CP Awadh Haji: Watakaoleta vurugu Uzinduzi mwenge wa uhuru kukiona cha moto

Jun 20, 2023
71
83
Jeshi la polisi nchini limewahakikishia Watanzania Hali ya Amani na usalama wakati wa sherehe za Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru utakaofanyika kesho Jumanne mkoani Kilimanjaro.

Tukio Hilo la kuwasha mwenge litafanyika kwenye uwanja wa mpira wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi. Mgeni rasmi Katika sherehe hizo ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na ni tikio la pili kuwashwa kwa mwenge huo katika mkoa huo baada ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanganyika.
Kamishina wa Oparesheni na mafunzo wa jeshi la polisi nchini(CP), Awadh Haji amesema Leo mjini Moshi kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vimejipanga kuimarisha usalama Katika sherehe hizo.

Ameonya kuwa yeyote atakayeonekana kuleta vurugu atashughulikiwa ipasavyo na kutoa wito kwa wananchi kushirikiana na vyombo vya Dola kuwafichua wahalifu.

"Naomba niwahakikishie watanzania sisi jeshi la polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya Dola tumeimarisha ulinzi Katika tukio la kesho"

Pia CP Awadh alisema jeshi la polisi pia litaimarisha Hali ya usalama wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa mapema Mwaka huu pamoja na uchaguzi Mkuu hapo mwakani.

Karibuni Moshi mji wa mlima Kilimanjaro tuuwashe Mwenge wa Uhuru pamoja.
 
Huyo kamanda amekosa cha kuongea.
Hivi ni nani mwenye akili timamu atakayeenda kufanya vurugu kwenye shughuli ya kichawi ya kuwasha mwenge? Au ameongea tu ilimradi naye kaongea ili asikike?

Mwenye ni shughuli ya kishirikina hata Mungu hapendi wakimbiza mwenge

Isaya 50:11
"Tazama, ninyi nyote mwashao moto, mjifungiao hiyo mienge; endeni ninyi katika mwali wa moto wenu, na katikati ya mienge mliyoiwasha. Mtayapata haya kwa mkono wangu; mtalala kwa huzuni."

Nchi ipo kwenye huzini tangu tulipoanza kukimbiza mwenge. Tukatae hii ibada ya sanamu ya mwenge
 
Ameonya kuwa yeyote atakayeonekana kuleta vurugu atashughulikiwa ipasavyo na kutoa wito kwa wananchi kushirikiana na vyombo vya Dola kuwafichua wahalifu.
Tunajua kazi ya jeshi la polisi nchini ni kumlinda mtanzania na mali zake, kwahiyo namuomba Kamishna Awashi aupunguze vitisho.
Kuwasha mwenge ni sherehe, haijawahi tokea fujo kwenye sherehe ya aina hiyo, vitisho vya nini?
 
Jeshi la polisi nchini limewahakikishia Watanzania Hali ya Amani na usalama wakati wa sherehe za Uzinduzi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru utakaofanyika kesho Jumanne mkoani Kilimanjaro.

Tukio Hilo la kuwasha mwenge litafanyika kwenye uwanja wa mpira wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi. Mgeni rasmi Katika sherehe hizo ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na ni tikio la pili kuwashwa kwa mwenge huo katika mkoa huo baada ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanganyika.
Kamishina wa Oparesheni na mafunzo wa jeshi la polisi nchini(CP), Awadh Haji amesema Leo mjini Moshi kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vimejipanga kuimarisha usalama Katika sherehe hizo.

Ameonya kuwa yeyote atakayeonekana kuleta vurugu atashughulikiwa ipasavyo na kutoa wito kwa wananchi kushirikiana na vyombo vya Dola kuwafichua wahalifu.

"Naomba niwahakikishie watanzania sisi jeshi la polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya Dola tumeimarisha ulinzi Katika tukio la kesho"

Pia CP Awadh alisema jeshi la polisi pia litaimarisha Hali ya usalama wakati wa uchaguzi wa serikali za mitaa mapema Mwaka huu pamoja na uchaguzi Mkuu hapo mwakani.

Karibuni Moshi mji wa mlima Kilimanjaro tuuwashe Mwenge wa Uhuru pamoja.


Wakati tunasherehekea Mwenge wa Uhuru Tujikumbushe Wale Wazee waliokwenda kusign Mikataba ya Mwenge

1. Masta Forojo Ganze
2. Primus Julius Mubanga
3. Shekh Yahya Hussein
4. Mfaume Saidi Goro
5......simkumbuki kwenye Rist.

Mwl Nyerere anajua siri ya kila kitu
 
Wakati tunasherehekea Mwenge wa Uhuru Tujikumbushe Wale Wazee waliokwenda kusign Mikataba ya Mwenge

1. Masta Forojo Ganze
2. Primus Julius Mubanga
3. Shekh Yahya Hussein
4. Mfaume Saidi Goro
5......simkumbuki kwenye Rist.

Mwl Nyerere anajua siri ya kila kitu
1. Ali Tarazo.
2. Komwe wa Komwe
3. Yahaya Hussein
4. Forojo Ganze 'Master'
 
Kamanda kama huyo kweli unategemea atabadilika? Yeye muda wote ana mtazamo hasi!

Nani alete vurugu kwenye mwenge wakati maandamano ya amani yanaruhusiwa! Hao watakaoleta vurugu kwenye mwenge ni wajinga pia!
 
Tukumbuke kusafisha zile cdm MAANA tunaziacha watoto wanakuja kupuliza...
 
Back
Top Bottom