi nimeongozana na marehemu Hidaya.

Hivi namaliza kuandika mvua imeanza kunyesha na nasikia Adhana Sala ya Isha kutoka Masjid Nur.


View: https://youtu.be/ZkTLHAj_KOw?si=4LCpDR_mR13qXwSN
 
1715283715790.png
Umewahi kuwa na rafiki mkristo?
Mna...
Naam nimewahi wake kwa waume:

NAMKUMBUKA RAFIKI YANGU WA UDOGONI GERSHOM CHIHOTA (1950 - 2023)

Kiasi cha kama siku tatu zilizopita nimepokea taarifa kutoka kwa Ally Max Marekani.

Ajabu jinsi kifo kinavyoweza kufungua majalada ndani ya ubongo wa binadamu.

Nataka kuanza na Ally Max.

Ally Max ni mdogo sana kwetu hapa nakusudia kwangu mimi na kwa marehemu Gershom kwani siku Ally alipokuja St. Joseph's kuanza shule mimi nilikuwa nimesimama sehemu tukiita ''School Compound.''

Ally alikuwa kashikwa mkono na dada yake Eyshe (Allah amrehemu).

Nyumba ya Mzee Abbas Max muasisi wa TANU Iringa na nyumba ya kina Chihota zilikuwa zimetenganishwa na uwanja mdogo wa mpira ambao watoto wa hapo mtaani wakicheza.

Ally Max akimjua Gershom toka udogo wake.

Hapa ni Magomeni Mikumi sisi vijana wa wakati ule tukipaita ''Soulville.''

Hii ilikuwa miaka ya mwishoni 1960 umri wetu ulikuwa wastani wa miaka 15.

Soulville ilikuwa kipande tu cha Magomeni Mikumi ambako wazee wetu wengi wao waliokuwa na nyadhifa kubwa serikalini walijenga nyumba zao hapo: Nyerere, Machapati, Muhuto, Mgone, Bakuname, Mwakinyo, Kandoro, Kambona, Chief Fundikira, Ntare, Mzena na Abdul na Ally Sykes kwa kutataja wachache.

Hii Soulville ni nini?

Huu ulikuwa wakati wa muziki wa ''Soul'' muziki uliokuwa unaeleza maisha ya mtu mweusi Amerika.

Wazimu wa muziki huu na sisi ulitusibu Dar es Salaam na tuliweza hata tukaupiga na ulikuwa unatoka Detroit mji ambao Ally Max leo anaishi.

Siku ya Jumatano shule ilikuwa mwisho saa sita mchana.

Hii ndiyo ilikuwa siku mchana wake na Jumamosi na Jumapili tunakutana Mikumi kupiga magitaa.

Gersom alikuwa ''Bassist'' hodari sana akitumia mkono wa kushoto.

Mimi nikimtania nikimwambia anapiga bass mkono wa kushoto kama Paul Mc Cartney wa The Beatles.

Gershom akicheza mpira vizuri sana akitumia mguu wa kushoto lakini mapenzi yake yalikuwa kwenye muziki.

Gershom Chihota tulikutana St. Joseph's mwaka wa 1967 na tukawa marafiki wakubwa sana tuko pamoja muda mwingi.

Kupitia kwake nikawajua kaka zake Raymond na Norman Chihota.

Norman akisoma Azania na alikuwa bingwa wa taifa wa mbio fupi mita 100 kiwango cha kimataifa kwani aliwakilisha Tanzania Michezo ya Commonwealth na kwengine kwingi.

Sifa ya Gershom ilikuwa ni upole kiasi tukampa lakabu tukimwita, ''Cool Kid.''

Kabla ya akina Chihota kuhamia Mikumi walikuwa wakikaa Temeke Wailesi na kupia kwake nikaja kufahamiana na vijana wenzangu wazaliwa wa Temeke Mick Jones (Mikidadi), Choggy Sly (Salum), Allah Brown (Ali Ngota) na nduguze wa kiume wote.

