Biashara ya nafaka ina umafia mwingi. Kwa wanaotarajia kuanza kuuza nafaka chukueni tahadhari

OMOYOGWANE

JF-Expert Member
Dec 30, 2016
3,872
9,728
Nimeona mdau mmoja humu anahamasisha watu wazame bush wakanunue kwa bei ndogo walete mazao mjini wauze kwa bei kubwa ili wapige pesa.

Hili wazo ni zuri sana lakini ni vyema tupeane tahadhari. Katika biashara zenye umafia mwingi basi hii ya nafaka kwangu ndio namba moja kwa umafia yaliwahi kunikuta.

Nitatoa umafia niliokutana nao ila pia wadau wengine watakuja kuleta ushuhuda.

Miaka flani Niliwahi kuzama bush na milioni moja nikakusanya magunia ya mpunga 20 ya debe 6 yale nkaenda kukoboa kisha nkaweka kwenye fremu yangu lengo niwe nauza kwa bei ya jumla, ule mchele ulitoka vizuri mno changamoto ikawa wali wake ukipikwa hauna ladha, wateja wote wakanikimbia nikaanza kuuza reja reja kwa bei ndogo lakini bado wakanikimbia walikuja mwanzo mwanzo kisha wakaishia mitini.

Baada ya kufanya uchunguzi nikagundua niliuziwa mpunga uliokaa miaka mingi stoo (kumbuka niliununulia bush) pia ile mbegu ya huo mpunga hutoa kilo nyingi lakini wali wake hua hauma radha. Niliuza kwa bei ya hasara mzigo wote kwa wauza vitumbua.

Nkajipanga tena awamu hii nkaamua niende mashineni nikanunur mzigo kwa bei chee kisha niuze kwa bei ya hapo mtaani. Nilinunua kilo 500 kufikisha mzigo kwenye fremu wateja wakafurika nkauza sana hiyo siku. Nashangaa jioni watu wanarudisha mchele wanadai unamawe meupe. Kuuangalia vizuri ni yale mawe meupe wahuni walinipiga walaaniwe sana washenzi wale. Wateja wote wakanikimbia.

Nkajipanga tena nafika mashineni kuchukua mzigo nakutana na madalali wengi sana nkaona hii biashara pasua kichwa nkaachana nayo

Kwa mlio wahi kukumbana na umafia kwenye nafaka njooni hapa mtoe ushuhuda.
 
Biashara yoyote ile huwa na changamoto zake. Walanguzi wengi sio waamifu. Hata wauza nguo nao wakikusimulia changamoto zao unaweza kukimbia. Mtu anafungua mzigo anaku tana na nguo za ndani za watoto wakati yeye aliagiza suruali.

Ukishaamua kuwa mfanyabiashara, anza kwanza kwa kufanya utafiti na kujifunza pia kwa waliokutangulia ambao ni waamifu. Maana ukikutana na tapeli watakuingiza chaka.
 
Huo sio umafia ni upuuzi.

Siku nilipojua kwamba mawe yanawekwa ktk mchele ili kuzidisha kilo,na mchele unapakwa mafuta ili ung'ae kuonekana ni mpya,nilijiskia aibu sana kuwa mbongo.

Kuna vitu vya kijinga vinatugharimu sana hasa mbele huko katika masoko ya watu makini, nimekumbuka story ya wanunuzi wa pamba kukuta mawe ktk marobota🤮🤮🤮
 
Biashara yoyote ile huwa na changamoto zake. Walanguzi wengi sio waamifu. Hata wauza nguo nao wakikusimulia changamoto zao unaweza kukimbia. Mtu anafungua mzigo anaku tana na nguo za ndani za watoto wakati yeye aliagiza suruali.

Ukishaamua kuwa mfanyabiashara, anza kwanza kwa kufanya utafiti na kujifunza pia kwa waliokutangulia ambao ni waamifu. Maana ukikutana na tapeli watakuingiza chaka.
Nimeipenda hii
 
Nimeona mdau mmoja humu anahamasisha watu wazame bush wakanunue kwa bei ndogo walete mazao mjini wauze kwa bei kubwa ili wapige pesa.

