Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo, Amos Makalla amesema Chama cha Mapinduzi (CCM) kinaheshimu mhimili wa Mahakama na katika usikilizaji kero za wananchi, viongozi wa chama hicho hawatajihusisha na kesi zilizopo mahakamani.
Makalla ameyasema hayo leo Jumanne Mei 7, 2024 akifanya mahojiano maalumu na waandishi na wahariri wa kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL) alipotembelea ofisi za kampuni hiyo, Tabata Relini jijini Dar es Salaam.
"Naulizwa mtangulizi wako hakuamini Mahakama na wewe unasema mnaiamini, je, tuchukue lipi? Chukueni kauli ya kwangu kwamba Chama cha Mapinduzi na Serikali yake inaheshimu Mahakama kama chombo cha kikatiba cha kutoa haki. Niwashauri wananchi kama jambo lipo mahakamani ukishindwa kata rufaa katika ngazi inayofuata," amesema.
Mwananchi
====
Pia soma:
- Makonda kusikiliza kero zenye kesi Mahakamani Arusha, asema yupo tayari kupoteza chochote mradi mtu apate haki yake
- Makalla atua Katavi na kusema Watasikiliza kero za Wananchi lakini siyo zile zilizopo Mahakamani
Makalla ameyasema hayo leo Jumanne Mei 7, 2024 akifanya mahojiano maalumu na waandishi na wahariri wa kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL) alipotembelea ofisi za kampuni hiyo, Tabata Relini jijini Dar es Salaam.
"Naulizwa mtangulizi wako hakuamini Mahakama na wewe unasema mnaiamini, je, tuchukue lipi? Chukueni kauli ya kwangu kwamba Chama cha Mapinduzi na Serikali yake inaheshimu Mahakama kama chombo cha kikatiba cha kutoa haki. Niwashauri wananchi kama jambo lipo mahakamani ukishindwa kata rufaa katika ngazi inayofuata," amesema.
Mwananchi
====
Pia soma:
- Makonda kusikiliza kero zenye kesi Mahakamani Arusha, asema yupo tayari kupoteza chochote mradi mtu apate haki yake
- Makalla atua Katavi na kusema Watasikiliza kero za Wananchi lakini siyo zile zilizopo Mahakamani