Baba yake Gershom, Mzee Chihota alihama Southern Rhodesia (Zimbabwe) kuja Tanganyika kutafuta maisha.

Ulipofunguliwa Ukumbi wa Arnautoglo Mzee Chihota akawa ndiyo meneja wake.

Mzee Chihota akapata nafasi ya kwenda kusoma Uingereza na huko akafariki na kuzikwa huko huko.

Nyumbani kwa kina Gershom kulikuwa na picha inamuonyesha mama yetu amekaa pembeni ya kaburi la mumewe.

Mama alikwenda Uingereza kulizuru kaburi la mume wake.

Mama yetu huyu alifanyakazi Ikulu hadi Zimbabwe ilipopata uhuru ndipo akarudi Zimbabwe miaka ya 1980.

Si muda mrefu watoto wake wakamfuata.

Mwaka wa 1993 nilikwenda Harare na nilimtafuta Gershom.

Nakumbuka mshangao alioupata baada ya kubisha hodi mlango wake na yeye akatoka akanikuta nimesimama mbele yake namtazama.

Gershom alikuwa wakati ule akifanya kazi Monamotapa Hotel moja ya hoteli kubwa sana Harare.

Wakati niko Harare Manu Dibango alikuwa mjini akifanya maonyesho.

Gershom na mimi tulimzungumza kidogo lakini nadhani rafiki yangu alitambua kuwa miaka imebadilika.

Gershom hakugusia kuniambia twende tukamsikilize Manu Dibango.

Ninachokumbuka tulizungumza kuhusu taarifa kutoka magazetini watu waliokwenda kwenye onyesho lake wakilalamika kuwa hakuwapigia nyimbo yake maarufu ''Soul Makosa,'' lau kama walimuomba afanye hivyo.

TAAZIA ILIYOCHELEWA: DR. EDITH KITAMBI

Nimesoma kuhusu kifo cha Dr. Edith Kitambi leo keshafariki muda mrefu na watu wameandika kama kumbukumbu.

Kwangu mimi ikawa ni msiba mpya na machungu yake naomboleza wakati wenzangu weshapoa.

Nilimfahamu Edith University of Wales Cardiff mwaka wa 1991 sote tukiwa Postgraduate Students kutoka Tanzania.

Alinizoea zaidi alipojua kuwa mimi na Ledgar Tenga aliyekuwa mchezaji wa Yanga na Timu ya Taifa ni marafiki.

Tenga ni kaka yake.

Alikuwa bint mzuri wa tabia na sura.

Nakumbuka yeye ndiye aliyenipa jina la "Sheikh" pale Cardiff na likaniganda kiasi jina langu likafa na wanafunzi kutoka Tanzania wote wakawa wananiita, "Sheikh."

Ukisikia Sheikh basi hakuna mwengine ila mimi.

Sababu ya jina hili ni kuwa ilikuwa kila Jumamosi kuna mahali nadhani ilikuwa club wanafunzi wengi wakienda kucheza disco na kujiburudisha na vinywaji.

Cardiff ni mji mdogo sana ukifananisha na London na miji mingine ya Uingereza kama Liverpool hivyo hata sehemu za starehe si nyingi watu hukutana mahali pamoja siku zote.

Ikawa siku zinapita wanafunzi wenzangu hawanioni kujumuika na wao.

Ulaya kwa mgeni ni mahali pa upweke sana ingawa mimi nilikuwa nimeshafika Uingereza kabla na napaelewa kwa kiasi kidogo.

Siku moja Edith akaniuliza kulikoni?

Nikistarehe sana kuzungumza na Edith sababu yeye tofauti na wengine wote alikuwa akisema Kiswahili kwa "accent" ya Dar es Salaam kabisa, utasema mwanamke wa Kizaramo wa Kariakoo.

Nilipata kumuuliza imekuwaje akaniambia kuwa yeye lau ni Mchagga lakini kazaliwa na kukulia Dar-es-Salaam.