Hili wazo ni zuri sana lakini ni vyema tupeane tahadhari. Ktk biashara zenye umafia mwingi basi hii ya nafaka kwangu ndio namba moja kwa umafia yaliwahi kunikuta.

Ntatoa umafia niliokutana nao ila pia wadau wengine watakuja kuleta ushuhuda.

Miaka flani Niliwahi kuzama bush na milioni moja nkakusanya magunia ya mpunga 20 ya debe 6 yale nkaenda kukoboa kisha nkaweka kwenye fremu yangu lengo niwe nauza kwa bei ya jumla, ule mchele ulitoka vizuri mno changamoto ikawa wali wake ukipikwa hauna radha, wateja wote wakanikimbia nkaanza kuuza reja reja kwa bei ndogo lakini bado wakanikimbia walikuja mwanzo mwanzo kisha wakaishia mitini.

Baaba ya kufanya uchunguzi nkagundua niliuziwa mpunga uliokaa miaka mingi stoo (kumbuka niliununulia bush) pia ile mbegu ya huo mpunga hutoa kilo nyingi lakini wali wake hua hauma radha. Niliuza kwa bei ya hasara mzigo wote kwa wauza vitumbua.

Nkajipanga tena awamu hii nkaamua niende mashineni nikanunur mzigo kwa bei chee kisha niuze kwa bei ya hapo mtaani. Nilinunua kilo 500 kufikisha mzigo kwenye fremu wateja wakafurika nkauza sana hiyo siku. Nashangaa jioni watu wanarudisha mchele wanadai unamawe meupe. Kuuangalia vizuri ni yale mawe meupe wahuni walinipiga walaaniwe sana washenzi wale. Wateja wote wakanikimbia.

Nkajipanga tena nafika mashineni kuchukua mzigo nakutana na madalali wengi sana nkaona hii biashara pasua kichwa nkaachana nayo

Kwa mlio wahi kukumbana na umafia kwenye nafaka njooni hapa mtoe ushuhuda.
Mkuu, hakuna biashara isiyo na changamoto hasa hizi ukiwa Bongo. Hii ni kwa sababu kila mtu haaminiki. Wewe ulikata tamaa mapema sana kwani changamoto kama hizo ndizo zinakufanya ukomae kwenye biashara. Labda mtaji ulikuwa mdogo.
 
Biashara yoyote ile huwa na changamoto zake. Walanguzi wengi sio waamifu. Hata wauza nguo nao wakikusimulia changamoto zao unaweza kukimbia. Mtu anafungua mzigo anaku tana na nguo za ndani za watoto wakati yeye aliagiza suruali.

Ukishaamua kuwa mfanyabiashara, anza kwanza kwa kufanya utafiti na kujifunza pia kwa waliokutangulia ambao ni waamifu. Maana ukikutana na tapeli watakuingiza chaka.
Pole sana, nikupe mbinu ya kwanza ukitaka kununua mpunga, lazima ufanye sample.

Fungua pekecha na kiganja kisha tafuta utajua huu ni mchele Mpya Au wa zamani.

Fanya random sampling kwa kila unachonunua ili uwe salama.
 
Huo sio umafia ni upuuzi.

Siku nilipojua kwamba mawe yanawekwa ktk mchele ili kuzidisha kilo,na mchele unapakwa mafuta ili ung'ae kuonekana ni mpya,nilijiskia aibu sana kuwa mbongo.

Kuna vitu vya kijinga vinatughalimu sana hasa mbele huko ktk masoko ya watu makini,nimekumbuka story ya wanunuzi wa pamba kukuta mawe ktk marobota
Mchele guwa unapakwa mafuta ili usiharibile,kupungua siyo kungara bwana wewe
 
Hata biashara ya wanyama ni mbaya. Niliwahi kununua Ng'ombe Mia kutoka Mbeya kwa ajili ya kuja kuuza Dar.

Kufika Iringa nikakuta Ng'ombe wote wamekonda.

Sijui wale wahuni waliwapiga sindano wale.

Kufikika Kibaha nilikokuwa napaki 21 wakafa.
 
Back
Top Bottom