Ndata
JF-Expert Member
- Mar 2, 2017
- 226
- 321
Nimekuwa kimya kwa siku kadhaa nikiutazama muelekeo wa siasa zetu za upinzani haswa sasa tukiwa tunaelekea kwenye uchaguzi mkuu wa October 2020. Naona mapicha picha tuu.
Dhana ya kuona wengine CCM B inazidi kusambaa na wasambazaji wakubwa wakiwa ni Chadema na viongozi wao, yaani hadi kiongozi mkubwa tu kama Mdee naye anashiriki kuita wenzake CCM B.
CUF waliitwa Ccm B na Chadema kisha wakaungana Kuunga UKAWA, walipoulizwa uCcm B wa CUF wakatafuna maneno baada ya CUF msalaba wa Ccm B ukawaangukia ACT na Zitto akapewa cheo cha Yuda escsriot wa siasa za mageuzi.
Mwaka huu mwanachama mwenza wa UKAWA ambae ni NCCR anageuka kuwa Ccm B, kisa anakijenga chama chake. Jamani vyama viache kujijenga kisa vitaonekana Ccm B? Vyama vikatae wanachama wapya kisa vitaonekana Ccm B? Huu ni ujinga ujinga unaoanza kuonekana tabia ya Chadema.
Eti kwenda Ikulu, kwenye awamu ya Kikwete Chadema walienda Ikulu mara nyingi zaidi kuliko wapinzani wowote waliowahi kutokea nchi hii na hakuna yeyote aliyewaita Ccm B, Chadema wameenda Mwanza kuomba ushirikiano na serikali hakuna yeyote aliyewaona wanatumika.
Leo Mbatia kuonana na Rais kwa malengo yaleyale ya kuimarisha umoja na mshikamano wa nchi hii anaonekana mamluki, mole na kibaraka wa Ccm. Mbona Maalim alienda na tangu atoke huko hakuna anayemuita Ccm B.
Hofu yao ni Nccr kusema wanataka kuwa chama kikuu cha upinzani? Kama wamejipima na kuona hio ni hatua namba moja kuelekea hatua ya pili kuing'oa Ccm. Chadema wameongoza kambi rasmi ya upinzani bungeni kwa miaka kumi mfululizo awamu mbili ni lazima wawe na nguvu zote za kuing'oa Ccm Nccr lazima ipambane kupata wabunge ili nafasi ya Ccm ichukuliwe na Chadema na nafasi ya Chadema uchukuliwe na Nccr Ccm ifutike kabisa.
Tafakuri yangu ya kijinga jinga inaniambia Chadema wanahofu ya kupokonywa dhamana ya kuwa vibaraka wa Ccm na Nccr, Chadema ni mamluki na ndio maana kila uchaguzi unapokaribia wataleta migogoro ya ndani ili watu wapoteze mori ya mabadiliko.
Ndatama Hassan
Sent using Jamii Forums mobile app
Dhana ya kuona wengine CCM B inazidi kusambaa na wasambazaji wakubwa wakiwa ni Chadema na viongozi wao, yaani hadi kiongozi mkubwa tu kama Mdee naye anashiriki kuita wenzake CCM B.
CUF waliitwa Ccm B na Chadema kisha wakaungana Kuunga UKAWA, walipoulizwa uCcm B wa CUF wakatafuna maneno baada ya CUF msalaba wa Ccm B ukawaangukia ACT na Zitto akapewa cheo cha Yuda escsriot wa siasa za mageuzi.
Mwaka huu mwanachama mwenza wa UKAWA ambae ni NCCR anageuka kuwa Ccm B, kisa anakijenga chama chake. Jamani vyama viache kujijenga kisa vitaonekana Ccm B? Vyama vikatae wanachama wapya kisa vitaonekana Ccm B? Huu ni ujinga ujinga unaoanza kuonekana tabia ya Chadema.
Eti kwenda Ikulu, kwenye awamu ya Kikwete Chadema walienda Ikulu mara nyingi zaidi kuliko wapinzani wowote waliowahi kutokea nchi hii na hakuna yeyote aliyewaita Ccm B, Chadema wameenda Mwanza kuomba ushirikiano na serikali hakuna yeyote aliyewaona wanatumika.
Leo Mbatia kuonana na Rais kwa malengo yaleyale ya kuimarisha umoja na mshikamano wa nchi hii anaonekana mamluki, mole na kibaraka wa Ccm. Mbona Maalim alienda na tangu atoke huko hakuna anayemuita Ccm B.
Hofu yao ni Nccr kusema wanataka kuwa chama kikuu cha upinzani? Kama wamejipima na kuona hio ni hatua namba moja kuelekea hatua ya pili kuing'oa Ccm. Chadema wameongoza kambi rasmi ya upinzani bungeni kwa miaka kumi mfululizo awamu mbili ni lazima wawe na nguvu zote za kuing'oa Ccm Nccr lazima ipambane kupata wabunge ili nafasi ya Ccm ichukuliwe na Chadema na nafasi ya Chadema uchukuliwe na Nccr Ccm ifutike kabisa.
Tafakuri yangu ya kijinga jinga inaniambia Chadema wanahofu ya kupokonywa dhamana ya kuwa vibaraka wa Ccm na Nccr, Chadema ni mamluki na ndio maana kila uchaguzi unapokaribia wataleta migogoro ya ndani ili watu wapoteze mori ya mabadiliko.
Ndatama Hassan
Sent using Jamii Forums mobile app