Ikawa sasa hata tukiwa na party za Watanzania 9 Desemba au Sabasaba hanioni kucheza muziki na Edith akitaka kuninyanyua kucheza namtuliza kwa kumwambia Sheikh hachezi dansi.

Yeye akiishia kucheka.

Na Edith akifanya hivi kwa kutumwa na wenzake ili wapate kucheka kwa kumuona sheikh anamwagika kwenye "dance floor."

Miaka ile kulikuwa na bendi kutoka Kenya, "Virunga," "Mazembe" ambazo miziki yake ikipendwa na kuvuma hadi Ulaya katika jumuiya za watu weusi.

Nakumbuka hawa Virunga walipata kufika Cardiff na wanafunzi kutoka Kenya wakawa wanauza tiketi za dansi.

Kulikuwa katika party zile muziki wa Judy Baucher sina hakika na hili jina yeye alikuwa na nyimbo za "blues" hizi zikiwatoa fahamu vijana wengi khasa mashairi yake ya mapenzi.

Nyimbo hizi zilikuwa lazima zipigwe.
Party za Watanzania zikinoga sana.

Vijana wa Kizungu walikuwa haziwapiti wakiwapenda sana dada zetu zaidi wanavyojua kucheza.

Ulaya ukialikwa party unakwenda na kinywaji chako.

Edith masikini akipenda kunitania nami siku zote nikimchekesha kwa kumwambia mie mzee na sheikh siwezi kucheza muziki afanye staha.

Tukazoeana sana nikawa nimepata pia daktari kidogo nikijisikia namwendea.

Edith alikuwa anafanya shahada ya pili katika Public Health.

Nakumbuka alipata kuniambia kuwa kwa tatizo nililokuwanalo la tumbo atanitibia kwa njia ya "food elimination," na akaniwekea orodha ya kutokula vyakula fulani kimoja baada ya kingine kwa muda mfupi niangalie tatizo langu kama litaendelea au la.

Nilipona.

Alipata siku moja kunipa mhadhara mzima wa ukimwi.

Akaniambia ni tabu mtu kupata ukimwi akiwa kajituliza lakini ni rahisi kuugua akiwa kinyume chake.

Akanieleza kuwa yeye katibia wagonjwa wengi na hili kaligundua kutokana na utafiti wake katika "lifestyles."

Nilimwacha Dr. Edith Kitambi Cardiff lakini nilipata kurudi tena Uingereza, London kwa muda mfupi nilimtembelea nyumbani kwake.

Baada ya hapo sikupata taarifa zake hadi leo zaidi ya miaka 30 kupita nasikia amefariki.

Nitaingia Maktaba kuangalia picha za Cardiff nikipata picha yake nitaiweka hapa.

1715283442496.jpeg

Gershom Chihota
1715283708647.png

Wa pili kushoto Dr. Edith Kitambi, Cardiff, 1992.​
 
Nchi sahv imekuwa ya ajabu sana
Watoto hawana sehemu maalumu za kucheza wanaishia kucheza barabarani na vichochoroni
Maeneo ya wazi yote hii serikali na chama chake wanauza maeneo ama kuwapangisha watu
Nchi ya ajabu sana hii

Ova
 
Mna...
Naam nimewahi wake kwa waume:

NAMKUMBUKA RAFIKI YANGU WA UDOGONI GERSHOM CHIHOTA (1950 - 2023)

Kiasi cha kama siku tatu zilizopita nimepokea taarifa kutoka kwa Ally Max Marekani.

Ajabu jinsi kifo kinavyoweza kufungua majalada ndani ya ubongo wa binadamu.

Nataka kuanza na Ally Max.

Ally Max ni mdogo sana kwetu hapa nakusudia kwangu mimi na kwa marehemu Gershom kwani siku Ally alipokuja St. Joseph's kuanza shule mimi nilikuwa nimesimama sehemu tukiita ''School Compound.''

Ally alikuwa kashikwa mkono na dada yake Eyshe (Allah amrehemu).

