Mbozi: Zahanati ya Kijiji yafungwa kwa kukosa Wahudumu. Wananchi wateseka

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,865
4,693
Zaidi ya wananchi 1,000 wa Kijiji cha Namwangwa, Kata ya Hezya Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe, wamekosa huduma za afya kwa miezi mitatu sasa, baada ya tabibu anayehudumu kwenye zahanati ya kijiji hicho kustaafu.

Wananchi hao wamekumbwa na changamoto hiyo baada ya mhudumu wa awali kustaafu tangu Novemba, 2023 na Serikali ilipeleka tabibu mwingine Februari, 2024 lakini mwezi uliopita amehamishwa na kusababisha zahanati hiyo ifungwe.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Mwananchi Digital leo Jumanne Aprili 16, 2024 kijijini hapo, baadhi ya wananchi wamesema zahanati hiyo ambayo ina uwezo wa kuhudumia wagonjwa 50 kwa siku, ilikuwa msaada mkubwa kwao, lakini sasa wanalazimika kufuata huduma maeneo mengine.

Mwananchi Digital imemtafuta Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Alex Mugeta ambaye amekiri zahanati hiyo kufungwa kwa kukosa mhudumu.

Hata hivyo, amesema tayari wameanza utaratibu wa kumpata tabibu mwingine na watakamilisha muda si mrefu, japo hakutaja ni lini hasa atapatikana.
 
Wakati hayo yanaendelea waziri was tamisemi anatenga mabilion kununua magari wakati wapiga kura wanakosa huduma,halafu utasikia hakuna ajira watu wajiajiri!!

Ajira zipo ndio hizo lakini tatizo vipaumbele vya serikali kunenepesha wanasiasa!!
 
Zaidi ya wananchi 1,000 wa Kijiji cha Namwangwa, Kata ya Hezya Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe, wamekosa huduma za afya kwa miezi mitatu sasa, baada ya tabibu anayehudumu kwenye zahanati ya kijiji hicho kustaafu...
Wauguzi na Matabibu wamejaa Mitaani.....a failed state.
 
  • Itakuwa ni maeneo ambayo mtu akipelekwa anawapa kuacha kazi kama hatohamishwa.
  • Kuna sehemu huko Mbozi hakukuwa na VEO anayeza kufanya kazi; kuna wazee 'watemi' hawasikii habari yoyote ya serikali; ikabidi DED atafute kijana wa kijiji hicho (mtoto wao) aliyehitimu kidato IV (bila kujali ufaulu wake) na kumwajiri kama VEO.
  • Huko mpaka sasa kama mtu yeyote hakubaliki na 'wazee; au akimbie au ndg zake wajiabdae kuomboleza.
 
Zaidi ya wananchi 1,000 wa Kijiji cha Namwangwa, Kata ya Hezya Wilaya ya Mbozi mkoani Songwe, wamekosa huduma za afya kwa miezi mitatu sasa, baada ya tabibu anayehudumu kwenye zahanati ya kijiji hicho kustaafu.

Wananchi hao wamekumbwa na changamoto hiyo baada ya mhudumu wa awali kustaafu tangu Novemba, 2023 na Serikali ilipeleka tabibu mwingine Februari, 2024 lakini mwezi uliopita amehamishwa na kusababisha zahanati hiyo ifungwe.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Mwananchi Digital leo Jumanne Aprili 16, 2024 kijijini hapo, baadhi ya wananchi wamesema zahanati hiyo ambayo ina uwezo wa kuhudumia wagonjwa 50 kwa siku, ilikuwa msaada mkubwa kwao, lakini sasa wanalazimika kufuata huduma maeneo mengine.

Mwananchi Digital imemtafuta Mganga Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, Alex Mugeta ambaye amekiri zahanati hiyo kufungwa kwa kukosa mhudumu.

Hata hivyo, amesema tayari wameanza utaratibu wa kumpata tabibu mwingine na watakamilisha muda si mrefu, japo hakutaja ni lini hasa atapatikana.
Serikali ingeendeelea kumwajiri huyo tabibu kwa mkataba maalum hadi hapo atakapopatikana tabibu kijana ambae ana asili ya hapohapo.

Na wakati huohuo serikali yasomesha vijana ambao wamefaulu na watokea hukohuko Mbozi waenda pale Mbeya wasomea utabibu.
 
Back
Top Bottom