Shinyanga: Watumishi waliowagaragaza raia kwa kushindwa kulipa ushuru wasimamishwa kazi

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,441
8,261

Kufuatia video inayosambaa mtandaoni ikionesha Mtu akipatiwa adhabu ya kugalagala chini pamoja na kuruka kichura baada ya kukaidi kulipa ushuru wa halmashauri kwa watumishi wanaohusika na ukusanyaji wa ushuru katika halmashauri ya Msalala wilayani Kahama Mkoani Shinyanga Mkuu wa wilaya ya Kahama @mboni_mhita ametoa ufafanuzi wa tukio hilo

Tukio hilo lilitokea Mei 2, 2024 likiwahusisha watumishi watano wa halmashauri hiyo kutoa adhabu kwa mwananchi aliyekaidi kulipa ushuru.

Wasafi Media imemtafuta Mkuu wa wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita kupata ufafanuzi wa suala hilo ambapo amekiri uwepo wa tukio hilo pamoja hatua walizochukuwa kwa watumishi hao waliojihusisha na kutoa adhabu hiyo na kusema kuwa kitendo hicho ni kinyume cha sheria.
 
View attachment 2986286
Kufuatia video inayosambaa mtandaoni ikionesha Mtu akipatiwa adhabu ya kugalagala chini pamoja na kuruka kichura baada ya kukaidi kulipa ushuru wa halmashauri kwa watumishi wanaohusika na ukusanyaji wa ushuru katika halmashauri ya Msalala wilayani Kahama Mkoani Shinyanga Mkuu wa wilaya ya Kahama @mboni_mhita ametoa ufafanuzi wa tukio hilo

Tukio hilo lilitokea Mei 2, 2024 likiwahusisha watumishi watano wa halmashauri hiyo kutoa adhabu kwa mwananchi aliyekaidi kulipa ushuru.

Wasafi Media imemtafuta Mkuu wa wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita kupata ufafanuzi wa suala hilo ambapo amekiri uwepo wa tukio hilo pamoja hatua walizochukuwa kwa watumishi hao waliojihusisha na kutoa adhabu hiyo na kusema kuwa kitendo hicho ni kinyume cha sheria.
Zamani, Nilikuwa, najiuliza, iliwezekqnq vipi wazungu wakatoka ulaya, wakaja Afrika, wakatukimbiza, wakatukamata wakatufunga kamba, wakatupandisha kwenye meli na mijeredi, tukapelekwa utumwani!
Unyonge wa, kiwango wa cha juu, unakutq watumishi wapo watstu wananchi kumi, wanafanyiwa hv
 
Kuna wananchi wakaidi sana kulipa ushuru.

Wakusanya ushuru wanahitaji uwezo mkubwa wa kujizuia na hekima.

Mtu anaambiwa alipe ushuru lakini anajibu tu hataki, au mzigo haujajaa!
 
Zamani, Nilikuwa, najiuliza, iliwezekqnq vipi wazungu wakatoka ulaya, wakaja Afrika, wakatukimbiza, wakatukamata wakatufunga kamba, wakatupandisha kwenye meli na mijeredi, tukapelekwa utumwani!
Unyonge wa, kiwango wa cha juu, unakutq watumishi wapo watstu wananchi kumi, wanafanyiwa hv
Bado utumwa upo tu ila sasa boti la kwenda ulaya wanajazana wenyewe tena na kulipia juu
Kisa kuwa mkimbizi
Yaani maisha ya mwafrika daa
 
Back
Top Bottom