Nyumba ya Mzee Abbas Max muasisi wa TANU Iringa na nyumba ya kina Chihota zilikuwa zimetenganishwa na uwanja mdogo wa mpira ambao watoto wa hapo mtaani wakicheza.

Ally Max akimjua Gershom toka udogo wake.

Hapa ni Magomeni Mikumi sisi vijana wa wakati ule tukipaita ''Soulville.''

Hii ilikuwa miaka ya mwishoni 1960 umri wetu ulikuwa wastani wa miaka 15.

Soulville ilikuwa kipande tu cha Magomeni Mikumi ambako wazee wetu wengi wao waliokuwa na nyadhifa kubwa serikalini walijenga nyumba zao hapo: Nyerere, Machapati, Muhuto, Mgone, Bakuname, Mwakinyo, Kandoro, Kambona, Chief Fundikira, Ntare, Mzena na Abdul na Ally Sykes kwa kutataja wachache.

Hii Soulville ni nini?

Huu ulikuwa wakati wa muziki wa ''Soul'' muziki uliokuwa unaeleza maisha ya mtu mweusi Amerika.

Wazimu wa muziki huu na sisi ulitusibu Dar es Salaam na tuliweza hata tukaupiga na ulikuwa unatoka Detroit mji ambao Ally Max leo anaishi.

Siku ya Jumatano shule ilikuwa mwisho saa sita mchana.

Hii ndiyo ilikuwa siku mchana wake na Jumamosi na Jumapili tunakutana Mikumi kupiga magitaa.

Gersom alikuwa ''Bassist'' hodari sana akitumia mkono wa kushoto.

Mimi nikimtania nikimwambia anapiga bass mkono wa kushoto kama Paul Mc Cartney wa The Beatles.

Gershom akicheza mpira vizuri sana akitumia mguu wa kushoto lakini mapenzi yake yalikuwa kwenye muziki.

Gershom Chihota tulikutana St. Joseph's mwaka wa 1967 na tukawa marafiki wakubwa sana tuko pamoja muda mwingi.

Kupitia kwake nikawajua kaka zake Raymond na Norman Chihota.

Norman akisoma Azania na alikuwa bingwa wa taifa wa mbio fupi mita 100 kiwango cha kimataifa kwani aliwakilisha Tanzania Michezo ya Commonwealth na kwengine kwingi.

Sifa ya Gershom ilikuwa ni upole kiasi tukampa lakabu tukimwita, ''Cool Kid.''

Kabla ya akina Chihota kuhamia Mikumi walikuwa wakikaa Temeke Wailesi na kupia kwake nikaja kufahamiana na vijana wenzangu wazaliwa wa Temeke Mick Jones (Mikidadi), Choggy Sly (Salum), Allah Brown (Ali Ngota) na nduguze wa kiume wote.

Baba yake Gershom, Mzee Chihota alihama Southern Rhodesia (Zimbabwe) kuja Tanganyika kutafuta maisha.

Ulipofunguliwa Ukumbi wa Arnautoglo Mzee Chihota akawa ndiyo meneja wake.

Mzee Chihota akapata nafasi ya kwenda kusoma Uingereza na huko akafariki na kuzikwa huko huko.

Nyumbani kwa kina Gershom kulikuwa na picha inamuonyesha mama yetu amekaa pembeni ya kaburi la mumewe.

Mama alikwenda Uingereza kulizuru kaburi la mume wake.

Mama yetu huyu alifanyakazi Ikulu hadi Zimbabwe ilipopata uhuru ndipo akarudi Zimbabwe miaka ya 1980.

Si muda mrefu watoto wake wakamfuata.

Mwaka wa 1993 nilikwenda Harare na nilimtafuta Gershom.

Nakumbuka mshangao alioupata baada ya kubisha hodi mlango wake na yeye akatoka akanikuta nimesimama mbele yake namtazama.

Gershom alikuwa wakati ule akifanya kazi Monamotapa Hotel moja ya hoteli kubwa sana Harare.

