Habari,
Nimeona tangazo Mtandaoni linadaiwa kutolewa na NEC, kwamba wametangaza nafasi za kazi ya uandishi wa daftari la kudumu la wapiga kura Mwaka 2024. Kinachonipa wasiwasi naona kama tovuti hii si rasmi.
Ukweli wake upoje?
Nimeona barua inasambaa Mtandaoni ikisema NECTA inaratibu zoezi la Kurekebisha Makosa ya majina kwenye vyeti vya Mwaka 2000-2023 kwa Malipo.
Barua hii inanipa mashaka sana, JamiiCheck nisaidieni kuhakiki.
Habari,
Kumekuwa na hoja mtaani inadai kwamba ikitokea upo porini na ukahisi harufu ya wali au mchele unapaswa kuchukua tahadhari kwani ni ishara kuwa chatu yupo karibu na anatoa harufu hiyo kukuvuta.
Je, kuna ukweli kuhusu hoja hii? Tunaomba ufafanuzi.
Katika mitandao ya kijamii nimeona video inayohusishwa na Rais Mpya wa Senegal, Bassirou Diomaye Faye, akikemea Ufaransa kuwa ni wakati wa kuondoka bara la Afrika.
Video hiyo inamuonesha Rais Faye akiimbia Ufaransa kuwa "Inakuwa wakati wa Ufaransa kuinua magoti yake kutoka shingoni mwetu na kumaliza ukandamizaji huu usio wa haki. Karne nyingi za mateso, biashara ya binadamu, ukoloni, na ukoloni mamboleo vimesababisha mateso yasiyohesabika. Ni wakati wa kumaliza mzunguko huu wa ukandamizaji,"
Wachangiaji wengi kwenye video hizo zinazozunguka mitandaoni walionesha furaha kwamba Rais Faye ameonesha msimamo imara dhidi ya Ufaransa kulikandamiza bara la Afrika.
Video hiyo inanipa mashaka.
Picha hii inadaiwa kuwa ya Rais Mteule wa Senegal, Diomaye Faye akiwa na mke wake.
JamiiCheck naombeni ufafanuzi maana nimewahi kuiona sehemu fulani sikumbuki ni wapi, lakini ilikuwa inamzungumzia mtu mwingine kabisa.
Nani asiyemjua mbabe Simba mfalme wa nyika? Yaani ukutane naye paaah! Utamzame machoni aone aibu na kuondoka? Bado siamini hili jambo naona hawa vijana wa ovyo wanataka kuniingiza chaka siku nikikutana naye mbashara nisichukue njia nyingine za kujiokoa eti nimtizame.
Hivi kweli Simba huyu kweli wa kumwonea aibu binadamu kisa kumuangalia machoni ana kwa ana kwa ujasiri.
Wakuu naombeni taarifa sahihi kuhusu hili jambo, huenda mada ikawa kichekesho lakini hili jambo linasemwa sana mtaani.
Salaam ndugu zangu,
Nimekutana na video ya kusikitisha ikimuonesha raia anayesemekana kuwa ni raia wa Tanzania Bara akichapwa viboko na Raia wa Zanzibar kwa kosa la kula mchana wa Ramadhani. Je video hiyo ni ya mwaka huu?
Kuna picha nimeona Rais Mstaafu wa Marekani, Barack Obama akizindua uidhinishaji wake wa mwisho wa mgombea urais 2022 nchini Kenya ambapo alionesha wazi kumuunga mkono Naibu Rais Ndugu William Ruto.
Barack Obama ana vinasaba vya Ujaluo, sijui ilikuwa vipi akashindwa kumuunga mkono Mjaluo mwenzio Mwamba Raila Amolo Odinga.
Chanzo: BBC
===
Video halisi iliyotumika kutengeneza picha hiyo
Mara nyingi nikiwa na stress na kupelekea kukosa usingizi, huwa navuta sigara ili kupunguza stress hizo. Hata iwe usiku wa manane nitajitahidi niende kwenye Club zinazokesha nikafuate sigara.
Suala la kuwa inanisaidia au lah, sidhani lakini pale napokuwa navuta huwa nakuwa katika hisia nyingine kabisa. Chanzo cha kutumia sigara kama relief ya stress, ni baada ya kuona kwenye muvi mara kwa mara, na ushauri kutoka kwa marafiki.
