Katika makuzi yangu nilimisi sana malezi ya baba ila hakujali kuhusu sisi

Jumanne Mwita

JF-Expert Member
Nov 18, 2014
424
1,045
Katika makuzi yangu nilipitia safari ambayo sikupendezwa nayo na leo ningeomba ni share pamoja na wengine wajue siyo vizuri pia kama nao wako hivyo.

Kipekee maisha yangu ya ukuaji nilikuwa bila mapenzi ya baba ilikuwa changamoto kubwa kwangu. Ingawa baba alikuwepo kimwili, hakuwa karibu nasi kihisia, na hii iliniumiza sana.

Kupitia upendo na msaada wa mama yangu pekee, nilijifunza thamani ya familia na upendo wa kweli. Uzoefu wangu ulinifundisha umuhimu wa kuwa karibu na watoto wangu na kuwapa upendo na msaada ambao niliukosa katika utoto wangu.

Katika hayo maisha niliyoishi bila ukaribu na baba, kuna kipindi nasoma nilitamani hata siku moja baba aone mtoto wake nini anafanya shule najiweza au hamna kitu, ila nikosa huduma hiyo kwa baba angu jambo ambalo nikikaa nasononeka mno.

Ningependa kusisitiza umuhimu wa baba kuwa mwepesi na kuhusika katika maisha ya watoto wao. Nilikuwa na tamaa ya kujisikia thamani na kuthaminiwa na baba yangu, lakini nilishindwa kupata hilo.

Kupitia uzoefu wangu, nimejifunza kuwa kama wazazi, ni muhimu kuweka familia kwanza na kuhakikisha tunawapa watoto wetu upendo, msaada, na mwongozo wanahitaji. Tusiache kuonyesha upendo na kuwa karibu na familia zetu, kwa sababu ndiyo msingi wa maisha yenye furaha na imara.

Natumai hadithi yangu inaweza kuleta ufahamu na kuhamasisha wengine kufanya tofauti katika malezi ya watoto wao, ili kizazi kijacho kiweze kukua katika mazingira yenye upendo na msaada.

Stori hii inanigusa mimi kwa yale niliyokosa kwa mzazi wangu moyo huwa unaniuma mno na kuwahamasisha wengine kufanya tofauti katika malezi ya watoto wao.
 
Mmh pole sanaa mkuu, kama umesha fanikisha maisha potezea tu, wengi maisha kama hayo tumeyapitia ila baba zetu tunawapenda kawaida tu, kuna wengine wame kosa malezi ya wote mama na baba. Kama bado unapigika endelea kupambana one day yes
Simlaum kwa sasa ila najaribu kuweka stori hii kama kumbukumbu kuwa ukiwa na familia basi jali familia hata kama maisha yako siyo mazuri upendo utakaouonyesha hata kama hujiwezi utasaidia sana kwa kizazi chako kukumbuka zaidi na zaidi.
 
Simlaum kwa sasa ila najaribu kuweka stori hii kama kumbukumbu kuwa ukiwa na familia basi jali familia hata kama maisha yako siyo mazuri upendo utakaouonyesha hata kama hujiwezi utasaidia sana kwa kizazi chako kukumbuka zaidi na zaidi
Mkuu umesha anzisha familia au bado?
 
Maelezo yako hayatoshelezi. Siyo lazima baba awe anaingilia maisha yako katika kila stage; hiyo huweza kukufanya ushindwe kuwa mtu independent. Tatizo ni kuwa ulipokuwa unapohitaji msaada au ushauri wa baba ulikuwa unaupata kwa wakati au anaghairi tu.

Na alipokuwa akighairi ulikuwa unakumbusha? Wakati wengine akina mama ndio wanajiingiza sana kwenye maisha ya watoto wao na kuwafanya watoto wadhani wanakosa baba kumbe ni makosa ya hao mama kuwa too much!
 
Ukiona baba yupo hai na hayupo karibu na mtoto mara nyingi chanzo ni Mama

Mwanamke aliyesaliti agano la ndoa anakuwa nusu shetani
 
Maelezo yako hayatoshelezi. Siyo lazima baba awe anaingilia maisha yako katika kila stage; hiyo huweza kukufanya ushindwe kuwa mtu independent. Tatizo ni kuwa ulipokuwa unapohitaji msaada au ushauri wa baba ulikuwa unaupata kwa wakati au anaghairi tu. Na alipokuwa akighairi ulikuwa unakumbusha? Wakati wengine akina mama ndio wanajiingiza sana kwenye maisha ya watoto wao na kuwafanya watoto wadhani wanakosa baba kumbe ni makosa ya hao mama kuwa too much!
Changamoto huwa inaanzia hapa. Sio mda wote mtoto anaitaji msaada wa vitu vinavyo shikika tu (fedha, nguo, nk) kuna mda anaitaji emotional support ili kutengeneza bond kati yako ww mzaza na mtoto.
 
Umeizaliwa mwanaume baba wa nin we ndo baba mwenyewe acha kulialia unataka mapenz ya baba una shida mahali believe me........dada zako nao wataliaje sasa
 
Changamoto huwa inaanzia hapa. Sio mda wote mtoto anaitaji msaada wa vitu vinavyo shikika tu (fedha, nguo, nk) kuna mda anaitaji emotional support ili kutengeneza bond kati yako ww mzaza na mtoto.
Definition ya emotional support ndiyo isiyoeleweka kwa watu wengine kusababisha watoto wakue bila kujithamini kwa kuaminisha kuwa kuna kitu wanakikokosa kwenye meisha yao. Angalia watoto wa simba wanavyolelelewa, chukua mfano huo wa simba kuwa ndiyo namna ya kulea watoto wenye self confidence
 
Pole sana,mi mdingi tulikua ni kuchapana tu siku zote,nikimuona ujue kuna msala.
Ni kipigo tu..
Sasa nashangaa alivyokufa nikalia km mtoto yatima.
Vipigo vyote nimesahau.
Mpaka leo nalia kila nikikumbuka.
Mama ye tupo wote siku zote.
Nafkiriri alimlilia mmewe si chini ya miaka 15.
Iliniuma sana.
 
Back
Top Bottom