Wakati niko Harare Manu Dibango alikuwa mjini akifanya maonyesho.

Gershom na mimi tulimzungumza kidogo lakini nadhani rafiki yangu alitambua kuwa miaka imebadilika.

Gershom hakugusia kuniambia twende tukamsikilize Manu Dibango.

Ninachokumbuka tulizungumza kuhusu taarifa kutoka magazetini watu waliokwenda kwenye onyesho lake wakilalamika kuwa hakuwapigia nyimbo yake maarufu ''Soul Makosa,'' lau kama walimuomba afanye hivyo.

TAAZIA ILIYOCHELEWA: DR. EDITH KITAMBI

Nimesoma kuhusu kifo cha Dr. Edith Kitambi leo keshafariki muda mrefu na watu wameandika kama kumbukumbu.

Kwangu mimi ikawa ni msiba mpya na machungu yake naomboleza wakati wenzangu weshapoa.

Nilimfahamu Edith University of Wales Cardiff mwaka wa 1991 sote tukiwa Postgraduate Students kutoka Tanzania.

Alinizoea zaidi alipojua kuwa mimi na Ledgar Tenga aliyekuwa mchezaji wa Yanga na Timu ya Taifa ni marafiki.

Tenga ni kaka yake.

Alikuwa bint mzuri wa tabia na sura.

Nakumbuka yeye ndiye aliyenipa jina la "Sheikh" pale Cardiff na likaniganda kiasi jina langu likafa na wanafunzi kutoka Tanzania wote wakawa wananiita, "Sheikh."

Ukisikia Sheikh basi hakuna mwengine ila mimi.

Sababu ya jina hili ni kuwa ilikuwa kila Jumamosi kuna mahali nadhani ilikuwa club wanafunzi wengi wakienda kucheza disco na kujiburudisha na vinywaji.

Cardiff ni mji mdogo sana ukifananisha na London na miji mingine ya Uingereza kama Liverpool hivyo hata sehemu za starehe si nyingi watu hukutana mahali pamoja siku zote.

Ikawa siku zinapita wanafunzi wenzangu hawanioni kujumuika na wao.

Ulaya kwa mgeni ni mahali pa upweke sana ingawa mimi nilikuwa nimeshafika Uingereza kabla na napaelewa kwa kiasi kidogo.

Siku moja Edith akaniuliza kulikoni?

Nikistarehe sana kuzungumza na Edith sababu yeye tofauti na wengine wote alikuwa akisema Kiswahili kwa "accent" ya Dar es Salaam kabisa, utasema mwanamke wa Kizaramo wa Kariakoo.

Nilipata kumuuliza imekuwaje akaniambia kuwa yeye lau ni Mchagga lakini kazaliwa na kukulia Dar-es-Salaam.

Ikawa sasa hata tukiwa na party za Watanzania 9 Desemba au Sabasaba hanioni kucheza muziki na Edith akitaka kuninyanyua kucheza namtuliza kwa kumwambia Sheikh hachezi dansi.

Yeye akiishia kucheka.

Na Edith akifanya hivi kwa kutumwa na wenzake ili wapate kucheka kwa kumuona sheikh anamwagika kwenye "dance floor."

Miaka ile kulikuwa na bendi kutoka Kenya, "Virunga," "Mazembe" ambazo miziki yake ikipendwa na kuvuma hadi Ulaya katika jumuiya za watu weusi.

Nakumbuka hawa Virunga walipata kufika Cardiff na wanafunzi kutoka Kenya wakawa wanauza tiketi za dansi.

Kulikuwa katika party zile muziki wa Judy Baucher sina hakika na hili jina yeye alikuwa na nyimbo za "blues" hizi zikiwatoa fahamu vijana wengi khasa mashairi yake ya mapenzi.

Nyimbo hizi zilikuwa lazima zipigwe.
Party za Watanzania zikinoga sana.

Vijana wa Kizungu walikuwa haziwapiti wakiwapenda sana dada zetu zaidi wanavyojua kucheza.