Nachotaka kujua kitaalam ni kama kweli sigara inasaidia kupambana na msongo wa mawazo tunaokumbana nao mara kwa mara.
Kumekuwepo na barua inayiosambaa Mtandaoni ikionesha kuandikwa na Mfalme Mswati III ametoa tangazo linalodai kuwa kutokana na uhaba wa Wanaume kwenye nchi yake, amewaomba wananchi wanaoishi Kusini mwa Jangwa la Sahara kuomba uraia kwenye nchi yake, na kila mwanaume atayeoa walau wanakwake 5 atamlipia gharama za harusi zao pamoja na kuwanunulia nyumba.
Ukweli wa taarifa hii upoje?
Katika pitapita mitandaoni nimekutana na huyu chawa wa Mtoto wa Rais Museveni, Kainerugaba Muhoozi akimtuhumu Kakwenza Rukira kuingia makubaliano ya siri na umoja wa Ulaya nchini Uganda katika kuhamasisha ushoga nchini humo.
Nakumbuka Uganda imezuia mahusiano ya jinsia moja na Rais Museveni amebana kweli kweli wazungu hawana pa kupumulia, naona wameamua kupitia njia za panya kuleta ushenzi wao.
Video hii kwenye Facebook imeeleza kuwa Naibu Rais wa Kenya Rigathi Gachagua amesema kuwa Rais William Ruto alimsaliti kwa kukutana na kinara wa upinzani Raila Odinga nchini Uganda.
Video hiyo ilikuwa na ujumbe kuwa “Ruto amenisaliti! DP Gachagua anazungumza baada ya Ruto na Raila kukutana Uganda jana,”
Mimi ni mmoja wa watoto waliotungwa mimba wakati mzazi bado ananyonyesha, bahati mbaya aliyenitangulia alifariki dunia kabla sijazaliwa. Hivyo wakati nakua niliambiwa na majirani kuwa kutungwa kwangu mimba kulisababisha afya ya dadangu kudhoofu na kupelekea kifo.
Hili suala ni kweli au vihoja na vijambo vya walimwengu.
RIP dada yangu Koku.
Habari Wadau,
Nimekutana na tangazo la kazi likionesha kuwa Kampuni ya usafirishaji ya Tilisho inahitaji Wafanyakazi kwa nafasi ya Wakatisha Tiketi na wahudumu wa ndani ya Mabasi.
Nimepata mashaka baada ya kuona ukilifuata tangazo hili ndani yake linahitaji usambaze link kwenye magroup ya WhatsApp na Facebook ili kuendelea hatua inayofuata.
Je, kuna ukweli juu ya Tangazo hili?
Habari,
Kuliwahi kutokea madai yakisema kuwa Olduvai Gorge ipo nchini Kenya. Rosemary Odinga alisema Olduvai Gorge ipo Kenya, Tazama video hapa chini:
Je, mnaweza kutusaidia kuweka kumbukumbu sawa hili?
Kumekuwepo na taarifa inayosambaa mtandaoni ikionesha kuwa mfuko wa Taifa wa bima ya Afya (NHIF) umerejesha mpango wa kusajili watoto kupitia kifurushi cha Toto Afya Kadi.
Taarifa hii ina ukweli kiasi gani maana naona kuna mvutano mkubwa, baadhi wanadai ni kweli na wengine wanasema si kweli.
Nimeona ujumbe wa WhatsApp unaotaka watu watume majina ya Wagonjwa wa Saratani ya Matiti kabla ya Machi 7 ili watibiwe bure.
Nina ndugu yangu ni mgonjwa. Naomba kufahamu kama tangazo hili lina ukweli ili nisitapeliwe bure.
ATTENTION!
Medical research authority of the US have found new cancer in human being caused by silver nitro oxide.
Whenever you buy recharge cards dont scratch with nails as it contains
silver nitro oxide coating and can cause skin cancer.
Share this msg with your loved ones.
---
Naye Bata batani mwaka 2012 aliuliza:
Here it is, kwanza
1. Kadanganya Miaka yake kwa wikipedia today changed his age 32 To 26
2. Anatafutwa as an international fugitive.
3. Out of all players, wameenda kwa mtu ana history ya ubakaji. Why?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.