Ulaya ukialikwa party unakwenda na kinywaji chako.

Edith masikini akipenda kunitania nami siku zote nikimchekesha kwa kumwambia mie mzee na sheikh siwezi kucheza muziki afanye staha.

Tukazoeana sana nikawa nimepata pia daktari kidogo nikijisikia namwendea.

Edith alikuwa anafanya shahada ya pili katika Public Health.

Nakumbuka alipata kuniambia kuwa kwa tatizo nililokuwanalo la tumbo atanitibia kwa njia ya "food elimination," na akaniwekea orodha ya kutokula vyakula fulani kimoja baada ya kingine kwa muda mfupi niangalie tatizo langu kama litaendelea au la.

Nilipona.

Alipata siku moja kunipa mhadhara mzima wa ukimwi.

Akaniambia ni tabu mtu kupata ukimwi akiwa kajituliza lakini ni rahisi kuugua akiwa kinyume chake.

Akanieleza kuwa yeye katibia wagonjwa wengi na hili kaligundua kutokana na utafiti wake katika "lifestyles."

Nilimwacha Dr. Edith Kitambi Cardiff lakini nilipata kurudi tena Uingereza, London kwa muda mfupi nilimtembelea nyumbani kwake.

Baada ya hapo sikupata taarifa zake hadi leo zaidi ya miaka 30 kupita nasikia amefariki.

Nitaingia Maktaba kuangalia picha za Cardiff nikipata picha yake nitaiweka hapa.
Hakika mzee Said leo umekumbuka mbali sana. Maandiko haya yanaonyesha namna una kumbukumbu timamu inayodumu.
 
Mna...
Naam nimewahi wake kwa waume:

NAMKUMBUKA RAFIKI YANGU WA UDOGONI GERSHOM CHIHOTA (1950 - 2023)

Kiasi cha kama siku tatu zilizopita nimepokea taarifa kutoka kwa Ally Max Marekani.

Ajabu jinsi kifo kinavyoweza kufungua majalada ndani ya ubongo wa binadamu.

Nataka kuanza na Ally Max.

Ally Max ni mdogo sana kwetu hapa nakusudia kwangu mimi na kwa marehemu Gershom kwani siku Ally alipokuja St. Joseph's kuanza shule mimi nilikuwa nimesimama sehemu tukiita ''School Compound.''

Ally alikuwa kashikwa mkono na dada yake Eyshe (Allah amrehemu).

Nyumba ya Mzee Abbas Max muasisi wa TANU Iringa na nyumba ya kina Chihota zilikuwa zimetenganishwa na uwanja mdogo wa mpira ambao watoto wa hapo mtaani wakicheza.

Ally Max akimjua Gershom toka udogo wake.

Hapa ni Magomeni Mikumi sisi vijana wa wakati ule tukipaita ''Soulville.''

Hii ilikuwa miaka ya mwishoni 1960 umri wetu ulikuwa wastani wa miaka 15.

Soulville ilikuwa kipande tu cha Magomeni Mikumi ambako wazee wetu wengi wao waliokuwa na nyadhifa kubwa serikalini walijenga nyumba zao hapo: Nyerere, Machapati, Muhuto, Mgone, Bakuname, Mwakinyo, Kandoro, Kambona, Chief Fundikira, Ntare, Mzena na Abdul na Ally Sykes kwa kutataja wachache.

Hii Soulville ni nini?

Huu ulikuwa wakati wa muziki wa ''Soul'' muziki uliokuwa unaeleza maisha ya mtu mweusi Amerika.

Wazimu wa muziki huu na sisi ulitusibu Dar es Salaam na tuliweza hata tukaupiga na ulikuwa unatoka Detroit mji ambao Ally Max leo anaishi.

Siku ya Jumatano shule ilikuwa mwisho saa sita mchana.

Hii ndiyo ilikuwa siku mchana wake na Jumamosi na Jumapili tunakutana Mikumi kupiga magitaa.

Gersom alikuwa ''Bassist'' hodari sana akitumia mkono wa kushoto.

Mimi nikimtania nikimwambia anapiga bass mkono wa kushoto kama Paul Mc Cartney wa The Beatles.

Gershom akicheza mpira vizuri sana akitumia mguu wa kushoto lakini mapenzi yake yalikuwa kwenye muziki.

Gershom Chihota tulikutana St. Joseph's mwaka wa 1967 na tukawa marafiki wakubwa sana tuko pamoja muda mwingi.

Kupitia kwake nikawajua kaka zake Raymond na Norman Chihota.

Norman akisoma Azania na alikuwa bingwa wa taifa wa mbio fupi mita 100 kiwango cha kimataifa kwani aliwakilisha Tanzania Michezo ya Commonwealth na kwengine kwingi.

Sifa ya Gershom ilikuwa ni upole kiasi tukampa lakabu tukimwita, ''Cool Kid.''

Kabla ya akina Chihota kuhamia Mikumi walikuwa wakikaa Temeke Wailesi na kupia kwake nikaja kufahamiana na vijana wenzangu wazaliwa wa Temeke Mick Jones (Mikidadi), Choggy Sly (Salum), Allah Brown (Ali Ngota) na nduguze wa kiume wote.

Baba yake Gershom, Mzee Chihota alihama Southern Rhodesia (Zimbabwe) kuja Tanganyika kutafuta maisha.

Ulipofunguliwa Ukumbi wa Arnautoglo Mzee Chihota akawa ndiyo meneja wake.

Mzee Chihota akapata nafasi ya kwenda kusoma Uingereza na huko akafariki na kuzikwa huko huko.

Nyumbani kwa kina Gershom kulikuwa na picha inamuonyesha mama yetu amekaa pembeni ya kaburi la mumewe.

Mama alikwenda Uingereza kulizuru kaburi la mume wake.

Mama yetu huyu alifanyakazi Ikulu hadi Zimbabwe ilipopata uhuru ndipo akarudi Zimbabwe miaka ya 1980.

Si muda mrefu watoto wake wakamfuata.

Mwaka wa 1993 nilikwenda Harare na nilimtafuta Gershom.

Nakumbuka mshangao alioupata baada ya kubisha hodi mlango wake na yeye akatoka akanikuta nimesimama mbele yake namtazama.

Gershom alikuwa wakati ule akifanya kazi Monamotapa Hotel moja ya hoteli kubwa sana Harare.

Wakati niko Harare Manu Dibango alikuwa mjini akifanya maonyesho.

Gershom na mimi tulimzungumza kidogo lakini nadhani rafiki yangu alitambua kuwa miaka imebadilika.

Gershom hakugusia kuniambia twende tukamsikilize Manu Dibango.

Ninachokumbuka tulizungumza kuhusu taarifa kutoka magazetini watu waliokwenda kwenye onyesho lake wakilalamika kuwa hakuwapigia nyimbo yake maarufu ''Soul Makosa,'' lau kama walimuomba afanye hivyo.

TAAZIA ILIYOCHELEWA: DR. EDITH KITAMBI

Nimesoma kuhusu kifo cha Dr. Edith Kitambi leo keshafariki muda mrefu na watu wameandika kama kumbukumbu.

Kwangu mimi ikawa ni msiba mpya na machungu yake naomboleza wakati wenzangu weshapoa.

Nilimfahamu Edith University of Wales Cardiff mwaka wa 1991 sote tukiwa Postgraduate Students kutoka Tanzania.

Alinizoea zaidi alipojua kuwa mimi na Ledgar Tenga aliyekuwa mchezaji wa Yanga na Timu ya Taifa ni marafiki.

Tenga ni kaka yake.

Alikuwa bint mzuri wa tabia na sura.

Nakumbuka yeye ndiye aliyenipa jina la "Sheikh" pale Cardiff na likaniganda kiasi jina langu likafa na wanafunzi kutoka Tanzania wote wakawa wananiita, "Sheikh."

Ukisikia Sheikh basi hakuna mwengine ila mimi.

Sababu ya jina hili ni kuwa ilikuwa kila Jumamosi kuna mahali nadhani ilikuwa club wanafunzi wengi wakienda kucheza disco na kujiburudisha na vinywaji.

Cardiff ni mji mdogo sana ukifananisha na London na miji mingine ya Uingereza kama Liverpool hivyo hata sehemu za starehe si nyingi watu hukutana mahali pamoja siku zote.

Ikawa siku zinapita wanafunzi wenzangu hawanioni kujumuika na wao.

Ulaya kwa mgeni ni mahali pa upweke sana ingawa mimi nilikuwa nimeshafika Uingereza kabla na napaelewa kwa kiasi kidogo.

Siku moja Edith akaniuliza kulikoni?

Nikistarehe sana kuzungumza na Edith sababu yeye tofauti na wengine wote alikuwa akisema Kiswahili kwa "accent" ya Dar es Salaam kabisa, utasema mwanamke wa Kizaramo wa Kariakoo.

Nilipata kumuuliza imekuwaje akaniambia kuwa yeye lau ni Mchagga lakini kazaliwa na kukulia Dar-es-Salaam.

Ikawa sasa hata tukiwa na party za Watanzania 9 Desemba au Sabasaba hanioni kucheza muziki na Edith akitaka kuninyanyua kucheza namtuliza kwa kumwambia Sheikh hachezi dansi.

Yeye akiishia kucheka.

Na Edith akifanya hivi kwa kutumwa na wenzake ili wapate kucheka kwa kumuona sheikh anamwagika kwenye "dance floor."

Miaka ile kulikuwa na bendi kutoka Kenya, "Virunga," "Mazembe" ambazo miziki yake ikipendwa na kuvuma hadi Ulaya katika jumuiya za watu weusi.

Nakumbuka hawa Virunga walipata kufika Cardiff na wanafunzi kutoka Kenya wakawa wanauza tiketi za dansi.

Kulikuwa katika party zile muziki wa Judy Baucher sina hakika na hili jina yeye alikuwa na nyimbo za "blues" hizi zikiwatoa fahamu vijana wengi khasa mashairi yake ya mapenzi.

Nyimbo hizi zilikuwa lazima zipigwe.
Party za Watanzania zikinoga sana.

Vijana wa Kizungu walikuwa haziwapiti wakiwapenda sana dada zetu zaidi wanavyojua kucheza.

Ulaya ukialikwa party unakwenda na kinywaji chako.

Edith masikini akipenda kunitania nami siku zote nikimchekesha kwa kumwambia mie mzee na sheikh siwezi kucheza muziki afanye staha.

Tukazoeana sana nikawa nimepata pia daktari kidogo nikijisikia namwendea.

Edith alikuwa anafanya shahada ya pili katika Public Health.

Nakumbuka alipata kuniambia kuwa kwa tatizo nililokuwanalo la tumbo atanitibia kwa njia ya "food elimination," na akaniwekea orodha ya kutokula vyakula fulani kimoja baada ya kingine kwa muda mfupi niangalie tatizo langu kama litaendelea au la.

Nilipona.

Alipata siku moja kunipa mhadhara mzima wa ukimwi.

Akaniambia ni tabu mtu kupata ukimwi akiwa kajituliza lakini ni rahisi kuugua akiwa kinyume chake.

Akanieleza kuwa yeye katibia wagonjwa wengi na hili kaligundua kutokana na utafiti wake katika "lifestyles."

Nilimwacha Dr. Edith Kitambi Cardiff lakini nilipata kurudi tena Uingereza, London kwa muda mfupi nilimtembelea nyumbani kwake.

Baada ya hapo sikupata taarifa zake hadi leo zaidi ya miaka 30 kupita nasikia amefariki.

Nitaingia Maktaba kuangalia picha za Cardiff nikipata picha yake nitaiweka hapa.
Nakuhusudu mzee uko vizuri sana upstairs.
 
Back
Top Bottom